waifu wangu anaye rafiki yake mmoja mwanamke mwenzie, alimaliza Arusha institute of accountancy sijui, yule dada katafuta kazi hadi amechoka, umri wake ni miaka kama 35 kwasasa. amekuja kupata juzi hapa. cha ajabu ni kwamba, wanawake maklassmate wenzie wote walikuwa wamepata kazi, mmoja alipata kazi kipindi cha yule jamaa wa BOT mwenye kesi ya ubadhilifu wa majengo ya twin towers, wenzie walihongwa love4 kila mtu, lakini hauwezi amini sasahivi anaiuza ile lave4 ili apate walau hela ya kununulia matunda, mayai na vyakula bora kwasababu tayari anaishi kwa matumaini, this is not a story, ni ukweli,.....i don't mean kwamba yule jamaa ndo ana ukimwi, ila labda alipata kwengine tu hilo hatujui...msichana mwenye umri wa miaka hata arobaini hajafika, hata maisha hajayala, anaenda kufariki kwasababu ya kazi na love4...think about that......hii ndo inayomnyemelea huyo mdada. pili, shetani lazima atakuja kumlengesha tu kwa mumewe, na kama ni muhehe, either atajinyonga huyo mwanaume amtengenezee historia mbaya ya ndoa, au atamcharanga mapanga kwa kigari hicho tu. ni dhambi kubwa sana kutoka nje ya ndoa, mimi ni mwanaume, lakini nachukia sana mtu anayetoka nje ya ndoa....ridhikeni na wake zeu au waume zenu wajameni...dunia hii ya hivyohivyo, hata upewe nini hautaridhika, bado utataka vinyi, na zaidi ya yote, utajiri na heshima vyatoka kwa Mungu, hauwezijua kama angeamua kukataa kutochukua iyo gari hata kama angefukuzwa kazi, pengine Mungu alikuwa ameandaa mazingira ya yeye kuendesha mashangingi na kuwa na majumba masaki ambayo Mungu angempa....mwogopeni Mungu, mwogopeni Mungu, mwogopeni Mungu. mwenye sikio la kusikilia na asikie!