TANZIA Dar: Ali Mohamed Kibao, kiongozi wa CHADEMA auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana

TANZIA Dar: Ali Mohamed Kibao, kiongozi wa CHADEMA auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana

Hii kitu inamchafua sana Mh. Rasi Mama Samia, asipofanya maamuzi mazito kukemea haya yanayoendelea hii nchi itamfia mikononi mwake.

Very sad new indeed.
 
Hii kitu inamchafua sana Mh. Rasi Mama Samia, asipofanya maamuzi mazito kukemea haya yanayoendelea hii nchi itamfia mikononi mwake.

Very sad new indeed.
Hili siyo la CHADEMA, bali wananchi wanapaswa kuja na utaratibu huu, hiyo ndiyo namna ya kujilinda
 
Anaandika Boniyai kutoka Account yake ya X
View attachment 3090046
View attachment 3090047

======


Ali Mohamed Kibao Ameuawa

Mjumbe wa Sekretarieti ya CHADEMA Taifa na Msaidizi wa Katibu Mkuu umekutwa hospitali ya Mkoa wa Kinondoni,Mwananyamala katika chumba cha kuhifadhia maiti mwili wake ukiwa UMEHARIBIWA VIBAYA SANA.

Mwili wa ALI MOHAMED KIBAO ulikutwa umetupwa jana alfajiri maeneo ya UNUNIO (jirani na viwanja vya NSSF) ukiwa na majereha makubwa sehemu za usoni kiasi ndugu zake walipata tabu kuutambua kirahisi.

ALI MOHAMED KIBAO alikamatwa na watu wanao dhaniwa kuwa ni askari wa Jeshi la Polisi eneo la TEGETA, mbele ya Jengo la KIBO COMPLEX baada ya gari mbili za Jeshi za Polisi za Landcruiser hardtop nyeupe kuzuia (block) basi la TASHIRIF lenye namba T 343 EES alilokuwa amepanda ALI MOHAMED KIBAO kutoka Dar es saalam kuelekea nyumbani kwao Mkoani Tanga.

Kwa bahati nzuri wakati wote wa tukio likitendeka ndani ya gari palikuwa na askari wa Jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani (Traffic) ambaye alikuwa kiti cha mbele kama abiria na alishuhudia tukio lote, anatambulika kama MACHIWA anayepatikana kwa namba 0652484802.

Namba ya simu aliyokuwa anatumia ALI MOHAMEDKIBAO ni +255 624 724 247 mpaka wakati anatekwa na kwenda kuuwawa,pia ndiyo namba ambayo mara kadhaa waliomteka walikuwa wakimpigia kuhakiki kama ni yeye.

Kwa mujibu wa wenyeji wa UNUNIO ambao ni walima mchicha, wanasema Jana asubuhi walitoa taarifa kwa Jeshi la Polisi baada ya Kuona mwili wa Mtu mzima, mweupe mwenye asili ya Kiarabu ambaye baadae Jana jioni ndugu waliutambua kuwa ni mwili ALI MOHAMED KIBAO ukiwa na majeraha.

Kabla ya umauti wake ALI MOHAMED KIBAO aliwahi kuwa afisa wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) akastaafu na kujiunga na CCM,baadae akachaguliwa kuwa Katibu Mwenezi wa CCM mkoa wa Tanga wakati wa Rais Kikwete,na baadae alijiunga CHADEMA.

Baada ya mauaji haya ya Mjumbe wa Sekretarieti ya CHADEMA na Msaidizi wa Katibu Mkuu kuwawa idadi ya Viongozi wa CHADEMA wakiotekwa inaongezeka
1. Dioniz Kipanya 2. Kombo Bwana Twaha 3. Godwin Mlay 4. Deusdedith Soka 5. Frank Mbise.


Soma Pia:

Boniface Jacob
Ex-Mayor
0712 239 595
Hadi kuzuia basi inaonekana kulikuwa na shutuma nzito ikizingatiwa bwana huyu amewahi kuwa mtumishi wa umma(Askari) kule unalishwa viapo vya kutunza Siri.

Pole yake na ndugu zake
 
Chadema tena!?ndio wanao tumia ma defender ya police!?mbona kama unaleta masihara kwenye matukio magumu!?
Uchunguzi ufanyike, dereva na abiria waitwe.

Sio kulishwa matango pori na watu wenye agenda zao.

Ni rahisi sana kufanya dhambi Tanzania kwa sababu ya ushabiki,

Sioni motive ya serikali kwenye hiko kifo.
 
Anaandika Boniyai kutoka Account yake ya X
View attachment 3090046
View attachment 3090047

======


Ali Mohamed Kibao Ameuawa

Mjumbe wa Sekretarieti ya CHADEMA Taifa na Msaidizi wa Katibu Mkuu umekutwa hospitali ya Mkoa wa Kinondoni,Mwananyamala katika chumba cha kuhifadhia maiti mwili wake ukiwa UMEHARIBIWA VIBAYA SANA.

Mwili wa ALI MOHAMED KIBAO ulikutwa umetupwa jana alfajiri maeneo ya UNUNIO (jirani na viwanja vya NSSF) ukiwa na majereha makubwa sehemu za usoni kiasi ndugu zake walipata tabu kuutambua kirahisi.

ALI MOHAMED KIBAO alikamatwa na watu wanao dhaniwa kuwa ni askari wa Jeshi la Polisi eneo la TEGETA, mbele ya Jengo la KIBO COMPLEX baada ya gari mbili za Jeshi za Polisi za Landcruiser hardtop nyeupe kuzuia (block) basi la TASHIRIF lenye namba T 343 EES alilokuwa amepanda ALI MOHAMED KIBAO kutoka Dar es saalam kuelekea nyumbani kwao Mkoani Tanga.

Kwa bahati nzuri wakati wote wa tukio likitendeka ndani ya gari palikuwa na askari wa Jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani (Traffic) ambaye alikuwa kiti cha mbele kama abiria na alishuhudia tukio lote, anatambulika kama MACHIWA anayepatikana kwa namba 0652484802.

Namba ya simu aliyokuwa anatumia ALI MOHAMEDKIBAO ni +255 624 724 247 mpaka wakati anatekwa na kwenda kuuwawa,pia ndiyo namba ambayo mara kadhaa waliomteka walikuwa wakimpigia kuhakiki kama ni yeye.

Kwa mujibu wa wenyeji wa UNUNIO ambao ni walima mchicha, wanasema Jana asubuhi walitoa taarifa kwa Jeshi la Polisi baada ya Kuona mwili wa Mtu mzima, mweupe mwenye asili ya Kiarabu ambaye baadae Jana jioni ndugu waliutambua kuwa ni mwili ALI MOHAMED KIBAO ukiwa na majeraha.

Kabla ya umauti wake ALI MOHAMED KIBAO aliwahi kuwa afisa wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) akastaafu na kujiunga na CCM,baadae akachaguliwa kuwa Katibu Mwenezi wa CCM mkoa wa Tanga wakati wa Rais Kikwete,na baadae alijiunga CHADEMA.

Baada ya mauaji haya ya Mjumbe wa Sekretarieti ya CHADEMA na Msaidizi wa Katibu Mkuu kuwawa idadi ya Viongozi wa CHADEMA wakiotekwa inaongezeka
1. Dioniz Kipanya 2. Kombo Bwana Twaha 3. Godwin Mlay 4. Deusdedith Soka 5. Frank Mbise.


Soma Pia:
Boniface Jacob
Ex-Mayor
0712 239 595
kwa masikitiko makubwa natoa pole na rambirambi zangu kwa ndugu, jamaa na marafiki wa ALI MOHAMED KIBAO ambae ametangulia mbele ya haki.

nawaombea wafiwa wote moyo wa ustahimilivu na subra katika kipindi hiki kigumu.
kifo ni fumbo, kifo hakizoeleki.

Mwenyezi Mungu aileze roho ya marehemu ALI MOHAMED KIBAO mahali anapostahili, Aimen. :CaptFailFish:
 
Mods wacheni tutoe ushauri na tahadhari ili kama wana masiko, basi na wasikie.

Wiki kama mbili zilizopita, yule dada maarufu anaeshi nchini marekani, aliandika katika mtandao wa X makala ndefu ila yenye maneno makali na matusi mazito juu ya kiongozi fulani kiasi yanayoendelea hapa nchini.

Nilikuwa nasoma na kusisimka, ila kwa tukio hili la leo, siwezi kusisimka tena hata aandike nini.

Nimalizie kwa kusema , kwa haya yanayoendelea, huyu dada sitashangaa akaja na makala nyingine mbaya zaidi na akapata uungwaji mkono mkubwa zaidi.

Washauri, mna uhakiki hii itasaidia na zaid mnaona mnamsaidia Bosi wenu au ndio mnazidi kumuharibia?

Kwa nature ya binadamu, mimi naona matukio haya yatawafanya watu wawe majasili zaidi na sasa waone hawana tena cha kupoteza.

Mtambue kuwa, kadri wengi wanavyoumizwa, ndio wengi zaidi huona na wao sasa hawana cha kupoteza na wanazidi kujawa na hasira. Hivyo, hii mbinu mnayotumia, ni sawa na kumwaga petrol kwenye moto ulionza kuwaka.

Pia, kwa haya yanayoendelea, hata mkiomba serikali ya huko aliko imrudishe nchini, inaweza kumuona kama ni mtetezi wa watu badala ya mhalifu.

Anyway, Mungu ana makusudi na kila jambo.
 
Hata kama ni CHADEMA, Serikali na Taasisi husika inabidi zichukue hatua na kukomesha huu upuuzi na upumbavu..., mmoja wetu akifa (mwananchi / nguvu kazi) lazima vyombo husika vifuatilie na kuwahoji watuhumiwa no matter their political stance....
 
Kwa nje wanaoteka na hatimae kupatikan watu wakiwa maiti inaweza kuonekana kama watu wenye nia ya kunyamazisha upinzani kwa faida ya chama tawala na raisi aliyepo madarakani.
Kwa uzoefu wangu watu hao ni majambazi ambayo yana nia mbaya na raisi.Wito raisi Samia awe makini sana kipingi hiki kuelekea uchaguzi.
Rais amebariki Utekaji na umeuita jina zuri la Drama, msihamishe magoli
 
Ukute hii Nchi inaongozwa na majitu mwitu (nephil ) maana haya majitu yana roho za kutu zilizopitiliza ,
Ccm ni cancer , haya majitu hayafai kuishi , rot in hell .
Scambags
 
Back
Top Bottom