Dah! Nimeamini Kwenye Mpira uchawi upo, Sio kwa Alichokifanya Ivory Coast leo!

Dah! Nimeamini Kwenye Mpira uchawi upo, Sio kwa Alichokifanya Ivory Coast leo!

Mali wanautoto ndio timu iliotoka kitoto ukiitoa hii ya kizimkazi
Hahaaaa kizimkazi Stars alipotoa sare na Zambia kama mimi ningekuwa Rais wa nchi hii, ningewaweka ndani hata wiki mara baada ya AFCON kuisha. Hata hao Mali, wanaenda kuwekwa ndani hususani yule kocha wao atachapwa na viboko kabisa.
 
Yaani kabisa ukaweka hela Mali imfunge Ivory Coast au ulikuwa hufuatilii hii michuano mkuu?
Vitu vingne viishie kwenye kubishana na watu ila sio kuweka hela yako kwa Mali dhidi ya Ivory Coast labda kama ni buku uliamua kumchangia mhindi
 
Kosa kubwa ambalo Mali walilifanya ni kuanza kulinda goli badala ya kuendelea kushambulia, lawama zote anabeba kocha, unatoa mshambuliaji ambaye alikuwa anasumbua hadi kusababisha kadi nyekundu ili ukalinde goli moja!

Alikuwa na hofu gani ilihali mpinzani wake alikuwa pungufu uwanjani, hivi sijui kwa nini hawa Makocha huwa wanaamini sana mbinu ya kujilinda baada ya kushinda, "Lawama abebe Kocha".
Hata Taifa stars walifanya hivyo walioo cheza na Zambia(chipolopolo,)
 
Hahaaaa kizimkazi Stars alipotoa sare na Zambia kama mimi ningekuwa Rais wa nchi hii, ningewaweka ndani hata wiki mara baada ya AFCON kuisha. Hata hao Mali, wanaenda kuwekwa ndani hususani yule kocha wao atachapwa na viboko kabisa.
Haaa😄😄...
 
Haya mawazo ya kijinga jinga ya kuamini kuwa uchawi unaweza ukafanya mpira ukaingia golini au usiingie yamebaki zaidi kwa watu wenye elimu ya shule za msingi hizi za kiswahili zilizojaa Tanzania. Bure kabisa.
 
Kwa Mimi mkongwe wa muda mrefu Kwenye kuangalia mechi za afrika na nje ya afrika hakuna uchawi pale , Mali walijimaliza wenyewe , na mtindo wao wa show game wakitaka zaidi kuonyesha mbwmbwe na madoido ya kusakata boli na kusahau jukumu no 1 la kufunga.
Nigeria ya kina okocha ikitisha dunia wc 1994 na 1998 kwa show game iliambulia kutolewa kwa uchungu .
Nigeria ya sasa imebadilika inacheza kwa kasi na kutamani kufunga kila wapato nafasi Kama Ivory Coast .
Ivory Coast ya kina drogba ilipenda show game matokeo yake ikazimwa na Zambia .
 
Akili za Vijana wa kubeti Mbovu sana.

Ivory Cost kuna Academy za kutosha za mpira.

Wale jamaa wamewekeza kwenye soka si mchezo.

Kama mpira ungekuwa Uchawi Nigwria angekuwa na Makombe 1000 ya Dunia.
 
Yani mtu anabeti anajipangia matokeo timu flani ishinde afu ikifungwa unaeza kusema oooh kanji mchawi sijui Kuna uchawi , Aya bhn we si uliingia na matokeo Yako mfukoni , kwani swala la matokeo ya mchezo si liko wazi yoyote anaweza akashinda. Sasa km unategemea timu inashinda 100% basi kulikuwa na haja Gani ya mech kuchezwa kupoteza mda?🤔 Akili kum kichwa
 
Back
Top Bottom