KERO Dada yangu amefariki kwa kuishiwa Oxygen baada ya Muhimbili kufosi kumpeleka Mloganzila

KERO Dada yangu amefariki kwa kuishiwa Oxygen baada ya Muhimbili kufosi kumpeleka Mloganzila

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Nilikuwa na mgonjwa wangu ambaye alikuwa anasumbuliwa na Saratarani, alikuwa anapatiwa huduma Ocean Road, tukiwa hapo tukapata referral ya kwenda Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (Upanga), Dar es Salaam.

Wakati tunaelekea Muhimbili tukapita Hindu Mandal kwa kuwa kuna Daktari ambaye pia tulihitaji kumuona, wakati tukiwa hapo tukapata huduma nzuri tu ya muda.

Tukapatiwa Ambulance iliyotupeleka hadi Muhimbili, wakampokea vizuri mgonjwa na kumpa huduma mbalimbali.

Muda mfupi baadaye wakatuambia kuwa tunatakiwa kulipia chumba kwa gharama ya Shilingi 50,000, pale Mwaisela, huku akiwa anaendelea kupatiwa matibabu ikiwemo kupewa Oxygen kwa kuwa mgonjwa alionakana ana shida ya kupumua.

Baada ya kulipa, wakatuambia hakuna vitanda hivyo wanataka kutupeleka Hospitali ya Mloganzila.

View attachment 3065740

Sisi tukakataa, muda huo ni saa kumi alfajiri, tukawambia tunaomba kama kweli hakuna kitanda basi mgonjwa abaki pale ‘Emergency’ hadi asubuhi kwa kuwa tayari tulishalipia chumba na kuanza kuangaika n ambulance kuelekea Mloganzila wakati tumeshafanya vipimo na taratibu nyingine itakuwa ni usumbufu na pia sio njema kwa mgonjwa.

Ukatokea ubishani pale, sisi tukakataa, lakini Madaktari wa Muhimbili waliokuwepo wakafanya maamuzi ya kibabe wakasema mgonjwa wetu Lilian anaingizwa kwenye Ambulance kupelekwa Mkoganzila.

Wakati wakifnya maamuzi hayo, kuna Nesi mmoja akasema “fanyeni haraka Oxygen inaisha”.

Walipofika Kimara, ndugu yetu aliyekuwa kwenye Ambulance akanijulisha kuwa Oxygen imekata, hadi wanafika Mbezi tayari Oxygen ilikuwa imeshakata na mgonjwa wangu akafariki.

Inawezekana ni siku yake ilikuwa imewadia lakini kilichotokea ni uzembe wa baadhi ya Madaktari wa Hospitali ya Muhimbili na watendaji wengine kadhaa waliokuwepo.

Kwanza najiuliza kwanini walitulipisha kitanda wakijua hakuna kitanda, pili kwanini walimwekea mgonjwa Oxygen kidogo na kwa kauli iliyotolewa pale ni wazi walijua hiyo haitamfikisha Mgonjwa Mloganzila.

Tatu kulikuwa na haja gani ya kumpeleka Mloganzila wakati tayari kulikuwa kunaelekea kukucha na mmoja wa Madaktari aliwaambia wenzake tubaki pale lakini wenzake hawakumsikiliza.
View attachment 3065743
Ambulance iliyombeba dada yangu.
Baada ya msiba nilipouliza mmoja wa Madaktari wa Muhimbili kwanini walitupa Oxygen kidogo anadai lile lilikuwa jukumu la watu wa Ambulance kukagua na sio jukumu lao.

Walichokifanya Madaktari hao wa Muhimbli waliokuwa zamu Usiku wa tukio hakikuwa cha kibinadamu na kama wanafanya hivi basi maisha ya watu wengi yapo hatarini.

Kwa nini nimewasilisha malalamiko yangu hapa JamiiForums, nataka Dunia ijue kuwa kuna baadhi ya Watumishi wa Muhimbili wanatakiwa kujirekebisha, najua roho ya dada yanu haiwezi kurudi ila basi angalau wasingetuonesha wazi kuwa wanataka ndugu yetu afe, pia iwe somo kwa wengine wawe makini.
View attachment 3065744
Miamala ya malipo tuliyofanya kabla ya Mgonjwa kulazimishwa kupelekwa Mloganzila
Mkuu Pole sana kwa Msiba.Tafdhali Ondoa Hizi Taarifa binafsi za marehemu Dada huku Mtandaoni.Pamoja na kwamba amefariki bado anastahili Faragha.

Pili Kwa mujibu wa mealezo yako hapo kunaweza kuwa na Kesi ila sifahamu kwa mujibu wa sheria za Tanzania Uwajibikaji wa Madaktari(Professional Malpractice) Ikoje.Mfano eneo la Fidia,etc.


All in all Fuatilia Kwa Ukaribu zaidi na Mungu awape Nguvu katika kipindi hichi kigumu.Apumzike kwa amani DADA Lilian
 
Hospital huwa wanaahirisha kifo sidhani.Hospitali NI wakweli Sana ndio maana huwa kuna mortuary wamejenga hospitalini kuwa mwenye macho haambiwi tazama kuwa MTU akikanyaga hospitali ajue kuna mawili kupona au kuishia kwenye jengo la mortuary analiliona hawafanyi Siri jengo liko wazi kama yalivyo majengo ya madaktari ,maabara,wodi nk
Basi huelewi lengo la tiba ni nini.

In fact hosptiali za nchi nyingi, kwa mfano marakeni hazina mortuary
 
Saratarani

Poleni sana kwa mgonjwa,

Saratani ya kinywa cha mdomo ina changamoto kubwa ikiwa imesambaa ktk mfumo wa pua na mdomo, kichwa, koo kwa ajili ya kuvuta pumzi ya uhai Oxygen. Kinga ndogo chini ya CD4 24, tiba ya miozi chemotherapy katika stage ya ugonjwa ilipofika ripoti inaonesha haitakuwa na manufaa yoyote.

Ilitakiwa madaktari wawapeni ndugu taarifa ya ukweli ya hali ya mgonjwa na ushauri nasaha / counselling kuwa mgonjwa amefikia hali ya mwisho wa uhai hivyo kupatiwa madawa ya kupunguza maumivu na mateso kwa kuwa hauna uwezekano wa kuponyeshwa ugonjwa ukiliomkuba Palliative care /for end of Life.

Hard palate cancer is a rare cancer that forms on the roof of your mouth.
 
Mortuary Marekani hata hapo Kenya nyingi NI private business zinaitwa funeral homes unafia hospital unapelekwahuko ukalipie private huko funeral homes
Siyo sehemu ya hospitali; zinapokea maiti kutoka popote pale kwa ajili ya matunzo ya mwisho kabla ya mazishi. Haina maana kuwa kwenda hospitali ni kwenda kufa na hivyo mortuarym iwepo pale pale kama sehemu ya hospitali.
 
Duh Pole sana Ndugu yangu, Mimi juzi nusura tumpoteze Ndugu yangu pale MOI, alipata Ajali Tanga, akapelekwa hospital ikaonekana ni issue KUBWA, tukaomba referral kuja MOI. Wakaondoka Tanga kuja MOI wakafika saa nne usiku, tukapokelewa, mgonjwa hakua na jeraha kwa nje ila alilalamika maumivu Sana, saa SITA na nusu usiku akafanyiwa vipimo.

Vichekesho vikaanza, mgonjwa wa referral akapewa majibu kuwa hajaumia yuko poa hayo ni maumivu Tu, tukaandikiwa dawa tukaruhusiwa tukiwa tumembeba mgonjwa wetu. Analia maumivu makali sana.

Asubuhi mgonjwa hali ikawa mbaya zaidi ikabidi tumpeleke hospital Fulani pale TEGETA akafanyiwa MRI ikaonekana ana internal bleeding na tayari mwili ulikua ushaanza ku-react, yaani damu inaisha na anahisi tumbo kuvimba na kushindwa kupumua.

Ikabidi tukubaliane afanyiwe emergency operation kuanzia saa Saba mchana Hadi saa mbili usiku, wakamtoa bandama, ndio ilikua imeumia na kupelekea damu nyingi sana kuvujia Ndani, walitoa damu 2ltrs.

Hayo ndio yaliyotukuta MOI yaani tungerelax tukamuamini yule Dr Leo Hii ningekua msibani.

Poleni Sana Ndugu zangu
Inaanzia kwenye mifumo ya nchi tu jinsi inavyoendeshwa ndivyo taasisi zote zinavyoreflect. Kiufupi hivi sasa ukipata shida yeyote inayokulazimu kwenda taasisi yoyote ya umma tegemea huduma ya hovyo tu.
 
Jf malalamiko mengi kama haya tunaletanayaficha hamtoi,mimi ndugu yangu mwezi wa 3 huu amelipia vifaa vya matibabu ya Gastro lakini tunaambiwa vimekwisha ma mzabuni hajaleta vingineara mzabuni kaleta vifaa vilivyochini ya kiwango madokta wamevigomea,nililets maandiko humu hamkujali wala kuyatoa mkayakalia,haya hili kwanini hsmkulikalia??
 
Tatizo mawasiliano unakuta daktari yeye hahusiki na vitanda Wala sehemu ya kugawa dawa wala sehemu Hizo za huduma nyingine ziwe maabara nk

Yeye akiona mgonjwa amemwandikia kuwa akalazwe n wapi atalazwa sio KAZI Yake hao walazaji ndio watajua kama watamlaza kwenye bodaboda au mtaroni au kwenye daladala haimhusu na pia kabla kulazwa inatakiwa kulipia Kwanza daktari akiandika ulazwe .Mpokea malipo sio daktari na hahusiki na kulaza MTU yeye hupokea malipo Tu akishapokea ndipo huota go ahead uende huko Kwa walazaji wajue wakulaze wapi

Sasa na wao wakipokea ndipo huanza kuhaha watamlaza wapi Hilo halihusu madaktari wala Mpokea pesa NI wao watafute pa kulaza

Hospital a serikali kuna urasimi na NI.pasua kichwa hawaruhusu MTU mmoja kufanya majukumu yote.au kuwa na information zote na kufanya maamuzi
Hapo

Pia hiyo mitungi ya gesi sio KAZI ya manesi kujaza wao huhusika Tu kuwekea Tu mgonjwa .Wanaojaza oxygen wengine

Ukiumwa NI.kukazana kuomba Mungu Sana tu pia badala Tu ya kuwa na Imani kubwa Sana Kwa hospital Tu

Msione watu wanajazana Kwa Mwamposya kuna maneno msije ona wajinga au wamechanganyikiwa
Wanaochukua pesa wanawajibika kujua kama vyumba vipo au hakuna, manesi hata kama hawajazi lakini wanatakiwa kujua kama tank lina Oxygen kiasi gani na mgonjwa anapata ya kutosha, ni uzembe tuu hakuna excuse yeyote
 
Nilikuwa na mgonjwa wangu ambaye alikuwa anasumbuliwa na Saratarani, alikuwa anapatiwa huduma Ocean Road, tukiwa hapo tukapata referral ya kwenda Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (Upanga), Dar es Salaam.

Wakati tunaelekea Muhimbili tukapita Hindu Mandal kwa kuwa kuna Daktari ambaye pia tulihitaji kumuona, wakati tukiwa hapo tukapata huduma nzuri tu ya muda.

Tukapatiwa Ambulance iliyotupeleka hadi Muhimbili, wakampokea vizuri mgonjwa na kumpa huduma mbalimbali.

Muda mfupi baadaye wakatuambia kuwa tunatakiwa kulipia chumba kwa gharama ya Shilingi 50,000, pale Mwaisela, huku akiwa anaendelea kupatiwa matibabu ikiwemo kupewa Oxygen kwa kuwa mgonjwa alionakana ana shida ya kupumua.

Baada ya kulipa, wakatuambia hakuna vitanda hivyo wanataka kutupeleka Hospitali ya Mloganzila.

View attachment 3065740

Sisi tukakataa, muda huo ni saa kumi alfajiri, tukawambia tunaomba kama kweli hakuna kitanda basi mgonjwa abaki pale ‘Emergency’ hadi asubuhi kwa kuwa tayari tulishalipia chumba na kuanza kuangaika n ambulance kuelekea Mloganzila wakati tumeshafanya vipimo na taratibu nyingine itakuwa ni usumbufu na pia sio njema kwa mgonjwa.

Ukatokea ubishani pale, sisi tukakataa, lakini Madaktari wa Muhimbili waliokuwepo wakafanya maamuzi ya kibabe wakasema mgonjwa wetu Lilian anaingizwa kwenye Ambulance kupelekwa Mkoganzila.

Wakati wakifnya maamuzi hayo, kuna Nesi mmoja akasema “fanyeni haraka Oxygen inaisha”.

Walipofika Kimara, ndugu yetu aliyekuwa kwenye Ambulance akanijulisha kuwa Oxygen imekata, hadi wanafika Mbezi tayari Oxygen ilikuwa imeshakata na mgonjwa wangu akafariki.

Inawezekana ni siku yake ilikuwa imewadia lakini kilichotokea ni uzembe wa baadhi ya Madaktari wa Hospitali ya Muhimbili na watendaji wengine kadhaa waliokuwepo.

Kwanza najiuliza kwanini walitulipisha kitanda wakijua hakuna kitanda, pili kwanini walimwekea mgonjwa Oxygen kidogo na kwa kauli iliyotolewa pale ni wazi walijua hiyo haitamfikisha Mgonjwa Mloganzila.

Tatu kulikuwa na haja gani ya kumpeleka Mloganzila wakati tayari kulikuwa kunaelekea kukucha na mmoja wa Madaktari aliwaambia wenzake tubaki pale lakini wenzake hawakumsikiliza.
View attachment 3065743
Ambulance iliyombeba dada yangu.
Baada ya msiba nilipouliza mmoja wa Madaktari wa Muhimbili kwanini walitupa Oxygen kidogo anadai lile lilikuwa jukumu la watu wa Ambulance kukagua na sio jukumu lao.

Walichokifanya Madaktari hao wa Muhimbli waliokuwa zamu Usiku wa tukio hakikuwa cha kibinadamu na kama wanafanya hivi basi maisha ya watu wengi yapo hatarini.

Kwa nini nimewasilisha malalamiko yangu hapa JamiiForums, nataka Dunia ijue kuwa kuna baadhi ya Watumishi wa Muhimbili wanatakiwa kujirekebisha, najua roho ya dada yanu haiwezi kurudi ila basi angalau wasingetuonesha wazi kuwa wanataka ndugu yetu afe, pia iwe somo kwa wengine wawe makini.
View attachment 3065744
Miamala ya malipo tuliyofanya kabla ya Mgonjwa kulazimishwa kupelekwa Mloganzila
Ungekwenda Mwananyamala Hospital Emegeny,ile hospital,wagonjwa wanashughulikiwa sana ,ikitokea kafariki,unajuwa wazi,-huyu wakati wake umefika.Uongozi na wafanyakazi wa Mwananyamala hospital,wanajitahidi sana.
 
Nafikiri kilichokosekana hapo ni 'Proper Counseling ' tu. Mgonjwa anaonekana alikuwa kwenye terminal illness, hata ORCI wameamua kumpeleka kwingine hawataki 'Death' nyingi zitokee kwao.

Lakini, ndugu yako alijuaje Oksijeni imekata? What if mgonjwa alianza kupoteza maisha kabla ya hiyo Oksijeni kukata?

Yote kwa yote, Pole sana komredi kumpoteza dada.
 
Back
Top Bottom