Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Rais Samia Suluhu Hassan amewasili hivi punde Kariakoo, Dar es Salaam, ambapo jengo la Gorofa liliporomoka Jumamosi na kusababisha vifo vya watu na wengine kujeruhiwa.
Kuhusu ajali hiyo, soma LIVE - Live Updates Kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo Nov 16: Watu 16 wafariki 77 waokolewa
Alipofika eneo la tukio, Mkuu wa Nchi alikagua jengo lililoporomoka kabla ya kuhutubia wananchi.
Rais Samia Suluhu Hassan aliyekuwa nchini Brazil kwenye Mkutano wa G20 ametua jijini Dar es Salaam leo na moja kwa moja kuelekea eneo lilipoporomoka jengo Kariakoo. Amesema taarifa aliyopewa, Watu 20 wamepoteza maisha kwenye jengo hilo
Amesema
“Jitihada zetu kubwa katika tukio hili ilikuwa kuwaokoa wenzetu walionasa ndani ya jengo hili wakiwa hai, ndilo lengo letu lililokuwa kubwa, lakini kama tunavyoambiwa jitihada haiondoshi kudra ya Mungu au kadara ya Mungu, pamoja na jitihada iliyofanywa na serikali na waokoaji hawa walioko hapa lakini bado kuna wenzetu ambao tumewapoteza na taarifa niliyopewa leo ni kwamba mpaka saa tatu asubuhi tumepoteza wenzetu 20 ambao serikali imeshirikiana na familia kuwasitiri wenzetu ipasavyo, lakini wenzetu majeruhi ambao walikuwa wamepelekwa hospitali naambiwa kuna watu watatu tu na nikitoka hapa nitakwenda niwaone niwasalimie.”
“Hili sio pigo kwa Familia zilizopoteza Watu wao pekee yao ni pigo letu kama Watanzania na tunaguswa pia, ni kumbukumbu ya kutisha kwa wenzetu waliookoka hapa, kwa jinsi jengo lilivyo Mtu akitoka hai bila shaka hawapo sawa (kisaikolojia), niombe wasifadhaike, wajipe moyo na tuendelee na shughuli zetu za kawaida bado Mungu ana kazi nao”
“Tukio hili ukiangalia kwa macho tu lina viashiria vya kuwepo kwa mapungufu ya kiutendaji hivyo nitoe wito kila Mtu atimize wajibu wake ipasavyo, ukiangalia jengo lile lilipewa vibali kutoka Serikalini vya ujenzi lakini jengo lile halikutazamwa ubora wake wakati wa ujenzi, niwaombe wote tunaohusika Serikali Kuu, Halmashauri na Wananchi wote kwa ujumla tuseme kwa pamoja kwamba matukio ya aina hii yasijirudie”
PIA SOMA
- Rais Samia atoa pole kwa waathirika Kariakoo. Aagiza kufanywa kila linalowezekana kufanikisha zoezi la uokoaji na tiba kwa majeruhi
- ZIMAMOTO: Watano wamefariki, zaidi ya watu 40 wameokolewa ajali ya ghorofa Kariakoo
- Waziri Mkuu Majaliwa awasili lilipoporomoka jengo Kariakoo, uokoaji waendelea
- Ghorofa laendelea kushuka, zoezi la uokoaji lasimama, mwananchi watawanywa
- Sauti za waliofukiwa na Ghorofa Kariakoo: "Tuko hai lakini tunateseka, tusaidieni tutakufa"
- Waziri Mkuu Majaliwa aagiza Polisi kumtafuta mmiliki wa Jengo lililoporomoka Kariakoo
Kuhusu ajali hiyo, soma LIVE - Live Updates Kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo Nov 16: Watu 16 wafariki 77 waokolewa
Alipofika eneo la tukio, Mkuu wa Nchi alikagua jengo lililoporomoka kabla ya kuhutubia wananchi.
Rais Samia Suluhu Hassan aliyekuwa nchini Brazil kwenye Mkutano wa G20 ametua jijini Dar es Salaam leo na moja kwa moja kuelekea eneo lilipoporomoka jengo Kariakoo. Amesema taarifa aliyopewa, Watu 20 wamepoteza maisha kwenye jengo hilo
Amesema
“Jitihada zetu kubwa katika tukio hili ilikuwa kuwaokoa wenzetu walionasa ndani ya jengo hili wakiwa hai, ndilo lengo letu lililokuwa kubwa, lakini kama tunavyoambiwa jitihada haiondoshi kudra ya Mungu au kadara ya Mungu, pamoja na jitihada iliyofanywa na serikali na waokoaji hawa walioko hapa lakini bado kuna wenzetu ambao tumewapoteza na taarifa niliyopewa leo ni kwamba mpaka saa tatu asubuhi tumepoteza wenzetu 20 ambao serikali imeshirikiana na familia kuwasitiri wenzetu ipasavyo, lakini wenzetu majeruhi ambao walikuwa wamepelekwa hospitali naambiwa kuna watu watatu tu na nikitoka hapa nitakwenda niwaone niwasalimie.”
“Hili sio pigo kwa Familia zilizopoteza Watu wao pekee yao ni pigo letu kama Watanzania na tunaguswa pia, ni kumbukumbu ya kutisha kwa wenzetu waliookoka hapa, kwa jinsi jengo lilivyo Mtu akitoka hai bila shaka hawapo sawa (kisaikolojia), niombe wasifadhaike, wajipe moyo na tuendelee na shughuli zetu za kawaida bado Mungu ana kazi nao”
“Tukio hili ukiangalia kwa macho tu lina viashiria vya kuwepo kwa mapungufu ya kiutendaji hivyo nitoe wito kila Mtu atimize wajibu wake ipasavyo, ukiangalia jengo lile lilipewa vibali kutoka Serikalini vya ujenzi lakini jengo lile halikutazamwa ubora wake wakati wa ujenzi, niwaombe wote tunaohusika Serikali Kuu, Halmashauri na Wananchi wote kwa ujumla tuseme kwa pamoja kwamba matukio ya aina hii yasijirudie”
PIA SOMA
- Rais Samia atoa pole kwa waathirika Kariakoo. Aagiza kufanywa kila linalowezekana kufanikisha zoezi la uokoaji na tiba kwa majeruhi
- ZIMAMOTO: Watano wamefariki, zaidi ya watu 40 wameokolewa ajali ya ghorofa Kariakoo
- Waziri Mkuu Majaliwa awasili lilipoporomoka jengo Kariakoo, uokoaji waendelea
- Ghorofa laendelea kushuka, zoezi la uokoaji lasimama, mwananchi watawanywa
- Sauti za waliofukiwa na Ghorofa Kariakoo: "Tuko hai lakini tunateseka, tusaidieni tutakufa"
- Waziri Mkuu Majaliwa aagiza Polisi kumtafuta mmiliki wa Jengo lililoporomoka Kariakoo