Dar: Sakata la Polisi kuuana wenyewe nje ya benki laacha sintofahamu

Mie nitasema kitu kimoja kwa Askari Polisi wetu, waache ubabe.. Magwanda wanayovaa na silaha wanazoshika zisiwape kiburi na kuacha kutumia hekima na busara.. Wawe wanaongea na kuelekeza bila ya kuwawekea raia kibesi.. Kwa mujibu wa maelezo hapo juu, marehemu hakutumia kauli ya kibusara katika kumuelekeza huyo askari wa JWTZ.. Naamini angetumia kauli ya busara, basi angekuwa bado yupo hai.. Nimeshaona na mwenyewe kukutana na kauli za kibabe na kutisha toka kwa hawa Askari wetu..
 
Nadhani utakuwa umechanganya vitu au ni mmoja wa kundi lile.

Dereva wa treni akipita kwenye barabara haina tabu, ila akiamua kuipitisha treni barabara ya magari itakuwa ajabu.

Huwezi kuelekeza silaha ya moto kwa mtu asiye na silaha hata silaha baridi. Yuko mmoja, mko wengi, maneno yakufanye uoneshe nia ya kutumia silaha?

Zaidi, kwakuwa mjeda alijua kuwa jamaa akili zao huwa wanaziacha nyumbani baada ya kuvaa yunifomu, aliamua kuokoa nafsi yake na raia wengine kwa kuelekeze silaha juu.

Na askari gani unashindwa kulenga tageti? Au ndo mambo ya ilikata kona na kumpiga wa kwake?

Si ajabu yuke mwanafunzi kwenda na moto, akili zenu si ndo hizi!
 
Wana Jamvi,
Katika Utaratibu wa aina yoyote Kiutendaji intendaji lazima discipline izingatiwe.
Mwanajeshi ni Mtu alipewa dhamana ya nchi hii, hivyo anapaswa kuwa mwadilifu na mwenue adabu katika kila jambo.
Aliona wale wakiwa katika utendaji na anajua wazi ubebaji na usafirishaji wa pesa ni kitu cha hatari isipokuwa tu kwa sababu mwanajeshi ni mkaidi mjinga asiejua mchango wake kwa taiga haya yote yametokea kwa ajili yake.
Kama lilikuea no swala la kudharauliwa angetii amri FFU wamalize kazi yao kisha awaulize madai take.
Anastaili kushtakiwa. Charge 1distortion or causing commotion to a working team causing them fail to render their services as carriage and preventive officers 2 causing death kama sheria zipo Tanzania na wanasheria wapo, Huyo! Wapeleke ukonga.
 
TUNASHUKURU KAMA HUYO Mwanajeshi yuko salama

Polisi, alishndwaje kuvumilia jamaa atoe hela kwa sababu ni kitendo cha dakika moja tu

Halafu sheria ya bunduki, usikwoneshe mtu ambaye huna nia ya kumpiga risasi
Utawezaje kutoa pesa ATM wakati wanaweka ,,, Elimu muhimu sana si kwa majeshi tu Bali kwa jamii nzima .
 
Huwezi kuwa na Busara kama huna elimu. Tuangalie wapi kuna makosa parekebishwe na siyo kutoa kawama.

Pole sana mwanajeshi
 
Huyu mwanajeshi ni hodari wa kujikinga.
Nahisi aliona mfyatua risasi anamlenga kisha akamuweka polisi kama kinga.
Polisi haruhusiwi kufyatua risasi kwa mtu ambaye hana silaha.
Ingetokea mwanajeshi amemnyang'anya polisi silaha na kutaka kuitumia kupiga, polisi angekuwa na haki ya
kutumia silaha yake.
Kuna mapungufu makubwa sana kwa polisi wetu katika kanuni za kutumia silaha za moto wakati wa matukio madogo.
 
Siwezi kumlaumu polisi au mwanajeshi kwakuwa sijashuhudia tukio.

Lakini nakumbuka wiki iliyopita nilienda kwenye ATM moja pale makumbusho sikujua kama ndani wanaweka hela, ile nasogea tu nikaambiwa na askari "toka, pita kule usisogee hapa" kwa ukali na lugha nyingine zisizoelezeka huku ameninyooshea bunduki.
Kila mteja aliyekuja pale alipatwa na kadhia hyo.

Tunaomba askari wetu wawe na lugha nzuri kwa raia, utanitukanaje wakati sijajua kama ndani wanaweka hela, si uniambie tu kwa kawaida?
Na je unavyoninyooshea bunduki risasi ikitoka ikanipata utasema ni bahati mbaya au Mimi ni jambazi? Mjitafakari nyie polisi.
 
Amekopi gazetini
 
maelekezo ya kipuuzi na ya kibabe ndio chanzo cha yote haya.walioendelea wanatenda kama hii mipuuzi yetu ? sio wote namaanisha baadhi ya mipuuzi yetu !!
 
Wewe ni Polisi?
 
Hawa ndo wale walikuwa kwenye lile kundi lililotembeza kichapo kwa raia maeneo ya ukonga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…