Dar es Salaam ni mji uliojaa wazururaji

Dar es Salaam ni mji uliojaa wazururaji

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Najua hii mada itawashtua wengi na wengine watapanda munkari ila embu tuelewane kwanza kabla haujajibu kwa jazba.

Kwa tathmini yangu ya muda mrefu ni kuwa mji wa Dar es Salaam umejaa watu wasio na kazi maalumu. Wale wenye ajira rasmi serikalini au katika sekta binafsi ni wachache sana, wengi ni wabangaizaji na wazururaji walio katika mwamvuli wa kujiajiri.

Ukitaka kujua hilo ni kitendo cha asilimia kubwa ya watu kupotea mitaani siku mbili zilizopita kisa wameambiwa barabara zitafungwa. Yaani unaambiwa usiende kutafuta ugali wako halafu hata manung'uniko hamna, watu wametii amri bila shuruti. Hii inakwambia wengi hawakuwa na mitkasi ya maana wakaona fresh tu.

Nadhani kauli mbiu ya mji wa Dar es Salaam inapaswa kuwa "Mtembea bure siyo sawa na mkaa bure".
 
Yaani ulitaka wakalalamike au kuinga kuzuiwa kwenda mjini? Hivi nani yuko tayari kupigwa kirungu au kulazwa mahabusu kisa kukiuka amri ya mkubwa?
 
😄😄🤣 huu ni ukweli usiopingika ila tarajia matusi kutoka kwa wazururaji subir wanakuja
 
Cc wamikoani tufanye kazi km tumeamua kufanya kazi,wa dar nao waaache wazurure km wameamua kuzurura mkuu wangu..

Kilaa mbuzi ula Kwa urefu wa kambaa yake
 
Mji uliojaa watafuta kazi kutokea Tanzania nzima si lazima wazurure hovyo.
.nchi ambayo mpaka miaka zaidi ya 60 ya uhuru haina mfumo wa wanaomaliza vyuo na shule waanzie wapi kujiandikishqnkihusi kazi.

Waajiri nao hawajui wakitaka wafanya kazi waende wapi.

Ukweli ni kuwa nchi yetu imejaa ujinga wa hali ya juu, hao walioaminiwa kuwa ni wasomi, hawajaelimika.
 
Mji uliojaa watafuta kazi kutokea Tanzania nzima si lazima wazurure hovyo.
.nchi ambayo mpaka miaka zaidi ya 60 ya uhuru haina mfumo wa wanaomaliza vyuo na shule waanzie wapi kujiandikishqnkihusi kazi.

Waajiri nao hawajui wakitaka wafanya kazi waende wapi.

Ukweli ni kuwa nchi yetu imejaa ujinga wa hali ya juu, hao walioaminiwa kuwa ni wasomi, hawajaelimika.
Elimu yetu inazalisha maintellectual n sio maintelligence ili ukuze uchumi unahitaji kuwa na maintelligence kuwa intelligence hakuhitaji ukae darasani kupoteza mda ukasome masters uje uendeshe bodaboda
 
Dar Kila mtu ana stress unaweza ukamsalimia mtu unashangaa anakushushia tu matusi
 
Graduates wengi wakimaliza vyuo wanakuja jiji la Dar.

Wahitimu wa six wengi wanakuja Dar

Waliomaliza form four wengi wanakuja Dar.

Walioishia darasa la saba wanakuja Dar.

Hoja ya kuzurura tunaikubali as wengi ni hustlers, nawe huko uliko fanya kazi usizurure.
 
Mji uliojaa watafuta kazi kutokea Tanzania nzima si lazima wazurure hovyo.
.nchi ambayo mpaka miaka zaidi ya 60 ya uhuru haina mfumo wa wanaomaliza vyuo na shule waanzie wapi kujiandikishqnkihusi kazi.

Waajiri nao hawajui wakitaka wafanya kazi waende wapi.

Ukweli ni kuwa nchi yetu imejaa ujinga wa hali ya juu, hao walioaminiwa kuwa ni wasomi, hawajaelimika.
Leo faizfoxy umeongea Point. Kumbe ukitulia vizuri akili zinafanya KAZI.
 
Dar watu wengi hawana maboss, ndo maana hata greda likiwa linakwangua barabara wanajaa kushangaa!
 
Back
Top Bottom