Daima usimdharau usiyemjua, mwenzenu leo nimekutwa na jambo

Daima usimdharau usiyemjua, mwenzenu leo nimekutwa na jambo

aliyetegwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
313
Reaction score
486
Niko zangu kibandani kwangu, hua nauza nguo kwa jumla na rejareja. Mara ghafula wanatokea watu wawili wachafu, mzee kwa umri zaidi ya miaka sitini akiwa amevalia suruali yenye viraka kila sehemu ila sehemu inayoonekana zaidi ni maeneo ya kwenye zipu ambapo pameshonwa na uzi mweupe wakati suruali ni nyeusi.

Chini kavaa viatu visivyoeleweka na kichwani kabeba sanduku lililochakaa aina ya Omega kubwa haswaa likiwa limejaa vumbi jekundu kama lile la Kigoma(wanaojua vumbi la Kigoma watapata picha).

Mtu wa pili alikua ni mwanamke aliye kwenye umri wa miaka thelathini ya mwanzo akiwa amechoka na maisha haswa kwa muonekano. Amevaa sketi ya pande sita isiyoeleweka, coat la tracksuit ambalo limenyonyoka manyoya haswaa na yuko na nywele chafu hatari.

Kitu kilichoniijia akilini mwangu moja kwa moja wale watu ni omba omba ila wanaanza nichanganya kwa kuulizia bei ya nguo na mimi sikutaka kujichosha nao maana najua ni omba omba ila ndo wameamua kunichosha nikawa nawapa bei ya jumla, nguo ya kwanza shilingi ngapi, nikajibu 37,000,/ akaulizia ya pili, tatu na nne, jibu langu likawa lilelile.

Baadaye yule mwanaume akaomba waonyeshwe sehemu ya kajaribishia, kwa jinsi walivyo nikaona wanaendelea kunizingua nikamwambia tuelewane bei kwanza ndio nguo zijaribishiwe. Akaniuliza kwani izo nguo nne ni kiasi gani jumla, nikamjibu ni 148,000, akaniambia we nionyeshe tuu pakujaribishia bei hatutoshidwana nikaona isiwe tabu wacha nimuonyeshe.

Yule bidada aliyechoka akaingia na kajaribishia nguo, kwa macho yangu hakuna nguo hata moja iliyomkaa vizuri ila tayari sikua nawatilia manani so sikua nikuangaika nao.

Picha linaanza mwanaume, yule mbaba anaomba nimpe usalama ili aweze kutoa pesa nikaona kama ananichanganya nikamwambia mimi sina usalama, mara papu anamwambia yule mwanamke njoo unisaidie kushusha sanduku.

Maana tangu wamefika mwanaume alikua na sanduku kichwani na hakua amelishusha, bidada akaenda, sanduku lilikua zito haswaa kiasi kwamba mwanaume hawezi kuliweka chini mwenyewe.

Mwanaume akaingiza sanduku lake ndani, mwanamke akakaa mbele yake na kumsisitiza atoe pesa za kutosha matumizi yote maana hapa dukani ndio sehemu yenye usalama na hawatopata sehemu nyingine salama.

Mwanaume anafungua kufuli lililokua limefunga zipu za sanduku, sijaamini macho yangu, lile sanduku lilikua limejaa pesa zilizofugwa kwenye mabunda ya milioni milioni. Akatoa kibunda kimoja kisha akafunga sanduku baada ya hapo akahesa noti kumi na tano za elfu kumi kumi yaani laki moja na hamsini, nikakata pesa yangu na kumrudishia shilingi elfu mbili.

Mwanamke akaja akamtwisha mwanaume sanduku wakaondoka zao wakiwa wameniacha mdomo wazi na maswali kibao. Naendelea kujiuliza wametoka wapi na wànakwenda wapi, izo pesa zimetikana na nini, wanazipeleka banki ama wapi sijui?!

Kiukweli sijapata majibu kabisa ila naendelea kuduwaa, staili yao ya uvaaji ni mbinu ya ulinzi kwao ama walikua makapuku ila pesa wameziokota? Sanduku lilikua limejaa vumbi haswa na limechakaa haswa kama vile lilikua kwenye buti ya bus ambalo linapiga masafa marefu kwenye barabara ya vumbi.

Sasa ni kwamba sanduku waliliweka kwenye buti wakati wa safari ama walikaa nalo ndani, sijui, nimebaki na maswali kibao na kujidharu kwa kuwadharau wakati mimi ni kapuku na wao ndo mabosi.

Ndugu zangu wana JF, tuheshimu watu wote tunaokutana nao barabarani maana hatujui walichobeba. Mwenzenu leo nimekutwa na jambo, ila nimeona isiwe tabu nililete kwenu pia maana sisi ni wanafamilia mnaweza kua mmekutana na visanga tofauti tofauti ambavyo vinaweza kua mafundisho kwetu sote.
 
Wapemba hao Kuna mzee kipind fulani alikuwa anaenda crdb na kapu kama muuza samaki ndani anaweka pesa, anaenda akiwa kavaa ndala miaka ya 2008 enzi nipo Tanga pale crdb karibu na soko la uzunguni ,sikuamini alikuja na kofia chafu zile wanavaa wauza samaki na nguo chafu nikafiria ametoka deep sea hapo karibu na kapu juu kaweka Yale majani ya mikoko kama wanavyofunikia dagaa akafungua pale ila wanamjua aisee pesa kibao ila mkononi kajaa mapete kibao ...Nikiangalia nywele zake nikajua mpemba jamaa ana pesa ila kingine kutokana na mapete Yale mengi nahisi atakuwa mganga
 
Matajiri wengi wa vijijini ndy swaga zao wakiwa mjini.
 
Niko zangu kibandani kwangu, hua nauza nguo kwa jumla na rejareja. Mara ghafula wanatokea watu wawili wachafu, mzee kwa umri zaidi ya miaka sitini akiwa amevalia suruali yenye viraka kila sehemu ila sehemu inayoonekana zaidi ni maeneo ya kwenye zipu ambapo pameshonwa na uzi mweupe wakati suruali ni nyeusi.

Chini kavaa viatu visivyoeleweka na kichwani kabeba sanduku lililochakaa aina ya Omega kubwa haswaa likiwa limejaa vumbi jekundu kama lile la Kigoma(wanaojua vumbi la Kigoma watapata picha).

Mtu wa pili alikua ni mwanamke aliye kwenye umri wa miaka thelathini ya mwanzo akiwa amechoka na maisha haswa kwa muonekano. Amevaa sketi ya pande sita isiyoeleweka, coat la tracksuit ambalo limenyonyoka manyoya haswaa na yuko na nywele chafu hatari.

Kitu kilichoniijia akilini mwangu moja kwa moja wale watu ni omba omba ila wanaanza nichanganya kwa kuulizia bei ya nguo na mimi sikutaka kujichosha nao maana najua ni omba omba ila ndo wameamua kunichosha nikawa nawapa bei ya jumla, nguo ya kwanza shilingi ngapi, nikajibu 37,000,/ akaulizia ya pili, tatu na nne, jibu langu likawa lilelile.

Baadaye yule mwanaume akaomba waonyeshwe sehemu ya kajaribishia, kwa jinsi walivyo nikaona wanaendelea kunizingua nikamwambia tuelewane bei kwanza ndio nguo zijaribishiwe. Akaniuliza kwani izo nguo nne ni kiasi gani jumla, nikamjibu ni 148,000, akaniambia we nionyeshe tuu pakujaribishia bei hatutoshidwana nikaona isiwe tabu wacha nimuonyeshe.

Yule bidada aliyechoka akaingia na kajaribishia nguo, kwa macho yangu hakuna nguo hata moja iliyomkaa vizuri ila tayari sikua nawatilia manani so sikua nikuangaika nao.

Picha linaanza mwanaume, yule mbaba anaomba nimpe usalama ili aweze kutoa pesa nikaona kama ananichanganya nikamwambia mimi sina usalama, mara papu anamwambia yule mwanamke njoo unisaidie kushusha sanduku.

Maana tangu wamefika mwanaume alikua na sanduku kichwani na hakua amelishusha, bidada akaenda, sanduku lilikua zito haswaa kiasi kwamba mwanaume hawezi kuliweka chini mwenyewe.

Mwanaume akaingiza sanduku lake ndani, mwanamke akakaa mbele yake na kumsisitiza atoe pesa za kutosha matumizi yote maana hapa dukani ndio sehemu yenye usalama na hawatopata sehemu nyingine salama.

Mwanaume anafungua kufuli lililokua limefunga zipu za sanduku, sijaamini macho yangu, lile sanduku lilikua limejaa pesa zilizofugwa kwenye mabunda ya milioni milioni. Akatoa kibunda kimoja kisha akafunga sanduku baada ya hapo akahesa noti kumi na tano za elfu kumi kumi yaani laki moja na hamsini, nikakata pesa yangu na kumrudishia shilingi elfu mbili.

Mwanamke akaja akamtwisha mwanaume sanduku wakaondoka zao wakiwa wameniacha mdomo wazi na maswali kibao. Naendelea kujiuliza wametoka wapi na wànakwenda wapi, izo pesa zimetikana na nini, wanazipeleka banki ama wapi sijui?!

Kiukweli sijapata majibu kabisa ila naendelea kuduwaa, staili yao ya uvaaji ni mbinu ya ulinzi kwao ama walikua makapuku ila pesa wameziokota? Sanduku lilikua limejaa vumbi haswa na limechakaa haswa kama vile lilikua kwenye buti ya bus ambalo linapiga masafa marefu kwenye barabara ya vumbi.

Sasa ni kwamba sanduku waliliweka kwenye buti wakati wa safari ama walikaa nalo ndani, sijui, nimebaki na maswali kibao na kujidharu kwa kuwadharau wakati mimi ni kapuku na wao ndo mabosi.

Ndugu zangu wana JF, tuheshimu watu wote tunaokutana nao barabarani maana hatujui walichobeba. Mwenzenu leo nimekutwa na jambo, ila nimeona isiwe tabu nililete kwenu pia maana sisi ni wanafamilia mnaweza kua mmekutana na visanga tofauti tofauti ambavyo vinaweza kua mafundisho kwetu sote.
TENA UKOME.MAJINI HAYO.
 
Watu kama wewe hamkufaa kuuza vitu vya kukutana na watu wengi wa aina tofaut tofauti kama hiyo.

Kwanini umchukulie mtu poa kisa mavazi? Una safari ndefu sana ya kuwajua wateja wenye pesa.
 
Back
Top Bottom