Dalili za kupotezea maeneo inayotawala M23

Dalili za kupotezea maeneo inayotawala M23

Hivi Tshisekedi mzima kweli yule? Tulitegemea amobilise vikosi vizito vizito ndio kwanzaa anasusa? Hata kuna kitu nakinusa hapa kumbe ndio maana baadhi ya nchi zilitoa majeshi huko huu ni mpango flani wa kipuuzi na upuuzi tena,
 
Kuna taarifa maeneo mengi ya Bukavu yameanza kurudishwa na Wazalendo toka mikonono mwa RDF ambao wanajiita M23 ukweli juu ya hili upoje?
Yes ni Kweli, Nina jamaa yangu Bukavu ni Mcongo, ananieleza kuhusu Wazalendo.

Wazalendo ni Vijana walioamua kujikusanya Pamoja kukamata silaha na kuamua wao kama wao kupambana na M23, hii bila ya amri ya Serikali Wala muongozo wa Jeshi la Serikali, kumbuka Vijana wengi huko Kivu wanajua kutumia Silaha, na Sasa Wana Silaha nyingi ambazo walizichukua baada ya Jeshi la Serikali hapo Bukavu kukimbia.

Na majuzi kukatokea majibizano ya Risasi baada ya Jeshi la Serikali kuingia Bukavu kutoka miji mingine na hao Wazalendo..... Naambiwa baadaye wakaelewana, na Sasa wamewapa Silaha zaidi....! Nikitizamq baadhi ya video, Yani Wazalendo wanaonekana wana hasira na machungu kuliko Askari wa Jeshi, wanapopita mtaani hivi, unaona Vijana wengine wanatoka majumbani wanawakimbilia kuwapa pesa, na wengine wanaomba kujiunga nao.

Jamii inawa support Kwa Vijana wengi kujiunga nao, kuwapa madawa na chakula......! Wamefanikiwa kuwarudisha nyuma M23 Toka maeneo ya Bukavu mjini.
 
Sisi wakongo twapenda tuwe sehemu ya Rwanda.Rwanda ni Nchi mzuri sana kuliko zote afrika mashariki
 
Kuna taarifa maeneo mengi ya Bukavu yameanza kurudishwa na Wazalendo toka mikonono mwa RDF ambao wanajiita M23 ukweli juu ya hili upoje?
Wazalendo Jazi waliingia waliingia mjini goma na wakashambulia na ku retreat.
 

Attachments

  • VID-20250303-WA0000.mp4
    2.8 MB
Yes ni Kweli, Nina jamaa yangu Bukavu ni Mcongo, ananieleza kuhusu Wazalendo.

Wazalendo ni Vijana walioamua kujikusanya Pamoja kukamata silaha na kuamua wao kama wao kupambana na M23, hii bila ya amri ya Serikali Wala muongozo wa Jeshi la Serikali, kumbuka Vijana wengi huko Kivu wanajua kutumia Silaha, na Sasa Wana Silaha nyingi ambazo walizichukua baada ya Jeshi la Serikali hapo Bukavu kukimbia.

Na majuzi kukatokea majibizano ya Risasi baada ya Jeshi la Serikali kuingia Bukavu kutoka miji mingine na hao Wazalendo..... Naambiwa baadaye wakaelewana, na Sasa wamewapa Silaha zaidi....! Nikitizamq baadhi ya video, Yani Wazalendo wanaonekana wana hasira na machungu kuliko Askari wa Jeshi, wanapopita mtaani hivi, unaona Vijana wengine wanatoka majumbani wanawakimbilia kuwapa pesa, na wengine wanaomba kujiunga nao.

Jamii inawa support Kwa Vijana wengi kujiunga nao, kuwapa madawa na chakula......! Wamefanikiwa kuwarudisha nyuma M23 Toka maeneo ya Bukavu mjini.
Pole yako. Ila tu cha kukushauri, za kuambiwa changanya na za kwako. kwa hiyo, Wazalendo wapo bora kuliko jeshi lenyewe! Si ndio! Yaani mtu wa kufundishwa kutumia bunduki siku mbili tatu,tayari ana mbinu za kijeshi kukabiliana na M23! We usicheze kabla ya mziki. Huyo ni mmoja, tafuta na wengine, Soma taarifa magazetini, huku unasubilia walau hata wiki hivi. ndo utajua uharisia wa ulichoambiwa.
 
Hili jambo naliongelea mimi kama mimi na kwa uelewa wangu.

Ni kweli, Makenga aliwahi kuwa mwanajeshi wa RDF. Kama kina Kagame walikuwa wanajeshi Uganda.
Mpaka hapa, kila mkimbizi anaweza kulihudumia jeshi la nchi furani,hasa hizi zetu, lakini uhalisia akiwa si raia.

Kwa M23, hao unaowasema, historia yao, wengi wao wakiwa wakimbizi Rwanda, waliweza kuingia jeshini.
Penda usipende, watutsi wa DRC na Rwanda ni wamoja.
Jeshi la Rwanda, unalijua uwezo wake. Huo huo, ndo wa M23. Na nahisi pengine, ndo maana sasa hivi kutofautisha hizi pande mbili ni ngumu.

Jambo usilotaka kuongelea, ni uwepo wa mataifa makubwa yanayotumia mgongo wa watu kupata yanachokipata. Kwa taarifa za wanaojua, inasemekana hakuna nchi yenye utajili wa madini duniani kama DRC.

Nadhani ulisikia kesi ya Apple, kuzuiliwa kununua madini ya DRC. Sasa, itafunga kiwanda? Wengine, watafunga viwanda?
We ni mmoja wao, ndio maana unapinga drc kukombolewa toka kwa waasi.
 
Kama watu wa Goma wanaishi vizuri chini ya M23 ni kheri kwao. Hicho ndiyo muhimu.
 
Back
Top Bottom