Dar: Mahakama ya Kisutu yajiweka kando kutoa uamuzi kesi ya Dkt. Slaa, Hakimu adai anafungwa mikono na Rufaa ya Jamhuri

Dar: Mahakama ya Kisutu yajiweka kando kutoa uamuzi kesi ya Dkt. Slaa, Hakimu adai anafungwa mikono na Rufaa ya Jamhuri

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Uamuzi uliotarajiwa kutolewa leo Januari 31, 2025 na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwenye shtaka linalomkabili Dkt. Wilbrod Slaa ikiwa ni baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kuagiza shauri la Dkt. Slaa lirejeshwe Kisutu kwaajili ya kushughulikiwa kwa dhamana yake umeshindwa kutolewa.

Hoja iliyoelezwa na Hakimu Mkazi Mkuu, Beda Nyaki kukwamisha uamuzi huo ni kuwa, Jamhuri imekata rufaa kwenye Mahakama ya Rufaa, hivyo wanafungwa mikono katika kutoa uamuzi mpaka majibu ya rufaa hiyo yatakapotolewa.

Kufuatia uamuzi huo baada ya mabishano ya kisheria, Wakili upande wa mshtakiwa, Peter Madeleka ameeleza kuwa yeye na timu ya mawakili wengine wa utetezi hawajaridhishwa na maamuzi hayo kwani uwepo wa rufaa bado hauzuii haki zingine za msingi za mshtakiwa kama dhamana.

Soma Pia: Mahakama Kuu yaagiza dhamana ya Dkt. Slaa ishughulikiwe haraka

Itakumbukwa leo Januari 31, 2025 ilitarajiwa kutolewa uamuzi wa pingamizi la uhalali wa hati ya mashtaka, ambapo kwa mujibu wa mwendo wa kesi hiyo endapo ingefanyika hivyo ndipo mahakama ingeweza kiendelea na shauri juu ya dhamana ya Dkt. Slaa.

Kwa sasa mtuhumiwa huyo ambaye leo hakuletwa mahakamani kutokana na kilichodaiwa kwamba kulikuwepo na changamoto ya gari iliyotakiwa kuwapeleka washtakiwa Mahakamani, hivyo anaendelea kukaa rumande.
 
Uamuzi uliotarajiwa kutolewa leo Januari 31, 2025 na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwenye shtaka linalomkabili Dkt. Wilbrod Slaa ikiwa ni baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kuagiza shauri la Dkt. Slaa lirejeshwe Kisutu kwaajili ya kushughulikiwa kwa dhamana yake umeshindwa kutolewa.

Hoja iliyoelezwa na Hakimu Mkazi Mkuu, Beda Nyaki kukwamisha uamuzi huo ni kuwa, Jamhuri imekata rufaa kwenye Mahakama ya Rufaa, hivyo wanafungwa mikono katika kutoa uamuzi mpaka majibu ya rufaa hiyo yatakapotolewa.

Kufuatia uamuzi huo baada ya mabishano ya kisheria, Wakili upande wa mshtakiwa, Peter Madeleka ameeleza kuwa yeye na timu ya mawakili wengine wa utetezi hawajaridhishwa na maamuzi hayo kwani uwepo wa rufaa bado hauzuii haki zingine za msingi za mshtakiwa kama dhamana.

Itakumbukwa leo Januari 31, 2025 ilitarajiwa kutolewa uamuzi wa pingamizi la uhalali wa hati ya mashtaka, ambapo kwa mujibu wa mwendo wa kesi hiyo endapo ingefanyika hivyo ndipo mahakama ingeweza kiendelea na shauri juu ya dhamana ya Dkt. Slaa.

Kwa sasa mtuhumiwa huyo ambaye leo hakuletwa mahakamani kutokana na kilichodaiwa kwamba kulikuwepo na changamoto ya gari iliyotakiwa kuwapeleka washtakiwa Mahakamani, hivyo anaendelea kukaa rumande.


🤦🏾‍♂️ rufaa inakuja baada ya maamuzi. Sasa rufaa ya nini wakati maamuzi hawajatoa😂
 
Uamuzi uliotarajiwa kutolewa leo Januari 31, 2025 na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwenye shtaka linalomkabili Dkt. Wilbrod Slaa ikiwa ni baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kuagiza shauri la Dkt. Slaa lirejeshwe Kisutu kwaajili ya kushughulikiwa kwa dhamana yake umeshindwa kutolewa.

Hoja iliyoelezwa na Hakimu Mkazi Mkuu, Beda Nyaki kukwamisha uamuzi huo ni kuwa, Jamhuri imekata rufaa kwenye Mahakama ya Rufaa, hivyo wanafungwa mikono katika kutoa uamuzi mpaka majibu ya rufaa hiyo yatakapotolewa.

Kufuatia uamuzi huo baada ya mabishano ya kisheria, Wakili upande wa mshtakiwa, Peter Madeleka ameeleza kuwa yeye na timu ya mawakili wengine wa utetezi hawajaridhishwa na maamuzi hayo kwani uwepo wa rufaa bado hauzuii haki zingine za msingi za mshtakiwa kama dhamana.

Itakumbukwa leo Januari 31, 2025 ilitarajiwa kutolewa uamuzi wa pingamizi la uhalali wa hati ya mashtaka, ambapo kwa mujibu wa mwendo wa kesi hiyo endapo ingefanyika hivyo ndipo mahakama ingeweza kiendelea na shauri juu ya dhamana ya Dkt. Slaa.

Kwa sasa mtuhumiwa huyo ambaye leo hakuletwa mahakamani kutokana na kilichodaiwa kwamba kulikuwepo na changamoto ya gari iliyotakiwa kuwapeleka washtakiwa Mahakamani, hivyo anaendelea kukaa rumande.
Slaa aache mdomo mchafu.Ajitambue yeye ni Babu sasa
 
Wanao fanya haya ipo siku sio mda na wao watakua jela, hii inadhihilisha Jamhuri lengo lao halikua zuri na sio zuri juu ya mzee uyu ,

Yalikuepo Magenge ya ajabu Zambia ya kutesa ,kukandamiza haki za watu ,leo kwisha .

So hata hapa kwetu ni swala la mda tu asema Bwana
 
Back
Top Bottom