Dar: Wafanyakazi wawili wa Kampuni ya Mwananchi Communication wakamatwa kwa kusambaza taarifa za uongo za Corona

Dar: Wafanyakazi wawili wa Kampuni ya Mwananchi Communication wakamatwa kwa kusambaza taarifa za uongo za Corona

Influenza

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2018
Posts
1,509
Reaction score
3,756
Jeshi la Polisi Kinondoni limesema limefanikiwa kuwakamata Wafanyakazi wawili wa Kampuni ya Mwananchi Communication-Kitengo cha Matangazo kwa tuhuma za kutuma taarifa za uongo na uzushi kuhusu #COVID19

Limesema waliokamatwa ni Hidari Hakimu (27), Afisa Biashara kwenye Kampuni hiyo ambaye ni mkazi wa Kigamboni pamoja na Alona Tarimo (42), Afisa Biashara ambaye ni mkazi wa Masaki

Hidari anadaiwa kuandika katika WhatsApp “Za chinichini kuna Padri wa Peramiho amefariki na Ugonjwa wa Corona. Alitokea Italia, akakaa Dar kidogo kisha akaelekea Mbeya kwa kutumia ndege na baadaye akatumia ‘private’ kuelekea Songea. Akazidiwa akawa ICU kule Peramiho na sasa amefariki. Waliomuhudumia wamewekwa katantini.”

Polisi wameeleza kuwa ujumbe huo uliotumwa Aprili 5, 2020 uliungwa mkono siku hiyo hiyo na Alona aliyeposti katika kundi hilo hilo la WhatsApp kuwa “Hizi Kigogo hajazipata ili aposti, then Serikali waweke wazi.”

Alona naye kwa kutumia simu yake Aprili 29, 2020 anadaiwa kutuma ujumbe katika mtandao wa WhatsApp unaosema “Mbezi Beach karibu na Kanisa la Mloganzila kuna Mzee kaondoka na Corona. Sorry Mloganzila Katoliki nimedata yaani."

Polisi wamefafanua kuwa Watuhumiwa hawa walituma taarifa hizo katika mitandao huku wakifahamu fika taarifa hizo ni za uzushi na uongo na hazina ukweli wowote
 
  1. Tunakusihi jitahidi kuosha mikono kwa maji safi na sabuni mara kwa mara
  2. Kwa siku chache hizi jaribu kutulia nyumbani kuepusha maambukizi
 
Mawasiliano ya watu private mnaingilia ya nini?Hayo ni personal

Likishakuwa kundi hakuna tena mawasiliano "private and personal." Serikali imo kwenye hayo makundi kwa kuomba kuunganishwa na kukubaliwa, utasemaje wameingilia mawasiliano private and personal?

Unapokuwa kwenye kundi hujui nani mwingine upo nae, na huna control juu ya nani mwingine anaingizwa, hata ungekuwa ni group admin, hauko admin peke yako. Kisheria hakuna ghafala, there is no reasonable expectation of privacy.
 
Polisi wanapambana Kama kipindi kile jiwe ameingia ikulu wao wenyewe Wako Kwenye jamii na huu ugonjwa unagusa kila Kona watakua wapolee tu Kama mwanzo.
 
Halafu unamsikia Bwana Msando anasema waandishi wapige kelele. Kama kwenye magroup ya Whatsapp inakuwa tabu hivi, itakuwa kwenye front page kweli?
 
Back
Top Bottom