Ng'wale
JF-Expert Member
- Nov 24, 2011
- 4,690
- 3,399
Lugha alivyoiweka Makonda ndiyo imekua tatizo na hata yeye nadhani hajajua hilo au hata kama amejua atakua ameamua kutorekebisha namna alivyoongea. Kiswahili alitakiwa akiweke kwamba "Tuko hapa kuhakikisha tunawapa majibu sahihi au taarifa sahihi na taarifa sahihi ZITAKUA ni Mo amepatikana na watekaji wako mikononi mwa vyombo vya dola" Yeye ameongea ktk namna ambayo inakutaka kua makini sana kujua kwamba anaongelea kitu ambacho KITAFANYIKA. Ameongea ktk hali ambayo usipotulia vizuri unaweza kujua kwamba anaongelea jambo ambalo limeshafanyika.Nimemsikiliza vizuri Makonda ........ amesema kuwa "Majibu sahihi ni kuwa Mo amepatikana na wahalifu wametiwa mikononi mwa vyombo vyetu vya dola...."
Kama siyo kweli basi AIBU KUBWA ............ Kiongozi Mkubwa kama yeye hakutakiwa kutoa habari zisizo na uhakika!!