DAR: Sheikh wa Mkoa, Mussa Alhad atangaza mwisho wa Mange Kimambi kutukana, kushughulika na JamiiForums kisheria

DAR: Sheikh wa Mkoa, Mussa Alhad atangaza mwisho wa Mange Kimambi kutukana, kushughulika na JamiiForums kisheria

Hicho anachokieleza kwamba Mange "ataondoka" ni kuwazia mambo yasiyowezekana! Katika nyakati zetu ni lazima kuacha kutumia matisho kama zamani kwamba ukimfanya hivi dhidi ya dini utadhurika. Kama anamaanisha kuwa Yeye Sheikh na viongozi wenzie watamuomba Mungu ili "amupumzishe" Kimange hilo ni jambo ambalo Mungu hawezi kufanya kabisa! Labda kama kuna Mungu tofauti na tunayemjua wengine. Ningeelewa zaidi ikiwa angemuombea Mange maisha marefu na kujaliwa moyo Wa kutambua makosa yake na kutubu.
Huyu Mungu wetu si wa visasi. Yeye hufanya njia pasipo na njia, kama Lisu walishindwa kumuua huku CCTV zikiwa zimeximwa kwa watu wasiojulikana na bunduki za kivita zilindima kwenye makao makuu ya nchi yenye ulinzi wa nchi bila mafanikio yeye atatumia nini? Labda awasiliana na Rais Kim wa Northern Korea
 
hawa masheikh ambao ccm wanawahonga pilau watupishilie mbali....badala ya kudai haki zinzovunjwa na ccm ww unhangaika na mange....alafu mange hajatukana sisi waislamu bali ww mchumia tumbo unakataka maaskofu wasifanye siasa ww unapigia kampeni ccm kwa ubwabwa tu
 
Sheikh wangu Alhad pole sana ila ulitakiwa ukae kimya sio kujibizana na chizi Mabge maana kazidi kuyasema tusiyotaka kuyasikia. Tafadhali kaa kimya haya yatapita tu
 
Kwahiyo ni dhambi au ukiukwaji wa sheria kwake kuwepo kwenye hicho kikao?
Rudia lalamiko la mange kuhusu kauli ya shekhe kukemea kuchanganya dini na siasa baada ya maaskofu Fulani kuonekana kukosoa,halafu ujijibu mwwnyewe
 
siasa hazijawahi kumuacha shekhe salama, kutumika ni kubata sana shekhe wangu!
 
Utofauti wa viongozi wa kislam na kikatoliki unauona hapa.
Ingekuwa ni askofu katukanwa hivyo wala asinge hangaika kujibu.

Kusoma falsafa na theoloji inasaidia kutoshiriki kwenye ujinga
Biblia inasema msikae barazani kwa wenye mizaha!
 
Mchumia tumbo tu huyo hana jipya ...SHEkhe SHEkhe ndio nni
.!!?
Anataka kuwa aminisha watu kuwa yeye hatendi uovu ..nayeye nikama nani haswaa mpka asisemwe ..kwahii statement yake yaonyesha wazi kuwa hapaswi kupewa cheo chakuwaongoza watu ktk dini hii ya uislam mafudisho ya dini yetu yanatukumbusha kuwa mtume muhhamad alifanyiwa vitimbi vikubwa mnoo ikiwemo hata kupigwa mawe na kutemewa mate ..na MUNGU ALIPOMTUMA MALAIKA WAKE KUMUULIZA MUHHAMAD ANGEPENDA ADHABU IPI ITOLEWE KWAWATU WALE ..MUHHAMAD ALIJIBU KWA BUSARA KABISA KUWA ANAMUOMBA MUNGU AJAALIE WATU WOTE WALE WALIOMPIGA MAWE MPKA VIZAZI VYAO VIPOKEE YALE MAFUNDISHO YAKE NA WAWE WAISLAM ....SASA YEYE KATUKANWA KIDOGO TU TENA NA MANGE BASI KACHACHAWA ..JE ANGETISHIWA MAISHA NA SIZONJE SINDIO ANGEIKANA DINI YAKE KABISA...FOOLISH
 
Hapa napo ni msibani?
FB_IMG_1517843666582.jpg
 
Mtumishi Wa mungu anamtisha mtu badala kumwombea abadilike jamani au ni Mtumishi Wa ccm
hilo neno lako LA mwisho pigia mstari ..tena usije kushangaa pindi atkpoitwa white house na kupewa bahasha ya kaki kama pongezi ya hiki alichokifnya
 
kukaa kimya nako ni ujumbe tosha.wewe sio mtu wa mitandao, waachie akina le mutuz na wengine lakini sio wewe,kesho tukisikia mitandaoni umefanya hiki hiki unadhani watakuonea huruma.sheikh wa ajabu kuwai kutokea kwenye mkoa wetu ni huyu,hana busara kabisa anawaza mabaya kwa watu,nini maana ya kiongozi wa dini?
 
Ha haa! Mbona shekhe amepanic kwa ishu ndogo tu kama hiii? Mwambieni asijisumbue na JF! Wenzake wameishitaki mahakamani mwaka mmoja sasa bado kesi haijahisha. Kama ana muda wa kupoteza wa kwenda na kurudi mahakamani, basi mwambieni aende ila asitegemee kama ataweza kupata ushindi...
 


Sheikh wa Mkoa wa Dar es salaam Sheikh Alhad Mussa Salim hivi sasa anazungumza na waandishi wa vyombo vya habari kuhusiana na kuhusishwa na kampeni zinazoendelea katika Jimbo la Kinondoni.

=====

Sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Mussa Alhad ameelezea picha inayosambaa kwenye mitandao inayomuhusisha yeye kufanya kampeni ambayo yumo yeye na pembeni kuna mgombea wa CCM jimbo la Kinondoni, Maulid Mtulia akila chakula pamoja na wenzake wa CCM. Amesema picha ilipigwa akiwa kwenye maziko ya Sheikh Masoud Ismail, amesema yeye ni kiongozi na mtu yeyote anaweza kupiga picha na yeye.

Amedai Mange Kimambi amekuwa akitukana viongozi mbalimbali kwenye Instagram na kusema pia alimtukana mufti wa Tanzania baada ya kuipongeza serikali na Rais John Magufuli.

Sheikh Alhad amesema ametukanwa kwa dhulma na uadui na kudai Mange anautumia ulimi na mikono yake vibaya kudhulumu watu(Heshima zao).

Alhad amesisitiza huu ni mwaka wa mwisho kwa Mange na baada ya mwaka huu hatamtukana mtu yeyote kwa kutumia ulimi au mkono wake kwa sababu amejihalalishia mwenyewe maangamizi kwa mkono wake. Amesema atamshtaki kwenye mahakama ya Mbinguni.

Juu ya tuhuma za Sheikh kushiriki siasa, soma => Picha za Sheikh Alhad Mussa na makada wa CCM zinatoa tafsiri gani? BAKWATA toeni ufafanuzi


Amesema kuna watu walimpa rai asimjibu kwani atamtukana sana na kudai wao wanataka aendelee kutukana na hatasikia sauti yake baada ya leo ikimjibu na yeye andelee kutukana.

Alhad amesema hawezi kujiingiza kwenye kampeni ya kuipigia debe CCM, amesema CCM ina kawaida ya kualika viongozi wa dini na chama chochote kinaweza kumualika kwenye jambo lake. Amesema ajabu, picha zake ndio zinaanikwa lakini za viongozi wengine hazianikwi.

Katika hatua nyingine, Sheikh ameiambia NEC kuhusu JamiiForums ambao wameandika kwamba sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam: Hivi mnajua kama anafanya kampeni Kinondoni! Alhad amesema watachukua hatua za kisheria ili wathibitishe sheikh wa mkoa wapi amefanya kampeni, kwa kuhudhuria kwenye maziko au sababu ya picha!.

Hivyo kuhusu JamiiForums, wataona namna gani ya kushughulika nao kisheria na wengine wote ambao kwa namna moja au nyingine, wajiingiza katika jambo hilo kichwa kichwa bila kulijua ili kuvunja heshma zao.

Nikiri kuwa mimi ni Muislamu.
Pia nikiri kuwa mimi nimpenda mageuzi na kuwa na upinzani ulio na nguvu.Pia msimamo wa sheikh Alhad nilishautilia shaka kwani alionekana na anaonekana kuwa huko biased kwani hatujamwona kwenye shughuli za vyama vingine.
Hili la kumjibu Mange ni kama vile kuibiwa nguo na kumkimbiza mwizi wa nguo.Sheikh utaudhalilisha Uislamu,muache Mange na yake.
 
Uchawi hauvuki bahari hata siku moja.Mwisho wake hapo Kigamboni halafu unaelekea Mbagala.
Shekhe atulie tu
 
Back
Top Bottom