Luigi Mangione
JF-Expert Member
- Jan 2, 2024
- 568
- 1,028
N
Nyonga hao kuluna mpaka akili ikawe sawaKongo imelaaniwa, tangu wapate Uhuru hawajawahi kupata utulivu. Dalili kuu ya mtu au Taifa lililolaniwa ni kukosa utulivu.
View attachment 3202870
DRC nchi iliyojaa madini. Kuna sehemu ukiingia msituni kabisa huko ukichota mchanga gunia 1 unaweza kupata pure gold debe moja lakini kwasababu ya laana iliyotokana na ardhi kushiba damu za watu hayo madini hayajawahi kuwa na mchango wa maana kwa wananchi.
DR Congo kuna ufukara uliokithiri. Kongo kuna nuka damu.
Viongozi nao shetani kawaziba macho wanadhani kutumia upanga kutalituliza Taifa. Juzi wameuwawa kikatili vijana wadogo (panya road) 102 na wengine wanatarajiwa kunyongwa kikatili pia soon.
Ni unyama, unyama na ushetani.
Wanadhani wanaliponya Taifa kumbe wanalinywesha damu zaidi lizidi kulaaniwa.