aliyetegwa
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 313
- 486
Niko zangu kibandani kwangu, hua nauza nguo kwa jumla na rejareja. Mara ghafula wanatokea watu wawili wachafu, mzee kwa umri zaidi ya miaka sitini akiwa amevalia suruali yenye viraka kila sehemu ila sehemu inayoonekana zaidi ni maeneo ya kwenye zipu ambapo pameshonwa na uzi mweupe wakati suruali ni nyeusi.
Chini kavaa viatu visivyoeleweka na kichwani kabeba sanduku lililochakaa aina ya Omega kubwa haswaa likiwa limejaa vumbi jekundu kama lile la Kigoma(wanaojua vumbi la Kigoma watapata picha).
Mtu wa pili alikua ni mwanamke aliye kwenye umri wa miaka thelathini ya mwanzo akiwa amechoka na maisha haswa kwa muonekano. Amevaa sketi ya pande sita isiyoeleweka, coat la tracksuit ambalo limenyonyoka manyoya haswaa na yuko na nywele chafu hatari.
Kitu kilichoniijia akilini mwangu moja kwa moja wale watu ni omba omba ila wanaanza nichanganya kwa kuulizia bei ya nguo na mimi sikutaka kujichosha nao maana najua ni omba omba ila ndo wameamua kunichosha nikawa nawapa bei ya jumla, nguo ya kwanza shilingi ngapi, nikajibu 37,000,/ akaulizia ya pili, tatu na nne, jibu langu likawa lilelile.
Baadaye yule mwanaume akaomba waonyeshwe sehemu ya kajaribishia, kwa jinsi walivyo nikaona wanaendelea kunizingua nikamwambia tuelewane bei kwanza ndio nguo zijaribishiwe. Akaniuliza kwani izo nguo nne ni kiasi gani jumla, nikamjibu ni 148,000, akaniambia we nionyeshe tuu pakujaribishia bei hatutoshidwana nikaona isiwe tabu wacha nimuonyeshe.
Yule bidada aliyechoka akaingia na kajaribishia nguo, kwa macho yangu hakuna nguo hata moja iliyomkaa vizuri ila tayari sikua nawatilia manani so sikua nikuangaika nao.
Picha linaanza mwanaume, yule mbaba anaomba nimpe usalama ili aweze kutoa pesa nikaona kama ananichanganya nikamwambia mimi sina usalama, mara papu anamwambia yule mwanamke njoo unisaidie kushusha sanduku.
Maana tangu wamefika mwanaume alikua na sanduku kichwani na hakua amelishusha, bidada akaenda, sanduku lilikua zito haswaa kiasi kwamba mwanaume hawezi kuliweka chini mwenyewe.
Mwanaume akaingiza sanduku lake ndani, mwanamke akakaa mbele yake na kumsisitiza atoe pesa za kutosha matumizi yote maana hapa dukani ndio sehemu yenye usalama na hawatopata sehemu nyingine salama.
Mwanaume anafungua kufuli lililokua limefunga zipu za sanduku, sijaamini macho yangu, lile sanduku lilikua limejaa pesa zilizofugwa kwenye mabunda ya milioni milioni. Akatoa kibunda kimoja kisha akafunga sanduku baada ya hapo akahesa noti kumi na tano za elfu kumi kumi yaani laki moja na hamsini, nikakata pesa yangu na kumrudishia shilingi elfu mbili.
Mwanamke akaja akamtwisha mwanaume sanduku wakaondoka zao wakiwa wameniacha mdomo wazi na maswali kibao. Naendelea kujiuliza wametoka wapi na wànakwenda wapi, izo pesa zimetikana na nini, wanazipeleka banki ama wapi sijui?!
Kiukweli sijapata majibu kabisa ila naendelea kuduwaa, staili yao ya uvaaji ni mbinu ya ulinzi kwao ama walikua makapuku ila pesa wameziokota? Sanduku lilikua limejaa vumbi haswa na limechakaa haswa kama vile lilikua kwenye buti ya bus ambalo linapiga masafa marefu kwenye barabara ya vumbi.
Sasa ni kwamba sanduku waliliweka kwenye buti wakati wa safari ama walikaa nalo ndani, sijui, nimebaki na maswali kibao na kujidharu kwa kuwadharau wakati mimi ni kapuku na wao ndo mabosi.
Ndugu zangu wana JF, tuheshimu watu wote tunaokutana nao barabarani maana hatujui walichobeba. Mwenzenu leo nimekutwa na jambo, ila nimeona isiwe tabu nililete kwenu pia maana sisi ni wanafamilia mnaweza kua mmekutana na visanga tofauti tofauti ambavyo vinaweza kua mafundisho kwetu sote.
Chini kavaa viatu visivyoeleweka na kichwani kabeba sanduku lililochakaa aina ya Omega kubwa haswaa likiwa limejaa vumbi jekundu kama lile la Kigoma(wanaojua vumbi la Kigoma watapata picha).
Mtu wa pili alikua ni mwanamke aliye kwenye umri wa miaka thelathini ya mwanzo akiwa amechoka na maisha haswa kwa muonekano. Amevaa sketi ya pande sita isiyoeleweka, coat la tracksuit ambalo limenyonyoka manyoya haswaa na yuko na nywele chafu hatari.
Kitu kilichoniijia akilini mwangu moja kwa moja wale watu ni omba omba ila wanaanza nichanganya kwa kuulizia bei ya nguo na mimi sikutaka kujichosha nao maana najua ni omba omba ila ndo wameamua kunichosha nikawa nawapa bei ya jumla, nguo ya kwanza shilingi ngapi, nikajibu 37,000,/ akaulizia ya pili, tatu na nne, jibu langu likawa lilelile.
Baadaye yule mwanaume akaomba waonyeshwe sehemu ya kajaribishia, kwa jinsi walivyo nikaona wanaendelea kunizingua nikamwambia tuelewane bei kwanza ndio nguo zijaribishiwe. Akaniuliza kwani izo nguo nne ni kiasi gani jumla, nikamjibu ni 148,000, akaniambia we nionyeshe tuu pakujaribishia bei hatutoshidwana nikaona isiwe tabu wacha nimuonyeshe.
Yule bidada aliyechoka akaingia na kajaribishia nguo, kwa macho yangu hakuna nguo hata moja iliyomkaa vizuri ila tayari sikua nawatilia manani so sikua nikuangaika nao.
Picha linaanza mwanaume, yule mbaba anaomba nimpe usalama ili aweze kutoa pesa nikaona kama ananichanganya nikamwambia mimi sina usalama, mara papu anamwambia yule mwanamke njoo unisaidie kushusha sanduku.
Maana tangu wamefika mwanaume alikua na sanduku kichwani na hakua amelishusha, bidada akaenda, sanduku lilikua zito haswaa kiasi kwamba mwanaume hawezi kuliweka chini mwenyewe.
Mwanaume akaingiza sanduku lake ndani, mwanamke akakaa mbele yake na kumsisitiza atoe pesa za kutosha matumizi yote maana hapa dukani ndio sehemu yenye usalama na hawatopata sehemu nyingine salama.
Mwanaume anafungua kufuli lililokua limefunga zipu za sanduku, sijaamini macho yangu, lile sanduku lilikua limejaa pesa zilizofugwa kwenye mabunda ya milioni milioni. Akatoa kibunda kimoja kisha akafunga sanduku baada ya hapo akahesa noti kumi na tano za elfu kumi kumi yaani laki moja na hamsini, nikakata pesa yangu na kumrudishia shilingi elfu mbili.
Mwanamke akaja akamtwisha mwanaume sanduku wakaondoka zao wakiwa wameniacha mdomo wazi na maswali kibao. Naendelea kujiuliza wametoka wapi na wànakwenda wapi, izo pesa zimetikana na nini, wanazipeleka banki ama wapi sijui?!
Kiukweli sijapata majibu kabisa ila naendelea kuduwaa, staili yao ya uvaaji ni mbinu ya ulinzi kwao ama walikua makapuku ila pesa wameziokota? Sanduku lilikua limejaa vumbi haswa na limechakaa haswa kama vile lilikua kwenye buti ya bus ambalo linapiga masafa marefu kwenye barabara ya vumbi.
Sasa ni kwamba sanduku waliliweka kwenye buti wakati wa safari ama walikaa nalo ndani, sijui, nimebaki na maswali kibao na kujidharu kwa kuwadharau wakati mimi ni kapuku na wao ndo mabosi.
Ndugu zangu wana JF, tuheshimu watu wote tunaokutana nao barabarani maana hatujui walichobeba. Mwenzenu leo nimekutwa na jambo, ila nimeona isiwe tabu nililete kwenu pia maana sisi ni wanafamilia mnaweza kua mmekutana na visanga tofauti tofauti ambavyo vinaweza kua mafundisho kwetu sote.