Dar es Salaam bila kitambaa hutoboi

Kinumbo

JF-Expert Member
Joined
Dec 8, 2019
Posts
3,039
Reaction score
5,560
Aisee! Hii hali kwa sasa katika jiji hili pedwa ni hatari sana.

Dar es Salaam kwa sasa kuna hali ya jua na joto kali sana, kuna joto ambalo ni zaidi ya joto lenyewe. Yaani bila kitambaa mkononi hutoboi salama unapo kwenda. Inabidi uwe na vitambaa viwili mikino yote miwili yaani unajifuta jasho huku na huku, maana ukifuta haichukui ata sekunde kumi inabidi ufute tena. Hatari sana kwa wale watembea kwa miguu.

Kuna muda nimetoka pale Duce kuelekea Uhasibu kupitia Kurasini umbali mfupi tu huo nimefika nimelowana mwili mzima utadhani nimemwagiwa maji. Shati limelowa kila mahala si mgongoni wala kifuani, ikanibidi nikae pembeni ili kurejesha hali niliyo kuwa nayo mwanzo.

Sio poa.
 
Sasa sisi wenye vipara ni huruma ukikamuwa uso Kwa vidole kuanzia kichwani kuja usoni unamwaga Bomba la maji hatari,Hapo Sasa ndo unapitisha kitambaa kupiga polishing.Bila hivo vitambaa vote vitalowa uwe unavikamuwa.
Wenye vipara huwa hawatoki jasho sana
 
mwanaume unatembea na kitambaa
 
Unaishije dar huna gari?
 
Nauza mataulo, vitambaa vya cotton, mitandio na vikoi.

Ila kuna watu Dar mko kama mnaishi Jehanamu. Nilipita huko mwezi Dec, aisee hilo jua sio mchezo.
Unaoga saa 1, ukijifuta tu maji. Saa 1 na nusu unaanza kusweat.
 
MMEZIDI UTAPELI
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…