DAR: Mgonjwa atibiwa tatizo kwenye ubongo bila kufungua fuvu

DAR: Mgonjwa atibiwa tatizo kwenye ubongo bila kufungua fuvu

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
2bd83fdc-b17f-437a-854e-0388909c4de5.jpg
Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) kwa kushirikiana na Hospitali ya Ramaiah India imeendesha kambi maalum ya uchunguzi na tiba ya mishipa ya damu kwenye ubongo bila kufungua fuvu kwa mbinu za kisasa.

Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Dkt. Respicious Boniface amesema zaidi ya wagonjwa 160 wameshapatiwa huduma katika maabara hiyo toka ilipoanza kazi mwaka 2021. Maabara hiyo imejengwa na Serikali kwa zaidi ya Tsh Bilioni 7.9.

“Hivi karibuni tulianzisha ushirikiano na wenzetu hawa Hospitali ya Ramaiah India ili tushirikane katika kuboresha huduma zetu za uchunguzi na tiba ya Ubongo hapa nchini, sasa ndio wamekuja na wamewahudumia wagonjwa pamoja na kutoa mafunzo kwa wataalamu wetu ikiwa ni pamoja na kuwapa mbinu za kisasa za upasuaji,” alisema Dkt. Boniface.
0f467f25-ef8d-4f50-956e-27524fefa978.jpg
Dkt. Boniface amesema hii ni sehemu ya mkakati wa MOI wa kuhakikisha huduma zote za kibingwa za ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu zinapatikana hapa nchini ili kuiondolea mzigo mkubwa Serikali wa kupeleka wagonjwa nje ya nchi kutafuta matibabu ambayo hayapatikani hapa nchini.

Kwa upande wake daktari bingwa wa upasuaji wa ubongo kutoka Hospitali ya Ramaia India, Dkt. Sunil Valentine Furtado amesema ujio wao umetokana na majadiliano ambayo yalifanyika baina yao na uongozi wa MOI ambapo ushirikiano baina ya Taasisi hizi unalenga kuboresha huduma kwa wagonjwa, kubadilishana uzoefu na mafunzo.


Source: Matukio na Maisha
 
Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) kwa kushirikiana na Hospitali ya Ramaiah India imeendesha kambi maalum ya uchunguzi na tiba ya mishipa ya damu kwenye ubongo bila kufungua fuvu kwa mbinu za kisasa.

Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Dkt. Respicious Boniface amesema zaidi ya wagonjwa 160 wameshapatiwa huduma katika maabara hiyo toka ilipoanza kazi mwaka 2021. Maabara hiyo imejengwa na Serikali kwa zaidi ya Tsh Bilioni 7.9.

“Hivi karibuni tulianzisha ushirikiano na wenzetu hawa Hospitali ya Ramaiah India ili tushirikane katika kuboresha huduma zetu za uchunguzi na tiba ya Ubongo hapa nchini, sasa ndio wamekuja na wamewahudumia wagonjwa pamoja na kutoa mafunzo kwa wataalamu wetu ikiwa ni pamoja na kuwapa mbinu za kisasa za upasuaji,” alisema Dkt. Boniface.
Dkt. Boniface amesema hii ni sehemu ya mkakati wa MOI wa kuhakikisha huduma zote za kibingwa za ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu zinapatikana hapa nchini ili kuiondolea mzigo mkubwa Serikali wa kupeleka wagonjwa nje ya nchi kutafuta matibabu ambayo hayapatikani hapa nchini.

Kwa upande wake daktari bingwa wa upasuaji wa ubongo kutoka Hospitali ya Ramaia India, Dkt. Sunil Valentine Furtado amesema ujio wao umetokana na majadiliano ambayo yalifanyika baina yao na uongozi wa MOI ambapo ushirikiano baina ya Taasisi hizi unalenga kuboresha huduma kwa wagonjwa, kubadilishana uzoefu na mafunzo.


Source: Matukio na Maisha
😍😍
 
Yaani kitu hulijui,Cha kisayansi lakini bado unaotea otea
Ningekua sijui nisingesema, mimi nisema ninachokijua, kwamba ni mionzi tu, hakuna namna nyingine. Halafu kuwa na reservation kwenye maneno yako, maana unaonekana taahira tu.

9E856869-393B-4855-9399-544E7C0C1C91.jpeg
 
'itakua'ni neno linaloakisi kukosa uhakika,Kama ulikua ni mionzi,ungesema mionzi
Itakuwa ni mionzi inamaanisha ninachokifahamu mimi ni hicho na sio kwamba naotea, ila pia inatoa room ya kuwepo possibility nyingine, maana technology inakuwa kila siku.
 
tumuombe Mungu uzima.
Humo ndani sio pazuri hata kupaangalia kwenye picha
 
Back
Top Bottom