Daktari anayetuhumiwa kwa utoaji mimba ashitakiwa kwa Uhujumu uchumi

Daktari anayetuhumiwa kwa utoaji mimba ashitakiwa kwa Uhujumu uchumi

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Daktari, Awadhi Juma (40) kutoka Hospitali binafsi ya Dental Clinic, iliyopo Sin ( 640 X 640 ).jpg


Daktari wa Dental Clinic iliyoko Sinza Mori, Dr Awadh Juma mkazi wa Kunduchi ambaye anatuhumiwa kwa utoaji mimba ambao ni kinyume cha sheria za nchi , amefikishwa kwenye Mahakama ya hakimu mkazi ya Kisutu akishitakiwa kwa makosa 7 likiwemo la utakatishaji wa kitita kikubwa cha pesa za kitanzania cha shilingi 260,000 ( laki mbili na elfu sitini)

Pamoja naye ameshitakiwa pia muuguzi wa clinic hiyo aitwaye Kidawa Ramadhan ambaye ni mkazi wa Manzese.

Kesi hiyo iko mbele ya Mh Hakimu Vicky Mwaikambo, ambapo mashtaka yamesomwa na Wakili wa serikali Simon Wankyo akisaidiwa na Glory Mwenda .
 
Daktari wa clinic moja iliyopo Sinza leo amepandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uhujumu uchumi.

Screenshot_20191227-185219_Twitter.jpg
 
Kwasasahivi ieleweke kuwa kila uvunjfu wa sheria ni ML.
So ML ni pi 3.14 ama k kwenye kila kosa
 
Mawakili wasomi wangetusaidia katika hili, ili ikiwezekana tufute sheria zote ili ibakie hiyo ya uhujumu uchumi pekee.

Maana kila kosa siku hizi linahamishiwa kwenye uhujumu uchumi, utakatishaji fedha na uendeshaji wa magenge ya uhalifu! Lengo Mtuhumiwa akose dhamana, na hivyo aozee mahabusu mpaka hapo atakaponyooka!

Sasa unajiuliza, Rais anataka msongamano magerezani upungue! Halafu wasaidizi wake ndiyo kwanza wako mstari wa mbele kuiongeza hiyo misongamano kwa kupindisha sheria kwa makusudi kabisa ili tu kuwakomesha baadhi ya watuhumiwa! Hii inachanganya sana kwa kweli.
 
Back
Top Bottom