Daktari anasoma miaka 5-7 na mhandisi anasoma miaka kati ya 3-4 lakini ona tofauti ya mishahara kati yao hapa chini

Daktari anasoma miaka 5-7 na mhandisi anasoma miaka kati ya 3-4 lakini ona tofauti ya mishahara kati yao hapa chini

Umeshawahi kufikiria kuwa huyo engineer akiumwa au akiumia nani anamtibu mkuu?

Daktari anahakikisha kwanza afya ya engineer huyo.
Maisha nikutegemeana, sijasema daktari hana manufaa kwenye jamii ila kutegemeana kwao ndo kunatufanya tuenjoy hii dunia tunayoishi now.
 
Pale kushoto baada ya Viktoria kuna ghorofa kubwa sana liko na matege fulani(Slanted) ni kama Ghorofa 15 au 20 hivi. Ni la Mhandisi,just for your information,na ni hela za Consultancy Services tu. Achana na hawa Graduate Engineer,Engineer mbobezi anakula hela ndefu kushinda hao Madaktari,kwanza Engineers wako kwenye miradi ambayo ni Billions of Money,kwenye udaktari ni kama wito,hizo million 6 au 7 ni ndogo sana kwa Mhandisi.
Ndo maana tunasema madaktari walipwe zaidi maana hawana fursa zinginezo za kupata pesa ndefu kuliko wahandisi
 
Hivi kwanini,Taasisi huwa Zina lipa mishahara Minono?
Nahitaji kufahamu
Mkuu umechanganya hapo,Tanroads ni Kama shirika la umma ama taasisi mishahara ipo tofauti na halmashauri ama serikali kuu,ulichofanya wewe umelinganisha daktari wa halmashauri na mwandisi wa taasisi.
Sasa nakupa home work linganisha daktari wa TFDA,NHIF,TANAPA na BOT na mwandisi anayefanyia huko.

Tena linganisha daktari wa halmashauri na hospitali au wilaya na mwandisi wa halmashauri au wilaya.
 
tatizo dr anaajiliwa na wizara na sio taasisi kama ilivyo kwa mhandisi wa TANROAD, laiti kungekuwa na shirika au taasisi inayojiendesha yenyewe upande wa afya wangekula ndefu sana. mishahara mikubwa katika mashirika makampuni na taasisi za serikali lakini serikali kuu nothing. mfano nenda shirika la Elimu Kibaha pale ml wa degree anaanza na 1M lakini wa wizara 700k even madaktari pale ni juu. yote ni kwa sababu hizi taasisi zinatoa salary inayopamgwa na board
Kipi kinafanya, Taasisi kuwa na Mishahara Mikubwa?
Kunatofauti Kati ya
Mamlaka na Taasisi?
 
Kaka nimekuelewa.
Ila hujanielewa vema
Mimi nikiwa specialist nikawa na vichaka vitatu kwa kufanya kazi masaa sita Sita mwishoni nina mshahara wa 21 million ukionganisha vichaka vitatu.
Posho za bima ya afya na za watu wa clinic bado na ukizingatia madaktari bingwa ni wachache maana inachukua miaka 9 kusomea huyo ni normal specialist.
Haya bado hujamgusia conc specialist ambaye alisomea specialization kwa miaka 3 akaongeza miaka 2 tena.
Huyo anakua km mwalimu at the same time daktari bingwa wa mabingwa na hapa bongo wapo wachache asee huyo mshahara mmoja tu ni million kumi kagusa bado wa kuwa kama mkufunzi wa madaktari wengine ni zaidi.
Tatzo engineer mpk project ije ilhali doctor daily hela zinakuja
Kwa aina hii ya ma specialist ni sawa wanaweza kuwa vizuri zaidi lakini inategemeana pia na lobbying maana mhandisi haumii sana kupiga pesa kama daktari
 
Kuna generators mkuu.
Ila kumbuka hawa electrical engineers wanazimiwa umeme kama wakifanya marekebisho no risk
Na source zingine za electricity km generators zipo.
Ila sasa ukishategua mshipa mmoja ktk mwili wa binadam kwa kukosea kufanya surgery au kwa kumchoma sindano mgonjwa ktk mshipa usio sahihi unampa ulemavu wa milele na hakuna replacement km inayofanyika ktk sources of electricity
Hizo source nyingine katengeneza daktar au Engineer wa Mitambo?
 
yameanzishwa na kanuni za bunge mf TANROAD hajanzisha waziri wala rais bali kanuni zake zimetungwa bungeni even namna ya mishahara kuwa hupangwa na board hujawahi sikia kamishna wa TRA kulipwa 35M kwa mwezi. zimepewa meno na bunge sio kama wewe uliopo wizarani
Thanks,Hizi Mamlaka za Mabonde (Water Basins)
Eg
Wami/Ruvu Basins
Rufiji Basins
Nazo huwa zimeanzishwa kwa kanuni au Ni part za Idara ndani ya wizara ya maji?
 
Me mwenyewe ni engineer ila doctors ni sahihi walipwe zaidi ya wanavyolipwa sasa napendekeza wazidishiwe mara mbili ya wanavyolipwa sasa hasa neurosurgeon ni viumbe adimu duniani hao watu shule zao ni ngumu sana, sasa hawa madaktari wanafunzi wana module inaitwa pathology sijui ni mwaka 2 au 3 aisee ni ngumu hatare then mazingira yao ya kazi si mazuri.naona hamuwaelewi kabisa wanachopigania na wao pia ndo maengineer wa mwili wa binadamu
Huu ndio uungwana,wahandisi wana fursa nyingi za lobbying ya pesa lakini kwenye projects posho za supervision tu zinaweza zidi salary mara dufu zaidi hapo bado ten percent kutoka kwa wakandarasi
 
ukizungumzia kuhusu risk labda unasemea risks za namna gani??
Kwamba hujui kukutana na wagonjwa inahatarisha afya zao? Wewe mwalimu una risk zipi kazini? Huna dharura,unapewa holidays na wikend afu unaongea nini mkuu
 
Umenikumbusha Enzi za utoto/ujana
ukisikia kabinti kamemkubali Fulani,na wewe unaenda kuomba mahusiano,ukikataliwa analalamika kwa kusema " mbona ulimkubali fulani na mimi unanikataa..?"

Na wewe kwa kulinganisha fani za watu hapo ndipo ulipokosea.
Nikuulize kwani huyo daktari hakujua ni wapi wanatoa mafunzo ya uhandisi?
Na tunapozungumzia wito,tunazungumzia msukumo wa ndani uliokusukuma kusoma fani
Fulani na si fani nyingine.Huo ndo wito,shida inakuja kama ulisoma kwa kufuata mkumbo lazima ulalamike.
 
Angalia muda wanaokaa darasani na kumbuka hizo ni gloss salary take home hapo ni 800,000 yaani hiyo ndio ya kuitafuta kwa miaka 5 university?

Kuna mtu anaitwa faiza foxy sijui Kama ashakutembelea Mana ulivyokomaa na hyo gloss n hatari.

Kila kitu kina mazingira yake ya ufanyaji kazi na kipato chake Kama unajiuliza kuhusu Hilo mbona hujafikiria mwalimu n sh ngapi vp huyu mwanasiasa tunayemtuma kila Jimbo atuwakilishe kwenye kutunga sheria zile pesa zote n zann?

Hata mkulima naye anateseka tuu anashinda shambani kwa tabu miez minne lakin dalali anakuja kuchukua kiulain Tena kwa pesa ambayo mkulima haitaki hata huyo mlaji wa mwisho ananunua karibu Mara tano ya mkulima lakini vipi mkulima anhekutana na mtu wa mwisho akamuuzia kwa nusu ya Bei ya dalali au mfanyabiashara ?

N hapo tuu kilimo kingekuwa n uti wa mgongo ila kiuhalisia kilimo n kukosa inshu ya maana ya kufanya naamini kwa hilo.
 
Udaktari tiba ni fani nyeti na ngumu sana lakini cha kushangaza daktari anapata salary ya Tsh.1,500,000 gloss hukuhandisi wa Civil pale TANROADS(case study) anapata 2,000,000
Clinical officer/tabibu =950,000 huku Civil Technician=1,118,000 per month

Kwa staili hii case za rushwa zitaisha huko hospitali na vituo vya afya?

Tafadhali serikali wapeni madaktari uzito unaostahili kwenye malipo,wanatumia kusoma na wanaumia kazini.

Hata kwenye stahiki za posho na benefits zingine daktari hamfikii mhandisi lakini pia mhandisi hasa wa civil wako kwenye industry ambayo possibility ya yeye kupata pesa ni kubwa kuliko watu wa afya hadi semina zije.

Chonde chonde serikali mnapopanga viwango mliangalie hili na ule mpango wa kuwianisha malipo ya wafanyakazi walio na elimu moja limeishia wapi?
Ikumbukwe ofisi ya daktar ni kwenye risk ya afya yake,anapambania uhai wa binadamu,anasoma kila siku ili akuokoe....mwalimu anastahili ila Dr is the second one after God........
 
Mkuu hapo kwa Clinical officer 950,000/= mbona kama sio kweli?

C.O anachukua 680,000/= kama take home na kabla huwa haizidi au haifiki 850k..ninaye ndugu yangu C.O
Kwa private mkuu 950,000.
Nilifanyaga mm ktk vituo vya afya vya taasis ya kiislam mkuu.
Hata mshahara wa MD wa serikali ni tofaut na private sielew kwann ipo hivi
 
Ugumu upo kila sehemu usifikiri upo kwenu tu kikubwa ni kila mmoja kutambua na kuthamini profession ya mwenzake na siyo kujikweza muonekane too special kuliko wengine huo ni ushamba.
Dah kaka hatujajikweza Umeshinda maana duuuh!
 
Jengo unalotumia kufanya operation hujui Engineer kahusika?
Ambulance inayotumika kuleta wagonjwa hujui kua injinia kahusika katika utengenezaji wake?
Barabara je?
Huwezi fanya comparison za kitoto hivyo... engineer hajengi ana design yy hata tofali hashiki, basi bora huo mshahara wake wapewe wale vibarua wanaopanda juu na matofali...
 
Back
Top Bottom