Ukweli ulio wazi ni kwamba .......
Kizazi cha mistari nondo uzao wa Fid Q kikiandika mtari mmoja Mtu kama Mwana FA ili alete maana ile ile anaandika Nyimbo nzima,
Angalia mfano:
"Pole pole... ndio mwendo kila akikumbuka inamuuma, kwanza viliumbwa vidole binadamu ndio akaunda uma" By Fid Q
"Naona mlango wa pepo ila sioni pakutokea, hii pesa imetoka jando inataka kuni babu sea" By Stamina
"Usimpige mkeo mpige shangwe, maana Young killer sio ngazi kwahiyo mwambieni shetani asinipande " By Msodoki BestMan
Huyo mwana FA wenu akitaka kuimba alete maana ya mstari wowote kati ya mistari hiyo basi ataandika nyimbo nzima,
Mfano mdogo, nyimbo nzima ya usije mjini Killer anaweza kuiandika kwa mstari mmoja ukasimama kuliko nyimbo nzima ya mwana FA,
Sasa msiwe mnafloo bila fact write down, mkishupalia mwana FA mkali bila vigezo na sababu mnakuwa na mapenzi tu hamna sababu.
CC:
kende youngd diCaprio Honey Faith Viol Farha
Hebu hesabu Punch humu ndani ya wimbo mmoja then urudi kulala;
MWANAFALSAFA
(Verse 1)
ukiwa fukara kamwe huwezi kuwa kiburi
maskini jeuri ni msemo tu
Usiuweke kwenye akili
Mwanaume kuwa tajiri ni kama demu kuwa
mzuri
Demu wako akiwa kwenye kioo we piga simu
utafute deal
Hela hazilali so ukilala wewe tu
Na zina kasi ya kutengenezwa hazikungoji
uamke mkuu
Me na make money mchana na make money
usiku
Iwe kwa tai au kwa jeans me naingiza mkwanja
tu
Naingiza mkwanja na jua na naingiza totoro
Mwenzangu sio unazbagua me sina nazo
mgogoro
Begi mgongoni na ramani kama mzungu
kabla hujafika ulipo nshafaham my next move
Pesa ni rock me ni roho
Wana wa long time ago
Uwezi kutuachanisha
Waliodei wote wanafall
Mikuki imepotea farasi wanarudi wenyewe....
Wale waliopanda wakati wa kwenda wanaomba
wafufuliwe
(Chorus)
(Usinipigie makofi utachoka mikono itauma
cause utamic nyingine
unanijua unaniskia)*2
Punch line zinafuatana
unanijua unaniskia
punch line zinaongozana unanjiua unaniskia
punch line zimegandana
unanijua unaniskia
So usinipigie makofi mikono utachoka
(verse:2)
Inakera kujua majibu na watu hawayulizi kutu
We unajua sie hatujui ila kaa navyo vyote kutu
Maisha kama ubao ila ayaandikwi kwa chalk
Siwezi kukupa vyote ujue na kwangu zimebaki
Mimi ile mitego ya mission na mission kabla ya
kudanja
Ya kwanza kuwa na mkwanja na ya pili kuwa
na mkwanja
Namweka mungu kwanza dunia inashindwa
nivunja
Nusu haramu nusu halali
Upande shehe na upande ninja
Kila bosi na bosi wake
Kama mnyonge na mnyonge wake
Mola alikupa punje na punje akawapa wengine
hakutaka unyanyaswe wala
unyanyase watu wake..
Alichokupa me hakunipani vyetu tutumie wote
Ukipata nusu ina maana umekosa nusu
Na tuseme ya mpoki au masanja we
hayakuhusu
Ni siku ya kwanza ya maisha yangu yaliyobaki
Hivi navyotaka iende
Huu wimbo ni man respect
repeat(chorus)
Unanijua unaniskia *2
(verse:3)
Sina mjadala na ujinga sina nafasi ya kuuweka
Umri unasonga sina muda
Mvi znasogea zitafika
Sipunguziki mimi kama bei za supermarket
Tuna uzito tofauti kama wa shuka na blanketi
Naisafisha sabuni ndo inisafishe maungoni
So usininyooshee kidole
We ni mchafu zaidi ya mimi
Wenzako hawaombi wanashukuru
Wanapenda walichopata
Omba samaki upewe nyoka
Omba upewe usichotaka
repeat(Chorus)