Dar: Mfanyabiashara Mohamed Dewji(Mo Dewji) atekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay

Habari za kuhuzunisha ni kuwa huyu mtu kupatikana imeshakuwa jambo gumu. Muda aliotekwa hadi kuanza kwa msako ni hayapungui masaa matatu, ambapo muda huo watekaji walishaweza kumfikisha kwenye mapori ya mkoa wa Pwani au Morogoro

Watekaji kumuachilia kwa sababu maneno na vitisho kupitia vyombo vya habari sidhani kama itasaidia. Usalama wa taifa wanaweza kutoa msaada na ushauri kutokana na uzoefu na weledi wao maana nadhani Hideouts zote zipo chini ya Surveillance yao. Kwa kumficha mtaani lazima watamuhamisha hamisha haiwezekani wakamuweka sehemu moja sababu waTanzania hatufichi siri za maovu kama utekaji au majambazi.

Usalama wa taifa ndio wenye msaada mkubwa kwenye hili
 
Najiuliza swali hili baada ya kuona vyombo vikubwa vya habari duniani vikiwemo BBC, CNN, Al jazira, Xiua na Reuters vikiripoti na kulifuatilia kwa karibu tukio hili la utekaji lililotokea nchini mwetu!
 
Hivi hawa walizni wa Hoteli huwa wanafanya kazi gani?
mapambo tu na vibunduki vyao
 
Namhurumia huyu mwanaspoti wetu mahili na Nimejiuliza mengi jinsi gani watu Hawa wabaya wanavyo m treat mtu huyu very innocent
Sijui wanampa maji, chakula kweli?
Huko mlipo watekaji tunajua mnafuatilia mitandao chonde msimhukumu au kumdhuru mtu huyo asiye na hatia kwa tamaa ya pesa, Wekeni ubinadamu mbele
Huyo mheshimiwa Ana family yake na bado wanamhitaji na anasapoti ajira za mamilioni ya watu
Mpeni mahitaji muhimu kwa Binadamu maji, chakula.
 
Nitajie nchi moja tu, yoyote ile ambayo tajiri wake mkubwa kuliko wote aliwahi kutekwa na saa 24 kupita bila vyombo vya dola kuwa na clue!

Kwamba, eti "haijalishi huyo mtu ni maarufu au kama mimi" hiyo ni kujaribu ku-justify uozo uliopo kwenye mfumo wetu wa ulinzi na usalama! Endelea kujidanganya kwamba akina eti sie tupo sawa tu na akina Reginald Mengi na kwamba, utekwaji wa yeyote miongoni mwetu hiyo ni ishara mbaya! Ni kweli, ni ishara mbaya lakini anapotekwa mtu kama Mo Dewji, hiyo sio tu ni ishara mbata bali ni ishara mbaya zaidi na zaidi!

Sie wengine miaka kadhaa iliyopita tulishuhudia Mzee Reginald Mengi akipewa ulinzi wa polisi nyumbani kwake Oysterbay baada ya kutishiwa kuuawa! Kama unaamini wewe na Mzee Mengi ni sawa, basi nenda kwenye kituo cha karibu ukaripoti kwamba unatishiwa kifo na kisha wathibitishe kwamba kweli unatishiwa kifo halafu uone kama unapewa askari polisi wa kuja kukulinda hapo unapoishi!!!

Mtu kama mimi, nitaenda viwanja gani kama sio Tandale, Mwananyamala, Manzese, Temeke n.k! Huko haitashangaza nikitekwa kwa sababu mfumo wetu wa ulinzi haujafika kisawasawa hadi Uswahilini!!! Lakini inapotokea mtu anatekwa maeneo kama ya Colleseum na kupita 24 hours bila vyombo vya dola kuwa na clue, hapo akina sie hatutaacha kujiuliza ikiwa maeneo kama yale na mtu kama yule anaweza kutekwa na watekaji kutokomea kusikojulikana! Maeneo ambayo angalau yana mifumo mizuri ya mitaa ambayo ingewezesha kuwa na street cams; vipi akina sie tunaoishi Kwa Mtogole! Huku kwetu watu si wanaweza kuingia hadi na vifaru na wasionekane!!

Ikiwa maeneo kama yake hayana hata Patrol inayoweza ku-respond kwa haraka anapotekwa mtu kama Mo Dewji, vipi huku kwetu?Ikiwa Richest Person anaweza kutekwa na polisi wasiwe na clue hata baada ya saa 24 kupita huku tukifahamu wamewekeza nguvu zao zote katika kufanya msako! Vipi ninapotekwa mtu kama mimi ambae polisi haitaweza kutoa japo askari mmoja kutafuta nipo wapi!!!

Kwa wale wanaoamini katika siku ya huku, mimi na Mo Dewji ni sawa lakini ni sawa mbele ya mwenye kiti cha enzi lakini hatuna usawa wowote mbele ya viti vya akina Magu!!

No wonder tunapotekwa akina sie wala hakuna anayejishughulisha! Endelea kuhangaika ku-justify ujinga!
 
Najiuliza swali hili baada ya kuona vyombo vikubwa vya habari duniani vikiwemo BBC, CNN, Al jazira, Xiua na Reuters vikiripoti na kulifuatilia kwa karibu tukio hili la utekaji lililotokea nchini mwetu!
Kuna watu sijui ni ugumu wa maisha!!? Yaani we unamuona Mo ni sawa na wewe? Hili kweli linashangaza?? Ulitegemea Mo atekwe alafu habari iishie hapo kwenu Missenyi?

Mo ni international figure. Sasa ajabu iko wapi kuona BBC, CNN, n.k kwao inakuwa habari kubwa??

Inaelekea hata Diamond akipotea ghafla utakuja kuuliza maswali yako haya haya ya kilevi
 
Bila CIA, MOSAD, nk hatufui dafu hapa, jamaa atapatikana amesha kula kichapo heavy hajitambui

Halafu naona raia wanaanza kuandaliwa kisaikolojia, kuwa hao watekaji watataka kiasi cha hela ili wamwachie huru hapa kuna wahuni watapiga hela.
 
Mbona umepanic!
 
Hujanishinda mimi.nimeamua ku logout kabisa.
Wacheni Ushamba, Katika maisha hakuna usawa wapo Watanzania wanaishi maisha daraja la kwanza hapa Bongo. Ndio nikasema ...Endapo MO aliwekewa Kifaa hicho (RFID chip) anaweza kutafutwa kirahisi.
Nikasema ANGALIZO Mimi namwamini Mungu na science ( wapo watu tafsiri potofu chapa ya shetani 666)
 
Najiuliza swali hili baada ya kuona vyombo vikubwa vya habari duniani vikiwemo BBC, CNN, Al jazira, Xiua na Reuters vikiripoti na kulifuatilia kwa karibu tukio hili la utekaji lililotokea nchini mwetu!
hivi kweli umekosa jibu la swali hilo hadi unaleta bandiko hapa?
 
Watu wa Kolomije wanadhani Bashite ni maarufu kuliko Mo...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…