Dan Friedkin mmiliki wa AS Roma anamiliki ardhi kubwa Tanzania, mamlaka zimchunguze

Dan Friedkin mmiliki wa AS Roma anamiliki ardhi kubwa Tanzania, mamlaka zimchunguze

BLACK MOVEMENT

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2020
Posts
4,548
Reaction score
11,901
Hawa wanaweza kuwa ndio wale wafadhili wa Royol tour ambao tulifichwa , sasa wanapewa mapande ya aridhi, na wana binasifisha, fikiria Mzungu ana binasifisha Aridhi ya Umma.

FB_IMG_1683223385154.jpg


======

Tanzania ni nyumbani kwa moja ya hifadhi bora za wanyama barani Afrika, ambayo inafanya iwe sehemu ambayo inapenda kutembelewa sana na watu wengi ulimwenguni, lakini kisichojulikana ni kuwa kuna hifadhi ya wanyama ya Mwiba ambayo inamilikiwa kibinafsi na bilionea Mmarekani.

mwiba-1.jpg


Mmiliki wa hifadhi hiyo anajulikana kama Bilionea Dan Friedkin, ambaye makao yake makuu yako Texas, ni Mwenyekiti wa Gulf States Toyota.


Dan Friedkin.jpg


Bilionea Dan Friedkin

Kulingana na makala ya Forbes, mfuko wa familia yake, Friedkin Conservation Fund (friedkinfund.org), unashiriki kikamilifu katika uhifadhi wa Afrika Mashariki na umekodisha ekari milioni 6 za eneo la pori la Tanzania kwa lengo la kulilinda.

Haijulikani bilionea alilipa kiasi gani kuipata hazina hii, lakini inasemekana kuwa hifadhi hiyo ilifanywa kuwa ya binafsi mwaka 2009.

Mwiba, ambayo inaenea zaidi ya ekari 125,000, inapakana na mpaka wa Magharibi wa eneo la uhifadhi la Ngorongoro na sehemu ya Kusini ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti

Uhamaji wa nyumbu wa Serengeti hupita kupitia Mwiba kati ya Desemba na Aprili. Ikiwa na vilima virefu, msitu mnene, mashimo ya maji na mito (iliyokauka) ambapo mabwawa hutokea, maji yake ya kudumu huvutia wanyama pori mwaka mzima

Wageni ambao wamewahi kufika Mwiba wanasema ni kama sumaku ya wanyama wakati sehemu ya Kusini ya Serengeti na maeneo ya Hifadhi ya Ngorongoro yanakauka kati ya Julai na Novemba kila mwaka.

Kulingana na Friedkin, Logde ya Mwiba, ambayo gharama yake ni dola za Kimarekani 1,800 (Milioni nne na ushee za Kitanzania) kwa mtu, ilijengwa ili kuwa na uwepo unaofanana na mandhari ya sehemu hiyo.

"Utekelezaji wa muundo ulikuwa jitihada ya pamoja, lakini mke wangu, Debra, ndiye anayepewa sifa zote kwa wazo kumbukumbu tuliotaka kuwapa wageni wetu," anasema.

The Citizen
 
Hawa wanaweza kuwa ndio wale wafadhili wa Royol tour ambao tulifichwa , sasa wanapewa mapande ya aridhi, na wana binasifisha, fikiria Mzungu ana binasifisha Aridhi ya Umma.View attachment 2610183
Nafikiri ni wawekezaji tu sidhani kama ni wamiliki wa ardhi hiyo kwa kuwa sheria yetu ya ardhi bado hairuhusu ardhi kumilikiwa na mgeni bali mwekezaji tu kwa masharti.
 
Ninavyojua sheria yetu inaruhusu Mwekezaji kupewa ardhi kwa ajili ya uwekezaji ila mara uwekezaji wake unapokoma tu anarudisha ardhi serikalini.
Sheri ipi? Hawa wanakodishiwa kwa miaka 99, huyu amebakiza miaka kama 98 na hio aridhi, ndio maana na yeye ana kodisha au kubinasifisha tena kwa pesa ndefu kuliko alivyo kodishiwa yeye
 
Mwiba Game Reserve imekuwepo muda mrefu kabla hata ya awamu ya sita ila kama mtu mmoja tena ambaye sio raia anaweza kumilikishwa ekari 25,000 basi twafa.
Reporting iko exaggerated. Nadhani amekosea kuandika huyo reporter. Hiyo 24,281 km ni sawa na ukubwa wa mikoa ya Geita (20Ksq km), Kilimanjaro (13Ksq km), Njombe (21Ksq km) au Mtwara (12K sq km)
 
Sheri ipi? Hawa wanakodishiwa kwa miaka 99, huyu amebakiza miaka kama 98 na hio aridhi, ndio maana na yeye ana kodisha au kubinasifisha tena kwa pesa ndefu kuliko alivyo kodishiwa yeye
Amekodi ardhi tu miaka ikiisha anaachia ama anaendelea, na kama madini yapo haruhusiwi kuchimba.

Madini ya Tanzania yanatawaliwa na Sheria ya madini ya mwaka 2017.

Hata nyumbani kwako ambako unayo Title Deed, ukikuta dhahabu ni mali ya Serikali. Ila wakikuta bangi ni mali yako
 
Hawa wanaweza kuwa ndio wale wafadhili wa Royol tour ambao tulifichwa , sasa wanapewa mapande ya aridhi, na wana binasifisha, fikiria Mzungu ana binasifisha Aridhi ya Umma.View attachment 2610183

Niliwahi kuuliza kuna post jamaa walifanya tafiti kilimanjaro na wakagundua sijui madini gani huko..... bado nao sasa hivi tutasikia ile aridhi wanamiliki wao!!! Hekari 25000 duuh
 
Back
Top Bottom