Dalili 10 kuonesha kwamba wewe uko kihisia zaidi

Dalili 10 kuonesha kwamba wewe uko kihisia zaidi

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
6,514
Reaction score
15,247
Screenshot_20241119_142130_Google.jpg


Unashindwa kusema HAPANA kwa watu wengine kwasababu unawajali sana

Unaweza kulia ukiwa mwenyewe na hauwashiriki wengine mambo yako, kwasababu unahofu watakuonaje

Huwa unafikiri kila mtu unayekutana naye ni rafiki yako na kutaka kuwasaidia hata kama wako na wewe kwa mda mchache

Uko mkarimu sana kwa watu na unawakirimu vizuri,na unategemea kuwa watakuwa wakarimu kwako pia

Hauoni mapema pale watu wanapo kutumia kwa manufaa yao,kwasababu wewe huwezi kuwafanyia hivyo

Huwezi kuwahumiza watu wengine kwa makusudi kwasababu una moyo mzuri sana

Unajikuta kwako ni vigumu sana kuwaeleza watu wengine hisia zako bila kuguswa na hisia zako au kuumizwa na hisia hizo

Unaweza kugundua hata baadhi ya mambo madogo ambayo watu wanakufanyia lakini unashindwa kuyaongelea

Unajali sana kuhusu wengine kiasi kwamba unataka kujua au kuelewa shida zao na kutaka kuwasaidia

Unapenda kuwasaidia wengine kwa hofu ya kupoteza marafiki,lakini mwisho wa siku unaishia kuwa mpweke

Ni hayo tu!
 
tukirudi kwenye mada,

hizo sifa ulizozitaja ukiwa nazo nyingi ni kiashiria cha tatizo

unakuwa boya
Kwanza kuwa emotional sio tatizo kwa maana ndio ubinadamu wenyewe,Mungu anapenda tupendane na tusaidiane sana

Lakini kila jambo lina kiasi chake,kwa maana kwamba ukipitiliza inakuwa tatizo,chukulia kwamba unasaidia watu mpaka wewe unajisahau hapo ni shida

Au unafanyiwa mambo ambayo sio mazuri badala ya kuyaongea ili yatafutiwe sululisho wewe unaumia tu hiyo ni shida

Au kuna mambo huyapendi lakini unashindwa kusema hapana hilo ni tatizo
 
Kwanza kuwa emotional sio tatizo kwa maana ndio ubinadamu wenyewe,Mungu anapenda tupendane na tusaidiane sana

Lakini kila jambo lina kiasi chake,kwa maana kwamba ukipitiliza inakuwa tatizo,chukulia kwamba unasaidia watu mpaka wewe unajisahau hapo ni shida

Au unafanyiwa mambo ambayo sio mazuri badala ya kuyaongea ili yatafutiwe sululisho wewe unaumia tu hiyo ni shida

Au kuna mambo huyapendi lakini unashindwa kusema hapana hilo ni tatizo
kwa mwanaume ni mbaya sana, wanawake watakutumia mpaka basi
 
Nifanyeje ili niondokane na stress, overthinking, depression?
Stress/depression hutokea kwasababu kuna mambo ambayo ndio chanzo au visababishi vya hali hizo

Kwahiyo kwanza unatakiwa ujue je,ni sababu zipi zinakuletea stress baada ya kujua shida ni nini,basi itabidi unadili na hivyo visababishi

Overthinking ni kuyachambua mambo au kuyafukunyua kiasi kwamba inakuwa shida kwako,kwahiyo don't take things personal,na usipende kufuatilia sana mambo kiundani
 
Mbona umeegemea kusaidia watu tu

Hautaki watu wasaidie wenye shida

Utakuwa wakala wa shetani wewe

Kusaidia watu nalo ni jambo hisia?

Upuuzwe
Usiwe na pupa bro chill,ebu soma andiko vizur kisha tafakari
 
Back
Top Bottom