KERO Dada yangu amefariki kwa kuishiwa Oxygen baada ya Muhimbili kufosi kumpeleka Mloganzila

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Nilikuwa na mgonjwa wangu ambaye alikuwa anasumbuliwa na Saratarani, alikuwa anapatiwa huduma Ocean Road, tukiwa hapo tukapata referral ya kwenda Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (Upanga), Dar es Salaam.

Wakati tunaelekea Muhimbili tukapita Hindu Mandal kwa kuwa kuna Daktari ambaye pia tulihitaji kumuona, wakati tukiwa hapo tukapata huduma nzuri tu ya muda.

Tukapatiwa Ambulance iliyotupeleka hadi Muhimbili, wakampokea vizuri mgonjwa na kumpa huduma mbalimbali.

Muda mfupi baadaye wakatuambia kuwa tunatakiwa kulipia chumba kwa gharama ya Shilingi 50,000, pale Mwaisela, huku akiwa anaendelea kupatiwa matibabu ikiwemo kupewa Oxygen kwa kuwa mgonjwa alionakana ana shida ya kupumua.

Baada ya kulipa, wakatuambia hakuna vitanda hivyo wanataka kutupeleka Hospitali ya Mloganzila.
Sisi tukakataa, muda huo ni saa kumi alfajiri, tukawambia tunaomba kama kweli hakuna kitanda basi mgonjwa abaki pale ‘Emergency’ hadi asubuhi kwa kuwa tayari tulishalipia chumba na kuanza kuangaika n ambulance kuelekea Mloganzila wakati tumeshafanya vipimo na taratibu nyingine itakuwa ni usumbufu na pia sio njema kwa mgonjwa.

Ukatokea ubishani pale, sisi tukakataa, lakini Madaktari wa Muhimbili waliokuwepo wakafanya maamuzi ya kibabe wakasema mgonjwa wetu anaingizwa kwenye Ambulance kupelekwa Mkoganzila.

Wakati wakifanya maamuzi hayo, kuna Nesi mmoja akasema “fanyeni haraka Oxygen inaisha”.

Walipofika Kimara, ndugu yetu aliyekuwa kwenye Ambulance akanijulisha kuwa Oxygen imekata, hadi wanafika Mbezi tayari Oxygen ilikuwa imeshakata na mgonjwa wangu akafariki.

Inawezekana ni siku yake ilikuwa imewadia lakini kilichotokea ni uzembe wa baadhi ya Madaktari wa Hospitali ya Muhimbili na watendaji wengine kadhaa waliokuwepo.

Kwanza najiuliza kwanini walitulipisha kitanda wakijua hakuna kitanda, pili kwanini walimwekea mgonjwa Oxygen kidogo na kwa kauli iliyotolewa pale ni wazi walijua hiyo haitamfikisha Mgonjwa Mloganzila.

Tatu kulikuwa na haja gani ya kumpeleka Mloganzila wakati tayari kulikuwa kunaelekea kukucha na mmoja wa Madaktari aliwaambia wenzake tubaki pale lakini wenzake hawakumsikiliza.



Ambulance iliyombeba dada yangu.
Baada ya msiba nilipouliza mmoja wa Madaktari wa Muhimbili kwanini walitupa Oxygen kidogo anadai lile lilikuwa jukumu la watu wa Ambulance kukagua na sio jukumu lao.

Walichokifanya Madaktari hao wa Muhimbli waliokuwa zamu Usiku wa tukio hakikuwa cha kibinadamu na kama wanafanya hivi basi maisha ya watu wengi yapo hatarini.

Kwa nini nimewasilisha malalamiko yangu hapa JamiiForums, nataka Dunia ijue kuwa kuna baadhi ya Watumishi wa Muhimbili wanatakiwa kujirekebisha, najua roho ya dada yanu haiwezi kurudi ila basi angalau wasingetuonesha wazi kuwa wanataka ndugu yetu afe, pia iwe somo kwa wengine wawe makini.

Miamala ya malipo tuliyofanya kabla ya Mgonjwa kulazimishwa kupelekwa Mloganzila
 
Hii hospitali ina ujinga mwigu sana, wanaendesha mambo yao kimaokoto maokoto na kisiasa. Mimi huwa naona Medical Ethics haifuaamtwi na swala la ku-Save life kwao si kipaumbele.

Kwanza inaezekanaje mgonjwa serious kama huyo Dada yetu apewe referral kutoka MNH Upanga apelekwe Mloganzila hii ndo science ambayo sijawah ielewa mpaka kesho.

Inaumiza sana, Pole ndugu yangu.
Ukiweza chukua hatua zaidi hii ni dharau na dhurma.
 
Poleni. Wapeleke mahakamani.
 
Kwa vielelezo hivi nenda mahakamani ili iwe funzo mana watumishi wengi wa afya ni wazembe kupitiliza ndugu zetu wengi hufariki kwa uzembe huo,usiliache lipite hivi hivi.
 
Dah poleni sana na nikupongeze kwa uandishi smart.Wala usione umelalamika hapana kifo ni mpango wa Mungu kama una imani ila kwa kifo cha dada yako kitumike pia kukomesha uzembe wa wahudumu wa afya natamani Waziri Ummy some uzi huu poleni kwa msiba ndugu RIP dada yetu.
 
Janab yeye katingwa na ulaji wa vyakula tu , ukurugenzi kausahau!

Wenyemgonjwa
Kwawote kwann tumekuwa na hulka yakupeleka wagonjwa muhimbili waliochoka

Kipindi Yuko ocean road ndo kipindi alitaliwa muhimbili ...poleni sana
 
Pole sana ndugu yangu; mwenyezi Mungu akupe faraja.
 
Pole sana. Mwaka 2021 nilipotenza mpendwa wangu pale MOI-ICU kwa uzembe wa madaktari na kutaka rushwa kwa baadhi ya vifaa , walikula hla nyingi lakini hawakufanya hivyo, eeh Mungu nimejifunza, ukiona vichaa barabarani usilaumu, ni mlaipo watu wanalipwa na mungu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…