Dar es salaam limegeuka jiji la makelele, Serikali imelala?

Dar es salaam limegeuka jiji la makelele, Serikali imelala?

Siku hizi ukitembea katika jiji la Dar es salaam, hali imekuwa si hali ni makelele mtindo mmoja. Hakuna utulivu kabisa.

Ukienda masokoni kila mwenye kibanda chake ana spika na rerding inayoita biashara yake non-stop kuanzia asubuhi saa mbili hadi usiku au jioni mida ya kufunga kazi.

Wakati huohuo kuna magari yanapita mabarabarani yanapiga muziki kwa sauti kubwa ajabu eti yanapromote makampuni fulanifulani. Wakati mwingine yanaweka kambi masokoni au sehemu yenye mkusanyiko mkubwa wa watu na kufungulia maspika yake ya muziki. Yaani ni makelele tupu mijini.

Kwa sasa ukiwa jijini Dar es salaam, unafanya mishe zako hakuna utulivu, huwezi kuconcentrate.

Ukiacha hilo, utakutana na bodaboda nao wamefunga mziki mzito, wanapiga singeli mtindo mmoja.

Hapo sijazungumzia Bar zinazofungulia muziki non stop katika makazi ya watu.

Noise pollution Dar ni kubwa mno imesababisha watu waumwe vichwa, uwezo wa kusikia kupungua, msongo wa mawazo, Quality of life imeshuka mno na sababu mojawapo ni Makelele mtindo mmoja.

Serikali haina budi kufanya yafuatayo.

1. Kuzuia kila mwenye biashara yake masokoni kuwa na kimtambo cha kupiga kelele kuita wateja. Hivi vispeaker vinafanya maisha ya ufanyaji shughuli masokoni kuwa headache

2. Serikali ipige marufuku kwa bodaboda kufunga speaker kwenye mabodaboda yao, kwanza haya mamiziki wanayofungulia ni hatari kwa usalama barabarani.

3. Serikali ithibiti haya matangazo ya magari ambayo huzunguuka mitaani huku wamefungulia muzik kwa staili ya Disco.

4. Miziki kwenye mabar iangaliwe upya, limit ya kiwango cha sauti (decibels) kiwekwe ili kupunguzia wananchi adha.
Sasa ukutane na daladala zile aina ya Eicher zina honi kali sana ambayo inaweza ikamuua mwenye ugonjwa wa moyo !
Wenyewe hata habari hawana !
Labda nayo hii inaingia kwenye vitu vinavyo husiana na Demokrasia 😳 !
😳😱 !
 
Noise Pollution imekuathiri tayari ... yaani unaona ukimya kama sio sawa vilee ... umezoea kelele na kupishana kwa kupigana vipushi kariakooo mkuu
Kabisa mkuu, yaani ile nafika Dom town naona kama watu wamekatazwa wasitoke maana naona magari ni machache road, watu wachache pia pako kimya sana. Maeneo kama kariakoo siyapendi kabisa maana kule no mama wa kelele dar nzima.
 
Siku hizi ukitembea katika jiji la Dar es salaam, hali imekuwa si hali ni makelele mtindo mmoja. Hakuna utulivu kabisa.

Ukienda masokoni kila mwenye kibanda chake ana spika na rerding inayoita biashara yake non-stop kuanzia asubuhi saa mbili hadi usiku au jioni mida ya kufunga kazi.

Wakati huohuo kuna magari yanapita mabarabarani yanapiga muziki kwa sauti kubwa ajabu eti yanapromote makampuni fulanifulani. Wakati mwingine yanaweka kambi masokoni au sehemu yenye mkusanyiko mkubwa wa watu na kufungulia maspika yake ya muziki. Yaani ni makelele tupu mijini.

Kwa sasa ukiwa jijini Dar es salaam, unafanya mishe zako hakuna utulivu, huwezi kuconcentrate.

Ukiacha hilo, utakutana na bodaboda nao wamefunga mziki mzito, wanapiga singeli mtindo mmoja.

Hapo sijazungumzia Bar zinazofungulia muziki non stop katika makazi ya watu.

Noise pollution Dar ni kubwa mno imesababisha watu waumwe vichwa, uwezo wa kusikia kupungua, msongo wa mawazo, Quality of life imeshuka mno na sababu mojawapo ni Makelele mtindo mmoja.

Serikali haina budi kufanya yafuatayo.

1. Kuzuia kila mwenye biashara yake masokoni kuwa na kimtambo cha kupiga kelele kuita wateja. Hivi vispeaker vinafanya maisha ya ufanyaji shughuli masokoni kuwa headache

2. Serikali ipige marufuku kwa bodaboda kufunga speaker kwenye mabodaboda yao, kwanza haya mamiziki wanayofungulia ni hatari kwa usalama barabarani.

3. Serikali ithibiti haya matangazo ya magari ambayo huzunguuka mitaani huku wamefungulia muzik kwa staili ya Disco.

4. Miziki kwenye mabar iangaliwe upya, limit ya kiwango cha sauti (decibels) kiwekwe ili kupunguzia wananchi adha.
Kuishi kwenye kelele ni mojawapo ya indicators za umasikini na ujima!! Kelele nyumbani, kelele barabarani, kelele maofisini, kelele nyumba za ibada.., ili mradi kelele kila mahali!!
 
Kabisa mkuu, yaani ile nafika Dom town naona kama watu wamekatazwa wasitoke maana naona magari ni machache road, watu wachache pia pako kimya sana. Maeneo kama kariakoo siyapendi kabisa maana kule no mama wa kelele dar nzima.
Sogea karume pale ukikaa pale masaa 3 njaa haijakuuma kwa yale makelele niite mimi lofa ila mimi nimependa ile ndio inavuta wateja watu hawapendi biashara za kupigana yaan shati hilo hilo wewe unauziwa 15,000 kuna mwenzio anauziwa 2000 kwa hio ikitangazwa 2000 hio inavuta wateja kwamba pale shati zote 2000 zamani walikua hawatangazi kwa hio ukifika pale unauliza bei na haijaandikwa kinachofuata ni kupigwa elfu 2 2 shati elfu 2 2 elfu 2 2 shati elfu 2 2
 
Kabisa mkuu, yaani ile nafika Dom town naona kama watu wamekatazwa wasitoke maana naona magari ni machache road, watu wachache pia pako kimya sana. Maeneo kama kariakoo siyapendi kabisa maana kule no mama wa kelele dar nzima.
For sure Dom ni mji wenye utulivu sana.
Hata machinga kule airport kuko kimya
Hata watu Wana ka utulivu fulani sio ka kariakooo mkuu! Kila mtu ni kama kavurugwa
 
Sogea karume pale ukikaa pale masaa 3 njaa haijakuuma kwa yale makelele niite mimi lofa ila mimi nimependa ile ndio inavuta wateja watu hawapendi biashara za kupigana yaan shati hilo hilo wewe unauziwa 15,000 kuna mwenzio anauziwa 2000 kwa hio ikitangazwa 2000 hio inavuta wateja kwamba pale shati zote 2000 zamani walikua hawatangazi kwa hio ukifika pale unauliza bei na haijaandikwa kinachofuata ni kupigwa elfu 2 2 shati elfu 2 2 elfu 2 2 shati elfu 2 2
Sidhani kama ishu ya bei ni sababu, watanzania tunapenda tu makelele. Kwa mfano kwenye daladala kuna konda anaita abiria kwa kutaja bei na sehemu gari inaenda halafu kuna mpiga debe naye anafanya kitu kilekile. Huwa najiuliza haya yote sababu ni nini...
 
Aisee hali makelele inatisha,yaani ukienda Kariakoo lazima urudi kichwa kinauma!!Kwa ujumla Dar kwa sasa ni jiji la kelele
 
Back
Top Bottom