Dada wa kazi za ndani na utapeli mpya mjini

Dada wa kazi za ndani na utapeli mpya mjini

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2021
Posts
590
Reaction score
1,648

Habari wakuu,

Kumekua na hii tabia inayokuwa kwa kasi inayofanywa na wadada wanaofanya kazi za nyumbani. Tabia ambayo imegharimu na inaendelea kuwagharimu watu, hivyo wanajamvi muwe makini na watu hawa mnaowachukua kwa lengo la kusaidia kazi za nyumbani.

Iko hivi, utakuwa na uhitaji wa kupata mtu wa kusaidia kazi hapo nyumbani, utatafuta huku na huko utapata mtu, utaambiwa mtu kapatikana sehemu fulani, utatuma nauli muhusika anafika. Baada ya muda fulani kati ya wiki hadi mwezi mmoja yule binti anaiba hapo nyumbani kwako chochote kitakachokuwa karibu (hasa pesa, sababu atakuwa ameshasoma mchezo wote hapo nyumbani na anajua hela zinakaa wapi) na kuondoka kurudi kwao.

Wewe baada ya kuibiwa utapiga simu kwa wazazi au walezi wake na kuwapa taarifa kwamba binti yao amekuibia kiasi kadhaa na ametoroka kurudi kwao unataka vitu vilivyoiba virudishwe, hapa ndipo meza inapogeuzwa.

Wazazi watakwambia kwanza mtoto wao hajafika nyumbani hivyo hiyo kesi ipo kwako, halafu umemtorosha mtoto wao wakati bado ni mwanafunzi. Wewe utaogopa kuwa na kesi ya kumtorosha na kumkatisha masomo binti yule hivyo unakaa kimya yaishe, huku nyuma mpango wao umefanikiwa wanatafuta mtu mwingine wa kumuingiza mjini.

Kuna ambaye alijiongeza akapiga simu kwa majarini ambapo alimchukua binti huyo na kuambiwa kuwa binti ameshafika nyumbani. Baada ya kutoa mikwara miwili mitatu pesa alizoiba huyo binti zikarudishwa kwa muhusika.

Hivyo watu muwe makini na mnapopata wadada hawa wa kazi, wengine wanakuja na mikakati yao kabambe wakishirikiana na wazazi/walezi wao, wanasubiri atakayejitokeza wamuingize mkenge.​
 
Na una bahati ningekukamata ungenijua mimi ni nani! Hivi unacheza na mimi wewe?
 
Nlikaaa na binti wa kazi kama mdogo angu kabiss,kuanzia nguo za ndani viatu kuuguaangio za skukuu mpaka simu aliyokuwq anatumia baba ake mzazi nlinunua mm,vyombo nlivokuwa napata kwny kikoba tuligawana nusu kupeleka kwao,hapo bado jdugu zake likizo walikuwa wanakuja kupumzika kwangu aloo kapata mimba kachukia kazi suku ya kuondoka kaniibia,nlivunjika moyo labiss na mabinti wa kazi nkampata mmoja kaja kakaa wiki alikuwa mdokozi balaa anadokoa mboga balaa aliwahi kula kuku nusu peke ndani ya wiki kanga kuondoka nkampata mwingine anafanya kazi vizuri ila hayuko familiar na watoto nkaona sio shida hee kakaa wiki kaseema baba ake kamuita..from there sikutaka kukaa tena na binti wa kazi japo mjamzito nakomaa dukani mwenyew nyumbani mwenyew napangilia kazi zangu vizuri na mr anatoa support maisha yanaenda sina ham na hao watu nlijifunza hata uishi nao vipi hawana weka wala shukran
 
Hawa wafanyakazi za ndani wanatumiwa/tumika kutapeli kwa njia tofauti.Kuna hawa watu wanaoagiza ma house girl kutoka mikoani.Ànakwambia nipe nauli nikuagizie msichana kutoka Iringa.Unampa, kweli baada ya muda msichana analetwa,anafanyakazi wiki moja au mbili, anakwambia nimepigiwa simu nimefiwa na ndugu wa damu au mzazi hivyo natakiwa kwenda msibani,unamruhusu, kumbe siyo kweli.Yule aliye mleta keishachukua nauli kutoka kwa mtu mwingine ambaye naye alimwambia kuwa ampe nauli ili amtafutie msichana wa kazi hivyo anapotoka kwako anapelekwa sehemu nyingine.Mchezo unakuwa Ni huohuo.
 
Nlikaaa na binti wa kazi kama mdogo angu kabiss,kuanzia nguo za ndani viatu kuuguaangio za skukuu mpaka simu aliyokuwq anatumia baba ake mzazi nlinunua mm,vyombo nlivokuwa napata kwny kikoba tuligawana nusu kupeleka kwao,hapo bado jdugu zake likizo walikuwa wanakuja kupumzika kwangu aloo kapata mimba kachukia kazi suku ya kuondoka kaniibia,nlivunjika moyo labiss na mabinti wa kazi nkampata mmoja kaja kakaa wiki alikuwa mdokozi balaa anadokoa mboga balaa aliwahi kula kuku nusu peke ndani ya wiki kanga kuondoka nkampata mwingine anafanya kazi vizuri ila hayuko familiar na watoto nkaona sio shida hee kakaa wiki kaseema baba ake kamuita..from there sikutaka kukaa tena na binti wa kazi japo mjamzito nakomaa dukani mwenyew nyumbani mwenyew napangilia kazi zangu vizuri na mr anatoa support maisha yanaenda sina ham na hao watu nlijifunza hata uishi nao vipi hawana weka wala shukran
Unapo mfanyia wema ndio anapanga baya tena

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Hawa wafanyakazi za ndani wanatumiwa/tumika kutapeli kwa njia tofauti.Kuna hawa watu wanaoagiza ma house girl kutoka mikoani.Ànakwambia nipe nauli nikuagizie msichana kutoka Iringa.Unampa, kweli baada ya muda msichana analetwa,anafanyakazi wiki moja au mbili, anakwambia nimepigiwa simu nimefiwa na ndugu wa damu au mzazi hivyo natakiwa kwenda msibani,unamruhusu, kumbe siyo kweli.Yule aliye mleta keishachukua nauli kutoka kwa mtu mwingine ambaye naye alimwambia kuwa ampe nauli ili amtafutie msichana wa kazi hivyo anapotoka kwako anapelekwa sehemu nyingine.Mchezo unakuwa Ni huohuo.
Hatari tupu

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Hawa wafanyakazi za ndani wanatumiwa/tumika kutapeli kwa njia tofauti.Kuna hawa watu wanaoagiza ma house girl kutoka mikoani.Ànakwambia nipe nauli nikuagizie msichana kutoka Iringa.Unampa, kweli baada ya muda msichana analetwa,anafanyakazi wiki moja au mbili, anakwambia nimepigiwa simu nimefiwa na ndugu wa damu au mzazi hivyo natakiwa kwenda msibani,unamruhusu, kumbe siyo kweli.Yule aliye mleta keishachukua nauli kutoka kwa mtu mwingine ambaye naye alimwambia kuwa ampe nauli ili amtafutie msichana wa kazi hivyo anapotoka kwako anapelekwa sehemu nyingine.Mchezo unakuwa Ni huohuo.
Hii ilishawahi kutokea nyumbani kwangu, binti aliletwa na mtu aliyejitambulisha kuwa ni shangazi yake. Huyo shangazi tuliunganishwa na family friend.
Binti alikuja kweli na alikuwa anafanya kazi vizuri tena sana. Tulimpenda na tukampokea kama mwanafamilia. Baada ya miezi miwili shangazi mtu akatupigia simu kuwa binti kafiwa na bibi ya mzaa mama hivyo inabidi asafiri kwenda msibani. Hatukuwa na hiyana tulimwandalia nauli na zawadi za nyumbani. Wakati anaondoka tulishangaa anabeba karibu nguo zake zote wakati tuliambiwa kuwa anaenda kukaa wiki tu.
Shangazi mtu akamchukua na kuondoka naye, baada ya siku mbili tu tangu aondoke binti akapiga simu kuwa anataka kurudi wife akamuuliza msiba umeisha? Binti akasema kavu kavu sikwenda shangazi alidanganya. Kwa hiyo uko wapi akasema yuko sehemu xx shangazi alimpeleka kufanya kazi lakini yeye anataka arudi kwetu.
Tukamuuliza unataka kurudi lini? Yeye akasema hata kesho. Wife akamuuliza na hapo kazi itakuwaje. Akasema wazi yeye ameshawaambia kuwa amedanganywa kuwa anaenda nyumbani kwenye msiba kumbe analetwa kufanya kazi sehemu nyingine kwa yeye anaomba arudi kule alikokuwa awali. Basi wakaridhia.
Basi binti akamwelekeza wife akaenda akamchukua, uzuri familia ile hawakuwa na hiana japo walihuzunika sana kwa sababu yule mama alikuwa anafahamiana na yule shangazi mtu...
Ajabu sasa shangazi mtu alivuta hela ya nauli na mshahara wa mwezi mmoja eti wazazi walitaka wawachie huko kwa kijijini. Nauli 40,000+ ujira 60,000/.
Shangazi mtu alipopigiwa simu hakupokea. Wife alikuwa yuko tayari kumrejeshea yule mama kiasi alichompa shangazi mtu ili kumaliza mgogoro. Yule mama alisema haina haja yeye kwa sababu anamfahamu shangazi mtu atambana atarudisha hiyo pesa.
Yule binti tulidumu naye sana, wife amfadhili kusoma ushonaji, akawa anashona akiwa anatokea kwetu, baadaye alipata mchumba akaolewa mimi nikasimama shughuli zote za send off. Mpaka leo binti huyo anakuja nyumbani kama amekuja kwa wazazi wake.
 
Back
Top Bottom