Tetesi: Daladala route ya K.koo na Posta toka Mbezi na Kimara imezuiliwa

Tetesi: Daladala route ya K.koo na Posta toka Mbezi na Kimara imezuiliwa

Mbona mimi napanda na mizigo kila mara, labda wewe unataka kupakia magunia ya viazi.
 
Mbona zinajaza sana abiria na joto la hapa inakuwa kero hata maana ya mwendokasi inakuwa haipo tena..kazi kupumliana na kupata hewa chafu ya vkwapa vya watu
 
Habari wana board..

Leo wakati Niko kwenye daladala toka Mbezi kwenda Simu2000 nilimsikia konda akitoa hii hoja.

Kwa maelezo yake ni kuwa kwa sasa ni magari ya mwendo kasi tuu ndio yanayo ruhusiwa kuchukua abira kutoka Mbezi, Kimara kwenda k.koo na Posta.

Daladala ambazo zilikuwa zinatumika kwa njia hiyo, kwa sasa zinatakiwa kuishia Ubungo.

Lakini kubwa zaidi ni hili, magari ya mwendo kazi hayabebi mzigo wa aina yoyote, sasa kama tujuavyo k.koo ni sehemu ambayo wafanyabiashara wengi wanaenda kuchukua bidhaa zao, hii kwa upanda Fulani itaongeza ugumu wa biashara kwa wafanyabiashara Hawa.

Lakini pia hata kwa wale wanaoenda Posta, yaani feri, Hawa pia watakutana na ugumu.

Baadhi ya watu wa daladala walienda Sumatra kulalamika, lakini jibu LA Sumatra ni kuwa na wao wamepewa order ya kufanya hivyo, ingawaje wanajua kuwa italeta changamoto kwa abiri.

Wakatoa ushauri kuwa, abiria na wadau wengine waandike barua ili wao wapate nguvu ya kupata sehemu ya kusimamia na kurudisha utaratibu wa awali.

Kumbuka, hizi ni tetesi, kama kuna mtu ana maelezo kamili tafadhali tujuze ili tuweze kulipinga Kwa pamoja.

Fursa kwa wenye vigari vya mizigo, Safi sana.
 
Na hayo ni moja ya masharti yaliyofikiwa kati ya serikali na hao wanaoendesha huo mradi,kuwa pasiwepo na ruti ya daladala ktk njia hiZo kinyume na hapo ni kukiuka mkataba na kutawafanya hao waendeshaji wa huo mradi kusitisha na kuidai fidia serikali kwa kuvunja makubaliano yao,KINACHOWEZA KUFANYIKA NI KUWASHAWISHI HAO WAENDESHAJI WA HUO MRADI KUKUBALI KUBEBA MIZIGO NA SIO KURUHUSU DALADALA NJIA HIZO.
Kwani ukiwa na mzigo kama beg,au kifurushi cchako Mwendo kas huwa hawakubari eeee au tu kwa sabab hakuna nafas mle ndan?
 
Taxi,Bajaji na Bododaba wale wapi?
Mie nawapongeza kwa kuikatisha route hii ili kipato kigawanyike.

Na nyie watu wa Mbezi na Kimara mmekuwa bahili kuliko wa Mbagala?alaaa
Kama unamzigo ukishuka chukua Bodaboda au taxi au Carry kabisaa na wao wapate
Hivi kwa mfano mtu anatoka ubungo kwenda kigambon ukodi tax? Au. Unaongea tu?
 
Kwani mwendo kasi wanakosa abiria au ni tamaa tu na uchoyo wa kuwazuia wengine?,*migar yenyewe tunabanana kama disco la welcome form one!!
 
tutaisoma namba mwaka huu km nini watuwekee na gari za mizigo
 
Inawezekana ni kweli hata MI nilisikia mwisho wao utakuwa mwezi kumi. Hata ukiwa unatoka makumbusho mwisho wake unaishi kwenye Ile round about mpya pale shekilango ili watu wapande mwendokasi ndio maana baadhi ya daladala ziliwahi root mpya mapema zikaandika makumbusho to gerezani kupitia mabibo. Ndio maana kama unatoka kariakoo Kuja makumbusho kupitia sinza utakesha kusubiri daladala ziko chache na nyingi zimebadili route mapema
 
Na kuna upuuzi wa hali ya juu uko pale, kuna wakati unafika pale hawana tiket wala hawana machine ya recharge kadi zao, sasa kama kadi yako haina pesa sijui ufanye nini?

Na wizi wa sh 50 kwenye vituo Ndio umeshika kasi, mpaka wakatisha tiket wameshaona kuwa Ile 50 ni haki yao,
Hivi ni kweli hizo 50 bank hazipo? Au kimradi cha kitapeli hiki kinalipa sana
 
Wakati mwingine tunapanda daladala kwa safari fupi labda kutoka
*manzese mpaka mwembe chai
*magomeni mpaka fire
*usalama mpaka jangwani
*akiba mpaka posta
Hakuna ulazima wa kukata tiketi na kukaa foleni kusubiri mwendokasi, pia sehemu ikiwa fupi tunalipia 300-400 hakuna haja ya kulipia 650, kwa kifupi 1,300 ni kubwa kwa vituo vya karibu karibu kwenda na kurudi.
 
Ambaye ni mdau katika sekta ya usafiri wa daladala, hao madereva na makondakta wao hupata habari kwanza kabla ya kukufikia wewe msafiri.
Si vizuri kudharau ni vyema kama una shaka uangalie comment za uthibitisho.
kusisitiza kwangu kua chanzo cha habar konda ni dharau????
 
duuh hii sasa kali uwiii ngoja nirudi zangu mwanza hadi muafaka upatikane nitarejea
 
Kwangu mimi hili ni jambo ovu zaidi kuwahi kutokea hapa Tanzania. Hilo la daladala na hili la bodi ya mikopo ni mambo ya kulaaniwa sana.
 
Mamia ya wananchi wanaotumia usafiri wa mabasi ya mwendo kasi wamejikuta wakikwama kwa masaa kadhaa katika stendi ya Mbezi kufuatia kuwepo kwa idadi kubwa ya abiria isiyoendana na mabasi yaliyokuwepo kituoni hapo kufuatia mabasi madogo yaliyokuwa na vibali vya kusafirisha abiria kufikia tamati hii leo.
Pia abiria wamehoji watafikaje Muhimbili kutoka Mbezi kwa kuwa hakuna mabasi ya mwendo kasi kwa route hiyo
 
Back
Top Bottom