DAR: Sheikh wa Mkoa, Mussa Alhad atangaza mwisho wa Mange Kimambi kutukana, kushughulika na JamiiForums kisheria

shekhe amekutana na chizi ambae amerogwa siku nyingi sana hahahahahahahaaa.....shekhe anatia huruma Mungu wangu anazidi kuvuliwa nguo tu inabidi asome leo hili kesho afariki chizi ambae kesharogwa tayari....kumbe ustadh anaudhuria sana tigo fiestaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.............
 
Kweli sheikh kujibu hoja kwa kutishia bado hujasimama katika msingi wa kiisilam nilijua ungejieleza tu na uendelee na yako hadi kutishia kushitaki kuna nini kimekugusa hapo au kuna ukweli kuwa umepiga kampeni? Maana sio mara moja wala mbili mashehe wameshawahi kupiga kampeni za kisiasa misikitini nami nikiwemo mungu anawaona manaposimami na anajua ukweli kamili, Siungi mkono matusi ya mange lakini kwenye tuhuma kunaweza mukawa na ukweli mashehe fanyeni mambo ya mungu acheni kujiingiza kwenye siasa mnatugawa waumini wenu mungu anawaona
 
Reputation ya sheikh inaweza ikashuka ghafla, nadhani hakunaga mtu ambae aligombana na Mange akabaki salama,.kakosea sana kumjibu.Mange ana source nyingi sana za info,wadangaji wote wa
Mjini wapo kule kwa mange,so yeye akilianzisha tu bhasi info zinakuwa zina flow tu. He has to learn from mh.Paul makonda
 
Unamaanisha huyo shehe mpenda ubwabwa yupo karibu na Mungu ??[emoji23][emoji23]

Kuwa katika position kama yake sio kitu cha mchezo mchezo tu

Maana ingekuwa ni rahisi hata wewe ungekuwa hapo
Lakini ana kipawa ambacho Mwenye Enzi Mungu anemtunuku!

Ndiyo maana kwenye Biblia Takatifu Mfalme Daudi hakuthubutu kumwuua Mfalme Sauli, tena alimwita mpakwa mafuta wa Mola, akamwambia Mwenye Enzi Mungu pekee ndiyo atakaye kuhukumu!

Hivi viti wanavyo kalia wakuu wa dini sio vya mchezo, ni watu wanao shika roho za watu yaani ni IMANI!

Tuwe wasngalifu sana kwenye maswala haya!

Tusiwafanye wakakunja roho zao!

Kweli nawaambia mwisho wake huwa sio mzuri hata!
 
Rudia lalamiko la mange kuhusu kauli ya shekhe kukemea kuchanganya dini na siasa baada ya maaskofu Fulani kuonekana kukosoa,halafu ujijibu mwwnyewe
Oh! Kumbe Mange...!! Yaani kwavile Mange kasema ndo basi tena unashindwa kutumia uelewa wako mwenyewe kupima?!

Kwanza nini maana ya kuchanganya dini na siasa?! Huyo Sheikh alikuwa anaongea mambo ya siasa msikitini hadi useme anachanganya dini na siasa?!

Isitoshe, picha ambayo uliisema wewe ni hii hapa:


Hapo juu unaona maelezo yanasema " Mbunge wa Temeke Abbas Mtemvu Akimkarisbisha Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam"

Hivi sasa Mbunge wa Temeke ni Abbas Mtemvu?!

Maelezo zaidi ya hiyo picha yanasema:
Kumbe kulikuwa na Mkutano Mkuu wa Jimbo la Temeke... lakini kwa kuwa mnameza kila mnacholishwa na Mange, mkakubali tu kwamba alikuwa kwenye kampeni za Ubunge Kinondoni!!!

Lakini mbaya zaidi, ni wakati Mbunge wa Temeke ni Abbas Mtemvu ambae hakurudi tena bungeni kwenye uchaguzi wa 2015. Kumbe kwa maana nyingine, mmelishwa matango pori kwa kuwekewa picha za zamani!!!

Picha zingine za hilo tukio ni hii hapa:




Na hili usidhani kwamba ni photoshop, tukio zima lipo hapa!

Au ni picha zipi hizo unazosema kwamba alikuwa anachanganya dini na siasa?!
 
Reactions: BAK
Albadili mpaka ipate e-passport ikapate viza ya states of america si jambo dogo akiulizwa sabb ya kupeleka marekan??? Na hapo kunamawili kama haijawah kupanda ndege itagoma ndege masikhara ingekua hapa hapa bongo labda
 
CCM wameitumia fursa ya Sheikh wa mkoa wa Dar-es-Salaam kupiga propaganda ktk uchaguzi mdogo wa Kinondoni.

Wito kwa sheikh wetu wa Mkoa BAKWATA Dar-es-Salaam kuwa mwaangalifu kuhudhuria hafla ambazo CCM au viongozi wateuliwa wa awamu hii ya tano watamualika au kuwepo mahali hapo.

Jamiiforums haihusiki kwa namna yeyote na sakata la Shehe wetu Alhad Mussa Salim kukaangwa na jamii ya watanzania "kisiasa".
 
Hakuna dua ya mwovu inayoweza kumshika huyo dada maana matusi ni sehemu ndogo tu ya maisha yake hivyo huyo sheikh atavuliwa nguo tu hadi akome maana hana akili timamu kusimama kama kiongozi wa kidini.

Watu wanaomwombea huyo Mange ni wengi si tu raia wa kawaida bali hata baadhi ya viongozi wanafurahia uwepo wake 100%
 
Yeyote anayejaribu kusaliti maslahi ya mungu kwa watu wake kwa ajili ya maslahi yake mwenyewe hatakuwa salama. Kumbuka ya yuda na vipande thelathini. Shekhe wa mkoa wa dar jitafakari upya. Watu wa mungu hawawi hivi, wewe ni tofauti
 
Huyu shekhe nae
Hahahhahaha et atamshtaki mahakama ya mbiguni kwakwakwkwa,,,tz kuna vituko
 
Viongozi wa dini wanapaswa kuwa na subira wao ni viongozi. Kumnuizia mtu jambo baya kwa sababu yeyote ile si halali, hii ni dalili ya kushindwa kuwa na subira. Ukiona umeshindwa kuwa na subira mbele ya Mwenyezi Mungu chukuwa hatua. Mungu tujalie heri na subira, tuvumiliane kwani hi dunia imejaa wanaadamu wa tabia tofauti na wote wapo chini ya viongozi wa kiroho.
 
Si kila kiongozi ni mtu wa Mungu kuna wengine ni watu wa Ibilisi sasa jiulize walifikaje huko juu soma hapa
[emoji116]
16 Kwa maana wawaongozao watu hawa ndio wawakoseshao, na hao walioongozwa na watu hao wameangamia.
Isaya 9 :16

Mara ngapi tumesikia masheikh, mapadri na hata maaskofu wamefumwa wakizini na hata kulawiti?

Hivi unajua kuwa kuna viongozi wa kidini walifika hapo kwa hongo? [emoji23] [emoji23] [emoji23] tulia kabisa viongozi wengine ni takataka kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…