Dar: Raia wa China wageuka machinga, Wananchi washitushwa

Dar: Raia wa China wageuka machinga, Wananchi washitushwa

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687
Wawekezaji kutoka China wakiendelea na shughuli za uwekezaji wa biashara zao Jijini Dar.

Pia soma Samia: Msiruhusu Wageni Kufanya Biashara za Wenyeji

====

UNAPOTEMBEA katika Mitaa ya Agrey, Nyamwezi, Livingstone, Swahili na Congo jijini Dar es Salaam, ni kawaida kuona raia wa kigeni wakifanya kazi ambazo zinapaswa kufanywa na Watanzania na wao kufanya kazi za kitaalamu na uwekezaji.

Hawa wageni wanapaswa kuwapo katika kazi za kitaalam na uwekezaji mkubwa, huku wakitakiwa kutekeleza majukumu yao katika kazi za kitaaluma.

Raia hao wenye asili ya China hutumia mbinu mbalimbali zikiwamo kuwa na maduka ambayo huonyesha wanauza bidhaa kwa jumla, lakini hugeuka kuwa wauzaji wa rejareja na wakati mwingine huchuuza bidhaa kutoka eneo moja hadi jingine la jiji la Dar Es Salaam.

Hivi karibuni, palizuka mgogoro baina ya raia wa China na Mtanzania wakigombea eneo la kupanga bidhaa zao.

Picha jongefu za tukio hilo zilisambaa kwa kasi kubwa kwenye mitaandao ya kijamii hatua iliyomshtua Rais Samia Suluhu Hassan, ambaye aliagiza mamlaka za serikali kuhakikisha raia wa kigeni wanafanyakazi kwa mujibu wa vibali vyao, huku akitaka kazi za Watanzania kulindwa.

Aidha, alitoa maelekezo kwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Seleman Jafo, “Nimeona video Mchina akipigana na mwenyeji tena mwanamke, mchina mwanaume na mwenyeji mwanamke, ngumu za kweli kweli, nilipouliza kulikoni nikaambiwa yule Mchina naye anauza mitumba, biashara ya wenyeji, tena wenyeji vijana wetu. Hilo nalo kalitizame”.

“Kama biashara haifai kufanywa na watu wa nje wasifanye, sababu ni nini mpaka wanapewa leseni ya kufanyabiashara za aina ile, na kama hawapewi leseni kwanini wanafanyabiashara za aina ile.”

Screenshot 2024-11-03 at 19.23.03.png
Screenshot 2024-11-03 at 19.23.15.png
 
sioni shida yeyote hapo, kwani ninyi mnaogopa nini? mnaogopa ushindani? ukienda china leo hii ukaseme ufanye kazi hizi za hali ya chini wakakuzuia utajisikiaje?

Sisi wabongo tufanye biashara tushindane nao, kwani tunawaogopa? na mbona bidhaa zao ni bei poa kuliko za kwenu au mnataka muendelee na syndicate zenu kuuzia watu vitu bei ya juu.
 
sioni shida yeyote hapo, kwani ninyi mnaogopa nini? mnaogopa ushindani? ukienda china leo hii ukaseme ufanye kazi hizi za hali ya chini wakakuzuia utajisikiaje?

Sisi wabongo tufanye biashara tushindane nao, kwani tunawaogopa? na mbona bidhaa zao ni bei poa kuliko za kwenu au mnataka muendelee na syndicate zenu kuuzia watu vitu bei ya juu.
Uko sahihi,najaribu kuwaza watanzania walio USA, Canada,nk wanafanya kazi Gani kama sio hizi za ajabu ajabu,iweje wachina wazuiliwe!?
 
Uko sahihi,najaribu kuwaza watanzania walio USA, Canada,nk wanafanya kazi Gani kama sio hizi za ajabu ajabu,iweje wachina wazuiliwe!?
wachache sana waliowahi kuishi nje wakabaguliwa kwenye fursa ndio watakuwa na uelewa kwamba mchina akifanya kazi yeyote hapa, kama haingilii maslahi yako na hakudhuru, hakuna shida. mwacheni afanye biashara. au wanataka tuwe kama wasouth, wavivu, wakiona wabongo na wasomali wanafanya biashara, wanawauwa ati wanafaidikia kwenye nchi yao, kwani wewe bongo wa kariakoo ukiona mchina anfanya biashara, na wewe si ufanye? anakuzuia nini? weka service nzuri mshindane, kwani tukija kwenye duka lako bila uwepo wa wachina unatupatia bidhaa bure? wapambane wawashinde wachina. pia wajue na wao kuna sikuw ataenda china, watazuiwa, wataenda ufaransa watazuiwa, wataenda ulaya watazuiwa, watajisikiaje wakati wanatafuta kipato?
 
Nilienda ofisi za kinglion pale mwenge kununua guta iliniuma watanzania kuona wameajiliwa kwenye ajira za kutumwa tumwa na nzito zenye ujira mdogo wakati huo wachina wameshika nafasi zenye pesa nono na ambazo siyo za manguvu.Nikamuona mkurugenzi anaendeshwa kwenye V8GXR nikawaza hivi watanzania tunashindwa Nini kufanya biashara kama wenzetu?
 
Back
Top Bottom