Dalili za kupotea kwa sanaa ya uchoraji kutokana na matumizi ya IA (Artificial Intelligence)

Dalili za kupotea kwa sanaa ya uchoraji kutokana na matumizi ya IA (Artificial Intelligence)

Matumizi ya AI yameshika kasi, uwezo wa program hizi kutengeneza picha kutokana na maono au mawazo ya mtumiaji, kumeongeza wimbi kubwa la picha hizo zikitumika katika maeneo tofauti.

Wasi wasi wangu ni kwamba itafika wakati hakutokuwa na haja ya kuwa na wachoraji wa picha, kwasababu program hizi zinaweza kutafsiri mawazo ya mtu na kutengeneza kitu au picha ambayo inaendana na matakwa ya mtumiaji.

Program hizi zitaeneza uvivu wa kutumia muda mrefu kuchora au kubuni picha, picha za wachoraji zitakosa soko kwani kila mtu anaweza tengeneza picha anayo taka akiwa amekaa nyumbani kwake au katika simu yake tu.

Wengi wanadhani AI ni mkombozi lakini ni vyema kukumbuka kwamba matumizi yake huzidisha uvivu wa kufikiri na kutenda.
Hii ni kawaida kwa dunia kuhama au kupiga hatua ya kutoka kuacha hiki na kuanza kutumia kilngine ambacho ni rahisi zaidi, hatua hiyo huitwa ni maendeleo.

Hata tulivyokuwa tukitumia kulimia au kuendea makazini kwa nyakati hizo, sivyo tunavyovitumia leo. Kwa hiyo, hakuna haja ya hofu, ikiwa dunia iko katika mchakato huo.

Siku hizi hata vituo vya taksi hakuna, kila kitu kinaisha kwenya Uber, kwani imerahisisha sana kwa kunetea taxi nilipo na mwenye taksi kuletewa mteja alipo.

Na kuna App ya msaada wa kisheria inasukwa, ili asiye na uwezo wa kuajili Wakili, apate mwongozo wa kwenda na kesi kwa App tu. Au App ya Afya inayoweza kukupima afya.

Kikubwa, tunapaswa kuwa kama Mamba ili kuendana na mazingira yote kwa namna yoyote yakibadilika kwa maendeleo. Tukikaa na kulia lia, dunia itatuacha.

Ova
 
Hii ni kawaida kwa dunia kuhama au kupiga hatua ya kutoka kuacha hiki na kuanza kutumia kilngine ambacho ni rahisi zaidi, hatua hiyo huitwa ni maendeleo.

Hata tulivyokuwa tukitumia kulimia au kuendea makazini kwa nyakati hizo, sivyo tunavyovitumia leo. Kwa hiyo, hakuna haja ya hofu, ikiwa dunia iko katika mchakato huo.

Siku hizi hata vituo vya taksi hakuna, kila kitu kinaisha kwenya Uber, kwani imerahisisha sana kwa kunetea taxi nilipo na mwenye taksi kuletewa mteja alipo.

Na kuna App ya msaada wa kisheria inasukwa, ili asiye na uwezo wa kuajili Wakili, apate mwongozo wa kwenda na kesi kwa App tu. Au App ya Afya inayoweza kukupima afya.

Kikubwa, tunapaswa kuwa kama Mamba ili kuendana na mazingira yote kwa namna yoyote yakibadilika kwa maendeleo. Tukikaa na kulia lia, dunia itatuacha.

Ova
Ni kweli kwamba tunaishi katika dunia yenye mapinduzi makubwa ya technology, lakini isifike pahala technology hizi zikapoteza uwezo asilia wa mwanadamu.

Pia kila kitu kuhamia Digital ni dalili ya kwamba sasa tunaingia katika kifungo au gereza, mfano matumizi ya Digital Currency au digital ID. Huu ni mtego na tukinasa tumekwisha.
 
IA inachora picha kwa kutumia maelezo ya mchoraji, picha itakiwa nzuri maelezo yakiwa yana usanii ndani yake.

Mtu ambae sie mchoraji akitumia AI picha zake zitaendelea kuwa za kidwanzi tu yaani ameiambia AI ifanye upuuzi yenyewe haikatai inafanya ufala huo japo itachorwa picha ambayo hawezi kuichora.

Kinachotakiwa kieleweke ni kwamba AI ni tool unaweza kuitumia kuchora, sasa bas kama unajua kuchora AI itakusaidia kuchora picha kali. ila kama hujui kuchora AI wala haitakusaidia kuchora picha kali.

Kuwa na siraha bora sio kwamba ndo umeshashinda vita, wanafunzi O'level wanatumia calculator lakini still math is a problem. miaka ya nyuma calculator hazikuruhusiwa O'level lakini tulifaulu viziri(knowledge and math skills ndo zinatumika sio calculator)

same applied to AI inasaidia is just a tool hivyo kuchora picha kali ni mpaka unajua sanaa ya uchoraji.
 
Kusaidia ku translate Mawazo yetu ni jambo jema ambalo AI imeleta, lakini tatzo ni kushindwa kubuni na kuwa na uvivu wa kufikiri.
Nani amekwambia unashindwa kubuni ? Inachobuni ni akili au kalamu..., AI kama Kalamu inachofanya ni translation za fikra na ili upate kitu unachotaka lazima uende na ile prompt kwa ufasaha na ili iwe unique unaweza ukaongeza manjonjo kwahio inasimplify kazi ya mbunifu..., Tungeendelea hivi hata nguo tungesema ziendelee kushonwa na mikono sababu mashine zinapunguza artistic input (there was a time kabla ya uzinduzi wa knitting machines ushonaji ulikuwa unafanywa kwa mikono tena pengine ni silk iliyokuwa inayokusanywa kutoka kwenye wadudu)
 
Dr Dre kipindi wanafanya kazi walikuwa wanachukua manjonjo na sampling kutoka huku na kule hata mtu akitaka mlio wa kuvunjika glasi inabidi ivunjwe sasa hivi kuna keyboard unabonyeza tu unapata mlio wowote (kwahio imewezesha hata msanii chumbani kwake kutoa kazi na sio kwenda kubembeleza studio)....

We should embrace every new technology and take it on the stride..., mambo ya kufanya bado ni mengi...., in the end what matters ni product na kama product ni superior who cares..., Shida sababu teknolojia hii ipo wazi unapata a lot of mediocre quantity ambayo ina dilute quality ni vigumu kukutana na kazi nzuri kama inabidi uchuje upuuzi mwingi ili kufikia quality.... (In short quantity imekuwa nyingi)
 
Dr Dre kipindi wanafanya kazi walikuwa wanachukua manjonjo na sampling kutoka huku na kule hata mtu akitaka mlio wa kuvunjika glasi inabidi ivunjwe sasa hivi kuna keyboard unabonyeza tu unapata mlio wowote (kwahio imewezesha hata msanii chumbani kwake kutoa kazi na sio kwenda kubembeleza studio)....

We should embrace every new technology and take it on the stride..., mambo ya kufanya bado ni mengi...., in the end what matters ni product na kama product ni superior who cares..., Shida sababu teknolojia hii ipo wazi unapata a lot of mediocre quantity ambayo ina dilute quality ni vigumu kukutana na kazi nzuri kama inabidi uchuje upuuzi mwingi ili kufikia quality.... (In short quantity imekuwa nyingi)
Ni kweli lazima tutumie fursa za teknolojia kama hizi, lakini bado tunapaswa kuwa makini kwasababu lengo hasa la AI sio kutoa msaada bali ni kuzidi kupunguza uwezo wetu wa kufikiri.

Ni vyema kufahamu kwamba kuna vita inaendelea dhidi ya akili ya mwanadamu, kila siku uwezo wa watu kufikiri unapungua na kimbilio la wengi ni solution ambazo ni nyepesi au Kitonga.
 
Ni kweli bado watu wanachora na michoro hiyo ina thamani kubwa, lakini huu ni mwanzo tu wa matumizi ya AI na matokeo yake yamekuwa makubwa.

Madhara yatakuwa badae ambapo program hizi zitakuwa na matumizi makubwa hasa kwa vizazi ambayo technology itakuwa sehemu kubwa ya maisha.
Ni kweli mkuu ila kwa upande wangu sioni kama itachukua nafasi kubwa kiivo kama inavyotegemewa maana IA tuu yenyewe kuijua na kuanza kuimasta ni kimbembe
 
Ni kweli mkuu ila kwa upande wangu sioni kama itachukua nafasi kubwa kiivo kama inavyotegemewa maana IA tuu yenyewe kuijua na kuanza kuimasta ni kimbembe
Sahihi kabisa mkuu, Nadhani matokeo kamili yatakuwa kwa vizazi vijavyo, hao ndyo watabobea katika matumizi makubwa ya AI
 
Ni kweli lazima tutumie fursa za teknolojia kama hizi, lakini bado tunapaswa kuwa makini kwasababu lengo hasa la AI sio kutoa msaada bali ni kuzidi kupunguza uwezo wetu wa kufikiri.

Ni vyema kufahamu kwamba kuna vita inaendelea dhidi ya akili ya mwanadamu, kila siku uwezo wa watu kufikiri unapungua na kimbilio la wengi ni solution ambazo ni nyepesi au Kitonga.
Kwanza ujio wa AI umefanya watu wengi waingie kwenye hii tasnia ya ubunifu; Kwa kusema kwako AI hii ya Text to Image inapunguzia watu kufikiri ni kama unasema kwamba wachoraji ndio walibeba fikra za dunia wakati AI inasaidia computing ya vitu ili watu wa concentrate kwenye the fundamentals...

Kwa logic yako watu tungeendelea kutumia Four Figure table au abacus kusehabu badala ya scientific calculator au normal calculator
1719858912354.png
 
Kwanza ujio wa AI umefanya watu wengi waingie kwenye hii tasnia ya ubunifu; Kwa kusema kwako AI hii ya Text to Image inapunguzia watu kufikiri ni kama unasema kwamba wachoraji ndio walibeba fikra za dunia wakati AI inasaidia computing ya vitu ili watu wa concentrate kwenye the fundamentals...

Kwa logic yako watu tungeendelea kutumia Four Figure table au abacus kusehabu badala ya scientific calculator au normal calculator
Akili yako imeenda mbali...
Ila itatukuta hapa.
Tupo hapa na uwanja ni mpana kama kwa mkapa
 
Licha ya kupoteza kazi tu, pia inapunguza uwezo wa kufikiri na kubuni.
Sasa kama AI inaweza kubuni wewe ujiangaishe na nini?
Siku hizi hatupati tena shida na content za website, unawapa tu tittle, unapewa full content! Kupoteza ajira ni uoga tu, sawa sawa waliokuwa wanaogopa computer!
 
Sasa kama AI inaweza kubuni wewe ujiangaishe na nini?
Siku hizi hatupati tena shida na content za website, unawapa tu tittle, unapewa full content! Kupoteza ajira ni uoga tu, sawa sawa waliokuwa wanaogopa computer!
Siku hizi watu hawataki kujiangaisha na wamekuwa wavivu mno, kwangu naona hilo ni tatzo wala sio jambo la kufurahia.
 
Amini husiamini, Sasa hivi kwa ulaya na marekani picha za kuchora na wasanii zinathamani kubwa sana tofauti na wenye kipato tuu ndio wanaweza kuzimudu. Yaani Leo hii mtu akiletewa zawadi ya picha yake illiyochorwa kwa mkono wa binadamu inathaminiwa sana.

Siku hizi kwa mfano moja ya kitu muhimu na chenye gharama kwenye harusi ni picha ambayo maharusi wataweka pozi na mchoraji atawachora papo kwa papo., hii kitu sio kila wanaharusi wanaimudu
 
AI inasifiwa saaaanaa lakini tusichokijua ni watu kupoteza ajira.

Elimu haitakuwa na thamani tena

. Huu ni uhuni tu wa makampuni makubwa kujitengenezea pesa na kutokulipa kodi.

Watu wengi watapoteza kazi. Just saying
Na pia vijana wetu watakuwa wavivu sana kufikiria na kubuni vutu mbalimbali
 
Amini husiamini, Sasa hivi kwa ulaya na marekani picha za kuchora na wasanii zinathamani kubwa sana tofauti na wenye kipato tuu ndio wanaweza kuzimudu. Yaani Leo hii mtu akiletewa zawadi ya picha yake illiyochorwa kwa mkono wa binadamu inathaminiwa sana.

Siku hizi kwa mfano moja ya kitu muhimu na chenye gharama kwenye harusi ni picha ambayo maharusi wataweka pozi na mchoraji atawachora papo kwa papo., hii kitu sio kila wanaharusi wanaimudu
Picha za kuchora bado zina thamani kubwa, waswas wangu ni hapo badae ambapo matumizi ya AI yatakuwa makubwa na watu wa kizazi hicho kushindwa kuipa thamani michoro ya picha.
 
1. Leonardo da Vinci
2. Vincent van Gogh
3. Pablo Picasso
4. Michelangelo
5. Claude Monet
6. Rembrandt van Rijn
7. Salvador Dalí

Hawa jamaa sanaa zao za uchoraji zinaheshimika na kupata thamani kubwa hadi sasa .
 
Back
Top Bottom