Mpalakugenda
JF-Expert Member
- Jun 2, 2015
- 4,611
- 5,009
Kwan nini unautaka?Mwenye ushahidi wowote wa Ndugulile akikemea utekaji au mauaji ya upinzani aweke hapa.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwan nini unautaka?Mwenye ushahidi wowote wa Ndugulile akikemea utekaji au mauaji ya upinzani aweke hapa.
Sidhani kama tuko salama tena
Bado tunasubiri taarifa ya uchunguzi
Hii serikali dhalimu imeshafanya yake
Si kila kifo ni kifo, vinginevyo ukimatwa kwa kujaribu kujiua utaadhibiwa. Unaua mtu kisha unajisafisha kwa kusema kifo ni kifo huku ukijisifu kwa kutimiza lengo lako la mauaji.Anaandika Boniyai kutoka Account yake ya X
======
Ali Mohamed Kibao Ameuawa
Mjumbe wa Sekretarieti ya CHADEMA Taifa na Msaidizi wa Katibu Mkuu umekutwa hospitali ya Mkoa wa Kinondoni,Mwananyamala katika chumba cha kuhifadhia maiti mwili wake ukiwa UMEHARIBIWA VIBAYA SANA.
Mwili wa ALI MOHAMED KIBAO ulikutwa umetupwa jana alfajiri maeneo ya UNUNIO (jirani na viwanja vya NSSF) ukiwa na majereha makubwa sehemu za usoni kiasi ndugu zake walipata tabu kuutambua kirahisi.
ALI MOHAMED KIBAO alikamatwa na watu wanao dhaniwa kuwa ni askari wa Jeshi la Polisi eneo la TEGETA, mbele ya Jengo la KIBO COMPLEX baada ya gari mbili za Jeshi za Polisi za Landcruiser hardtop nyeupe kuzuia (block) basi la TASHIRIF lenye namba T 343 EES alilokuwa amepanda ALI MOHAMED KIBAO kutoka Dar es saalam kuelekea nyumbani kwao Mkoani Tanga.
Kwa bahati nzuri wakati wote wa tukio likitendeka ndani ya gari palikuwa na askari wa Jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani (Traffic) ambaye alikuwa kiti cha mbele kama abiria na alishuhudia tukio lote, anatambulika kama MACHIWA anayepatikana kwa namba 0652484802.
Namba ya simu aliyokuwa anatumia ALI MOHAMEDKIBAO ni +255 624 724 247 mpaka wakati anatekwa na kwenda kuuwawa,pia ndiyo namba ambayo mara kadhaa waliomteka walikuwa wakimpigia kuhakiki kama ni yeye.
Kwa mujibu wa wenyeji wa UNUNIO ambao ni walima mchicha, wanasema Jana asubuhi walitoa taarifa kwa Jeshi la Polisi baada ya Kuona mwili wa Mtu mzima, mweupe mwenye asili ya Kiarabu ambaye baadae Jana jioni ndugu waliutambua kuwa ni mwili ALI MOHAMED KIBAO ukiwa na majeraha.
Kabla ya umauti wake ALI MOHAMED KIBAO aliwahi kuwa afisa wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) akastaafu na kujiunga na CCM,baadae akachaguliwa kuwa Katibu Mwenezi wa CCM mkoa wa Tanga wakati wa Rais Kikwete,na baadae alijiunga CHADEMA.
Baada ya mauaji haya ya Mjumbe wa Sekretarieti ya CHADEMA na Msaidizi wa Katibu Mkuu kuwawa idadi ya Viongozi wa CHADEMA wakiotekwa inaongezeka
1. Dioniz Kipanya 2. Kombo Bwana Twaha 3. Godwin Mlay 4. Deusdedith Soka 5. Frank Mbise.
Boniface Jacob
Ex-Mayor
0712 239 595
Soma Pia:
- CHADEMA: Mzee Ally Kibao ametekwa na Vyombo vya Ulinzi na Usalama akiwa kwenye basi. Usalama wa Taifa waeleze alipo
- Polisi: Tunachunguza kubaini chanzo na watu waliohusika kumchukua Ally Kibao
- LIVE - Tanga: Yanayojiri Kwenye mazishi ya Ali Kibao Kiongozi wa Chadema
- Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana
Kwani wao na watoto wao wataishi milele??..Damu ya mtu haipotei bure. Amini hilo.
Watalipwa hapa hapa..
Kwa mungu hakuna mtu asiyejulikana
Hii serikali dhalimu imeshafanya yake
Nchi yetu sasa hivi haina tofauti na utawala wa Iddi Amini. Imekuwa ya CHINJACHINJA