TRA Tanzania
Senior Member
- Jul 16, 2022
- 128
- 370
asante sana TRA kwa muongozo huu wengine tulikuwa hatujui vizuri hizi taratibu.Ni muhimu sana kubadili umiliki maana dunia imeharibika kwa sasa unaweza uza gari likaenda tumika kwenye wizi au kuvusha madawa mwisho wa siku ukajikuta upo kwenye matatizo au limegonga na kuua halafu dereva kasepa wakikagua mmiliki imekula kwako mpaka uje kuthibitisha. pia naona hata ukinunua likiibiwa au ungua changamoto bima au polisi kuwa wewe ndiye mmiliki maana inakuwa halipo kwenye jina langu. Niwaombe sana TRA mzidi kutupa elimu zaidi na kwenye mambo mengi tu hata ukifungua kampuni nini tufanye ili tuepuke adhabu na hatimaye tulipe kodi tunayostahili. Mwisho niwapongeze kwa makusanyo ya mwezi Desemba na kuwa karibu na sisi wafanyabiashara naona mmebadilika sana endeleeni na jitihada hizi za kuwa karibu na walipa kodi.View attachment 3200864
Mambo muhimu ya kuzingatia wakati wa kubadilisha umiliki wa chombo cha moto
1: Kadi ya usajili wa chombo cha moto iliyosainiwa na muuzaji na mnunuzi
2: Mkataba wa kisheria wa mauziano na risiti ya efd toka kwa mwanasheria aliyepitia mkataba huo
3:TIN ya mnunuzi
4: Kiapo cha umiliki
5: Picha ndogo 2 za mnunuzi na muuzaji
6: Barua ya maombi ya kubadili umiliki
7: Kopi ya kitambulisho cha muuzaji
Inawezekana huna Hari Ila kwa FAIDA ya walio na magari wanaweza kufanya chochote....kufungwa au kupigwa faini..Usipobadili mnatufanya nini?
yote umesema kwel ila huu ndio mzizi wa fitna ndio maana nikauliza hivyo...SIla.kikuba nachokiona wanataka kuanzisha Kodi nyingine Sasa wanawajaza watu kwenye mfumo wawanyonge vizuri hasa magari ya biashara
Sawa,View attachment 3200864
Mambo muhimu ya kuzingatia wakati wa kubadilisha umiliki wa chombo cha moto
1: Kadi ya usajili wa chombo cha moto iliyosainiwa na muuzaji na mnunuzi
2: Mkataba wa kisheria wa mauziano na risiti ya efd toka kwa mwanasheria aliyepitia mkataba huo
3:TIN ya mnunuzi
4: Kiapo cha umiliki
5: Picha ndogo 2 za mnunuzi na muuzaji
6: Barua ya maombi ya kubadili umiliki
7: Kopi ya kitambulisho cha muuzaji
Utitiri wa Kodi kwa mlipa Kodi yule yule ,ni kukamuana mpaka tone la mwishoInawezekana huna Hari Ila kwa FAIDA ya walio na magari wanaweza kufanya chochote....kufungwa au kupigwa faini..
1.kuna Sheria kwenye by laws za traffic act zinazotaka dereva kukabidhiwa kwa mwandishi gari kutoka kwa mmiliki...IPO na hawaifuatilii nadhani bado haijabadilishwa..
2.nilitaka kuvuka boda na gari yangu nilikuwa sijabadilisha umiliki...nikatakiwa niwe na barua ikionysha nimekabidhiwa Hari na niruhusiwe kuvuka..usumbufu NI mwingi
3.wanaweza kukustaki kukwepesha mapato ya serikali kwa kutofanya transfer....
4.aliyekopa anaweza kuwa anadaiwa na mamlaka ikaamua kutaifisha malinzake...utalia na mama yako...
Ila.kikuba nachokiona wanataka kuanzisha Kodi nyingine Sasa wanawajaza watu kwenye mfumo wawanyonge vizuri hasa magari ya biashara
Wanataka wappige hela hapaVigezo kibao,niliuza gari kiholela mwaka 2010,nadhani lishakatwa screpa hadi leo hii
Ni wapuuz hawa dawa yao ban ya maishaHawana msaada kabisa maswali hawajibu
KAMA TUMEPEANA BURE JE?2: Mkataba wa kisheria wa mauziano na risiti ya efd toka kwa mwanasheria aliyepitia mkataba huo
Wao wanawaza kuuziana tu. What if nimempa mtu gari FREESawa,
What if tuliiziana kishikaji tu na alieniuzia katangulia mbele ya haki??
HahahahaHizi gari zetu zimeshapita kwa wamiliki zaidi ya watano kwa kupeana kadi TU ni changamoto!!
Kuna noah ilishanitesa sana 😂😂