Dada huyu anaomba Msaada wenu kimawazo .....

Dada huyu anaomba Msaada wenu kimawazo .....

Mkwe sasa huyu mwanamke mbona anacheza na moto kwanini asimwambie mumewe mambo yatakapokuja kufumuka itakuja kum-cost sana maana itaonekana alikuwa anaficha siri wakati inawezekana sio hivyo ni bora akamwambia once and for all ili waone inakuwaje ikiwezekana wakutane maana haya masuala ya kupigiwa na kutumiwa message saa nane za usiku ili hali wewe ni mke wa mtu inatia shaka maana mwanaume akigundua anaweza kuja na conclusion kuwa mkewe ana mahusiano na mwanaume mwingine so its best akamwambia na wakakaa chini wakayamaliza maana hiyo ndio njia itakayoondoa usumbufu.

Mkwe naomba ujifunze sawa eeeh matatizo yako usijebebesha wengine mkwe wangu.
Unaendeleaje lakini?
 
Mahawara huwa hawaachani.

Babu anaweza kuapa!
 
Kwa mtazamo wangu nikiwa kwenye ndoa ,Najua haya maisha yana leo na kesho na hasa ukizingatia huyu dada kazaa na huyo X- wake kuna leo na kesho kuwa na mawasiliano si mbaya,Kwani inawezekana mtoto akapata tatizo ambalo baba yake anaweza kufahamishwa kwa namna moja au nyingine ,
Lakini huyu mwanaume si muungwana hata kidogo kwa nn amsumbue mwenzake wakati tayari anajua yuko kwenye ndoa yake ? hili nalo wanaume inabidi mjifunze kuwa makini kama maisha yamekuchanganya kwa nini ubebeshe lawama kwa mtu asiyehusika.?:sick:
Kama wengi walivyoshauri ni vyema dada huyu atafute namna ya kukaa na mmewe na kumweleza linalomkabili ingawa ,inawezekana pia mwanzo mme anaweza asimuelewe kwa sababu za wivu wa mapenzi lakini muda unavyokwenda atamuelewa mkewe .
kama alivyosema Michelle kwa nini anawasiliana na X wake
Dada anadai X-wake alimpigia simu akiwa kazini na kuanza kumweleza mlolongo wa matatizo kama binadamu alimsikiliza na mpaka mwisho kabisa alimweleza hataweza kumpa msaada wowote kwani yeye yupo kwenye ndoa na maamuzi yote wanafanya na mmewe
Ndipo alipoanza kuambiwa akumbuke fadhira.:coffee:
Huyu madame anasoma post hizi na imani atayafanyia kazi kabla ndo hii haijaingia matatani
Mungu ni mwema

Ingekuwa ndo mimi siku hiyo ananieleza hayo mambo ningemwambia hivi, dunia hii ni kubwa na pana sana, anao ndugu zake na rafiki zake na jamaa zake hao msaidie yeye halafu mimi nitaendelea kumpa msaada wa kumlelea mtoto wake!! Basiii!!!

Mi mwanaume aliyenitenda tena nikiwa na kiumbe chake, halafu Mungu anijalie nipate Mume mwema hata arudi na gorofa na sisi na mme wangu tunalala kwenye banda namtoa nduki!! Achilia mbali huyo anarudi na shida??
 
Kwa mtazamo wangu nikiwa kwenye ndoa ,Najua haya maisha yana leo na kesho na hasa ukizingatia huyu dada kazaa na huyo X- wake kuna leo na kesho kuwa na mawasiliano si mbaya,Kwani inawezekana mtoto akapata tatizo ambalo baba yake anaweza kufahamishwa kwa namna moja au nyingine ,
Lakini huyu mwanaume si muungwana hata kidogo kwa nn amsumbue mwenzake wakati tayari anajua yuko kwenye ndoa yake ? hili nalo wanaume inabidi mjifunze kuwa makini kama maisha yamekuchanganya kwa nini ubebeshe lawama kwa mtu asiyehusika.?:sick:
Kama wengi walivyoshauri ni vyema dada huyu atafute namna ya kukaa na mmewe na kumweleza linalomkabili ingawa ,inawezekana pia mwanzo mme anaweza asimuelewe kwa sababu za wivu wa mapenzi lakini muda unavyokwenda atamuelewa mkewe .
kama alivyosema Michelle kwa nini anawasiliana na X wake
Dada anadai X-wake alimpigia simu akiwa kazini na kuanza kumweleza mlolongo wa matatizo kama binadamu alimsikiliza na mpaka mwisho kabisa alimweleza hataweza kumpa msaada wowote kwani yeye yupo kwenye ndoa na maamuzi yote wanafanya na mmewe
Ndipo alipoanza kuambiwa akumbuke fadhira.:coffee:
Huyu madame anasoma post hizi na imani atayafanyia kazi kabla ndo hii haijaingia matatani
Mungu ni mwema

Uko sahihi FirstLady1 unaposema kuwa kama mtu aliyezaa nae (huyo dada) anapaswa kuwasiliana na mzazi mwenzake..hiyo mimi naikubali kabisa,ishu ni kwamba kwa nini amesita kumweleza mumewe right away?maana kauli ya mwishi aliyoitoa kwa mzazi mwenzke kuwa yeye sasa yuko kwenye ndoa na maamuzi wanatoa pamoja yeye na mumewe ilikuwa kauli thabiti na sahihi,nini kimempa kigugumizi cha kumweleza mumewe mpaka aombe msaada?..Anapaswa kuliweka wazi kwa mumewe kuanzia hapo naamini kila kitu kitakwenda sawa.
 
Mi naona huyu dada hana msimamo. Mtu alikuacha zamani, ukahangaika na hatimaye Mungu akakushushia mana... unataka kuila jangwani? Wala usibadili namba yako ya simu.. mwambie mumeo yanayokusibu. Huyo X-wako kama angekuwa na busara na anajuta kweli wala asingekughasi namna hiyo. Huyu ni mchfuzi wa ndoa za watu. Alishakuona nyani.. je sasa umekuwa tumbili? Huyo ni shetani katika sura ya binadamu, mkatae kwa nguvu zako zote.

Mentee umeongea yaliyomo moyoni mwangu huyo dada hana msimamo kabisa, haiwezekana ifikie hatua ex wako ambae hajawahi hata kutunza mtoto wake akupigie simu usiku wa manane, sasa huo usiku ndio anataka msaada gani jamani? Huyo anataka kumuharibia ndoa huyo dada amini nawaaambia cause hata kama angekua anatunza mtoto mtu mwenye busara zake hawezi kupiga simu usiku wakati anajua dada wa watu ameolewa zake, hata kama ni huruma huyo ex wake hana huruma na huyo dada na nia yake ni kumuharibia mazima hafai hata kupewa msaada wa shilingi mia kwani hana adabu. Hiyo ingenikuta mimi ningeimaliza kwa muda wa siku 3 tu bila kuhitaji msaada. Dada awe na msimamo na amaanishe anachokisema kwa maneno na matendo mimi naamini akiwa serious kwamba haitaji mchezo na ndoa yake huyo mwanaume atakua na adabu tu ila inaonyesha anamuonyesha vijihuruma visivyo na msingi sasa asubiri kuachika kama mtu alishindwa kuhudumia damu yake ukiachika halafu una mtoto mwingine tayari ndio utapata habari kamili
 
Kyabushaija cha msingi nenda kama uko karibu nenda kawasaidie misaada wanayohitaji nadhani utakuwa umefanikisha kwa karibu
Asante

Umemwambia ukweli aende akasaidie sio kudiscuss bila msaada "MAISHA LAZIMA YAENDELEE NO MATTER WHAT"
 
Can we diskasi about Gongo la Mboto pls?

Tudiscus nini sasa umeshapeshapeleka mchango wako??
Ningekuelewa kama ungesema hata jamani tujipangeni MMU tufanye kitu kwa ajili ya wenzetu gongo la Mboto!!
 
Sasa kama ameolewa kwa nini asimwambie mme wake hilo suala? Yeye amwambie mme atapima siyo kufichaficha. Sasa ukijulikana na hakuwahi kumwambia itakuwaje? Lazima awe muwazi kwani alikuwa anafaidi enzi hizo sasa kwa nini domo liwe zege.
 
Back
Top Bottom