Dar: Dibron Saidi ahukumiwa kunyongwa kwa kosa la kumuua Mkewe Herieth Justine kwa kisu, ni baada ya kumfumania

Unaua, unajua umefanya kosa, unajaribu kujiua, inashindikana, unakamatwa na unahukumiwa kifo, unaomba upunguziwe adhabu.
 
Ifikie hatua serikali iwachukulie hatua wanaotembea na wake za watu Ili Watu wapate pa kushtaki, Hapa aliefumaniwa keshajiona mshindi[emoji3525]
Mkuu mke wa mtu ana alama!!? Sema sheria itungwe wake za watu na waume za watu wawekwe alama usoni,na kwanini useme wanaotembea na wake za watu!!? Je wewe unamchukulia kuwa mwanamke ni kiumbe dhaifu asiye na maamuzi?

Sheria ya namna hiyo haiwezekani kwa ulimwengu wa sasa,na Mimi nikisikia hivyo nitakuwa mstari wa mbele kupinga sheria hii.

Mimi naamini mwanamke ana maamuzi yake,akikwenda nje ya ndoa achana naye kama huwezi vumilia na sio kumuua!!
 
Huwezi kuua kwa ajili ya mapenzi, lakini wewe waweza kuuliwa kwa ajili ya mapenzi.

Kabla haujafa kaika maisha haya, hauna uwezo wa kuzuia hulka za mtu mwingine kufanya jambo ovu juu yako.
Aisee, tukimbilie wapi!? Wajameni
 
Kama India mke wa mtu ana kidoti pajini na mme, na nyingine sijui wanaita sinduri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…