JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,780
- 6,607
Uamuzi uliotarajiwa kutolewa leo Januari 31, 2025 na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwenye shtaka linalomkabili Dkt. Wilbrod Slaa ikiwa ni baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kuagiza shauri la Dkt. Slaa lirejeshwe Kisutu kwaajili ya kushughulikiwa kwa dhamana yake umeshindwa kutolewa.
Hoja iliyoelezwa na Hakimu Mkazi Mkuu, Beda Nyaki kukwamisha uamuzi huo ni kuwa, Jamhuri imekata rufaa kwenye Mahakama ya Rufaa, hivyo wanafungwa mikono katika kutoa uamuzi mpaka majibu ya rufaa hiyo yatakapotolewa.
Kufuatia uamuzi huo baada ya mabishano ya kisheria, Wakili upande wa mshtakiwa, Peter Madeleka ameeleza kuwa yeye na timu ya mawakili wengine wa utetezi hawajaridhishwa na maamuzi hayo kwani uwepo wa rufaa bado hauzuii haki zingine za msingi za mshtakiwa kama dhamana.
Soma Pia: Mahakama Kuu yaagiza dhamana ya Dkt. Slaa ishughulikiwe haraka
Itakumbukwa leo Januari 31, 2025 ilitarajiwa kutolewa uamuzi wa pingamizi la uhalali wa hati ya mashtaka, ambapo kwa mujibu wa mwendo wa kesi hiyo endapo ingefanyika hivyo ndipo mahakama ingeweza kiendelea na shauri juu ya dhamana ya Dkt. Slaa.
Kwa sasa mtuhumiwa huyo ambaye leo hakuletwa mahakamani kutokana na kilichodaiwa kwamba kulikuwepo na changamoto ya gari iliyotakiwa kuwapeleka washtakiwa Mahakamani, hivyo anaendelea kukaa rumande.
Hoja iliyoelezwa na Hakimu Mkazi Mkuu, Beda Nyaki kukwamisha uamuzi huo ni kuwa, Jamhuri imekata rufaa kwenye Mahakama ya Rufaa, hivyo wanafungwa mikono katika kutoa uamuzi mpaka majibu ya rufaa hiyo yatakapotolewa.
Kufuatia uamuzi huo baada ya mabishano ya kisheria, Wakili upande wa mshtakiwa, Peter Madeleka ameeleza kuwa yeye na timu ya mawakili wengine wa utetezi hawajaridhishwa na maamuzi hayo kwani uwepo wa rufaa bado hauzuii haki zingine za msingi za mshtakiwa kama dhamana.
Soma Pia: Mahakama Kuu yaagiza dhamana ya Dkt. Slaa ishughulikiwe haraka
Itakumbukwa leo Januari 31, 2025 ilitarajiwa kutolewa uamuzi wa pingamizi la uhalali wa hati ya mashtaka, ambapo kwa mujibu wa mwendo wa kesi hiyo endapo ingefanyika hivyo ndipo mahakama ingeweza kiendelea na shauri juu ya dhamana ya Dkt. Slaa.
Kwa sasa mtuhumiwa huyo ambaye leo hakuletwa mahakamani kutokana na kilichodaiwa kwamba kulikuwepo na changamoto ya gari iliyotakiwa kuwapeleka washtakiwa Mahakamani, hivyo anaendelea kukaa rumande.