Dar: Show ya Heshima kwa Wakongwe wa Bongo Fleva si ya Kukosa

Dar: Show ya Heshima kwa Wakongwe wa Bongo Fleva si ya Kukosa

pantheraleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2013
Posts
692
Reaction score
880
Deiwaka World chini ya Joseph Mbilinyi “SUGU” kwa kushirikiana na Alliance Francaise (Kituo cha Utamaduni cha Ufaransa), imeandaa “Bongo Flava Honors” Concerts ambalo ni Jukwaa mahsusi kwa Wakongwe wa Bongo Flava.

Concerts hizi zitafanyika Alliance Francaise, Upanga, Dar Es Salaam.

Kila mwezi kutakuwa na Concert moja kwa ajili ya Mkongwe mmoja, ambapo Mkongwe huyo atafanya Show live kwa kupigiwa na band ya Swahili Blues na usiku wote utakuwa ni maalum (dedicated) kwa ajili yake.

Madhumuni ya BongoFlava Honors ni kuweza kuwa na Jukwaa litakalotumika kutambua na kuheshimisha muziki wa Wakongwe wa Bongoflava, na pia kuwapa fursa mashabiki wa enzi hizo (Golden Era) za muziki huu kujikumbusha na kupata burudani ambayo wameikosa kwa muda mrefu na wanaitamani .

Na pia Bongo Flava Honors zitasaidia kuondoa gap kati ya zamani na sasa, Mashabiki wa zama mpya wanatapata nafasi ya kuona Wakongwe mbalimbali na kuweza kufuatilia historia ya muziki wetu kupitia ratiba hizi za kila mwezi.

Mwezi huu tarehe Februari 24, 2023 siku ya Ijumaa kuanzia saa 12 jioni mpaka saa 6 usiku. Tutakuwa na Mkongwe TID.

Host wa Concerts hizi za kila mwezi atakuwa ni Msanii mkongwe Sugu, na pia atakuwepo Dj Mkongwe Boni Luv kwa burudani zaidi.

KARIBUNI NYOTE!
#HeshimaKwaWakongwe

9cea5a417bb94a1dbad1f96e05b6f548.jpg
 
Boonge la "aidia" ni vile tu naishi Ilala vijijini so ni mbali kidogo na City center!!
Ningefurahi kuhudhuria!
 
Tatizo wasanii wazamani wengi wamekuwa wavuta bangi na unga...Hii yote ni sababu ya stress za kupata hela na kuzichezea sasa wamebaki kapuku....Tusishangae kuwaona wanavua mpaka nguo Majukwaani na kubaki uchi....Wakwanza atakuwa huyo TID.
 
Tatizo wasanii wazamani wengi wamekuwa wavuta bangi na unga...Hii yote ni sababu ya stress za kupata hela na kuzichezea sasa wamebaki kapuku....Tusishangae kuwaona wanavua mpaka nguo Majukwaani na kubaki uchi....Wakwanza atakuwa huyo TID.
Heshim wasani wa zamani
Bila wao mziki wenu usingefika
Hapa,watu wamefanya movement
Za kutosha
Heshimu ma legend

Ova
 
Ungejua struggling walizofanya hadi muziki huu unamekubalika ungewapa heshina zao.
Achana na kina Diplomatz watoto wa kishua, Rmread the history utajua mengi na naamini utawapa heshima!!!
 
Back
Top Bottom