Daima usimdharau usiyemjua, mwenzenu leo nimekutwa na jambo

Kuna siku alikuja mzee wa kinyamwezi dukani afla simu yake ikaita simu ya tochi na mlio wa marimba. Jamaa wakacheka sana mzee kumaliza kuongea alikasirika sana alihisi kudharauliwa. Nikampooza pale na kumpa mkono wa salamu, mzee alitumia hela hapo mpaka jamaa wote walibaki kushangaa. Na alikuwa na hela ndefu tu, aliishia na kusema:- sipendi mtu anidharau kama sio huyu kaka ningali ondoka zamani sana. Usidharau kimuonekano wala kimatendo mpe heshima kila mtu
 
Hahahahaaaa mpaka nimechekaka ndugu mana hata mimi niliwahi kumuona sana yule mzenji hapo hapo so umenikumbusha mbali sanaa na mishati yake michafu chafu yule tajiri wa maboti ya uvuvi nadhani
 
Hahahahaaaa mpaka nimechekaka ndugu mana hata mimi niliwahi kumuona sana yule mzenji hapo hapo so umenikumbusha mbali sanaa na mishati yake michafu chafu yule tajiri wa maboti ya uvuvi nadhani
Kuna stori nilizisikia!! eti Kuna siku majambazi walimuotea🤣🤣🤣wakampora
 
Fanya zoezi moja dogo tu. Chukua sarafu ya shilingi mia Tano (500/) itupe kwenye tope kisha itoe halafu isafishe.

Thamani yake imebadilika? Thamani ya binadamu haiondolewi na dhambi au muonekano wake.
 
Kuna siku nipo ktk hiace karume kuelekea home. Nimekaa ktk bansen burner. Ile kwanza nyuma ya dereva. Upepo mkali nikafunga kioo. Kuna jamaa alikuwa amekaa mbele yangu aliniuliza swali kuwa nina elimu gani?
Yaani umri wangu ulikuwa mdogo wa sekondari then aliniuliza lile swali.

Nikatafakari sana..kwamba umri huu nilitakiwa kuwa na elimu gani ili niweze kujibu kulingana na matakwa ya huyu ndezi. Kiukweli niliumizwa sana na zile dharau tena jamaa alikuwa mkubwa Sana ki umri. Niliamua kukaa kimya. Ila nilikuwa na hasira sana. Sijasahau ile dharau.
 
Pole mkuu
 
Hahahaha wamekuachia chuma ulete. Jipange.
 
Hii itakuwa ni hadithi Kama zilivyo hadithi nyingine naona,pesa Ina adabu zake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…