Dar: Wakazi wa eneo la Kunduchi Mtongani ambao nyumba zao zimepitiwa na ujiuji wa volcano ya tope, watakiwa kuhama

RC wa Mkoa wa Dar Es Salaam Aboubakar Kunenge awataka baadhi ya wakazi wa eneo la Kunduchi Mtongani ambao nyumba zao zimeathiriwa na uji wa tope la volcano kuhama katika eneo hilo.

Chanzo: ITV

My take: Hiki ni kitu gani au ndio dalili ya volcano na madhara yake ni nini?
 
Mshambiwa hameni msije mkasema hamjambiwa

Ova

Wataalam wa jiolojia wa Chuo kikuu DSM, Jana sikuona wanatoa sababu za kisayansi kuhusu tukio hilo - walikuwa wana zungumza kama ma layman vile!!

Binafsi naona tukio hilo haliwezi kuwa limesababishwa na Volcano kwa kuwa hapakuwepo na moto, lojolojo ya miamba nk.
 
... Let's wait for Geological Survey of America achana na wawinda teuzi Chief.
 
Hilo tope limekuaje mkuu,una pic au link nipate vizuri hii habari ,am interested it sounds km mother nature
 
Natoa wito kwa kamati ya Amani mkoa wa Dsm inayoongozwa na Alhad Mussa Salum dua zao zisiishie kwa wanasiasa tu bali wazielekeze kwa jamii nzima.

Kunduchi mtongani kuna tishio la makanisa takribani matano kuzolewa na tope baridi la Volcano. Makanisa hayo ni KKKT, Anglican, Katoliki, Sabato na Pentecoste yaliyo karibu karibu katika eneo linalonyemelewa na tope maji la volcano.

Ninajua shehe Alhad Salum na msaidizi wako askofu Gamanywa mnapita hapa JF, Tafadhali sana kamati yenu izuru eneo la maafa hapo Kunduchi mtongani kwa diwani Urio.

Maendeleo hayana vyama!
 
Hivi pale ile ni Volcano kumbe mana kama sikosei wk ile kuna mtoto alitumbukia pale akatolewa sasa Volcano ukitumbukia kama unakuwa mzima sijui ni Volcano gani hiyo ila ninavyofahamh pale hadi Bemaco bev kwenye zile kota ni eneo la maji mana linaenda mpaka kokoni kule kwa mzee ndevu
 
Mabingwa kutoka vyuo vyetu vinavuoheshimika hata wao hawana uhakika ni nini kimetokea!
 
Mabingwa kutoka vyuo vyetu vinavuoheshimika hata wao hawana uhakika ni nini kimetokea!
Ni kawaida ya wasomi wetu ila mi ninavyofahamu lile eneo kwa wenyeji ni eneo ambalo linaonyesha lina maji mengi sana na ndio mana zile nyumba za pale bemaco zimetitia na hata ukienda mpaka eneo la kanisa la KKKT kile kidogo kilititia kabla la hilo kubwa kujenga na hata nyumba zilizopo maeneo ya kuanzia pale kwa Mwalimu dachi zote zinaonyesha kumezwa ila kwa Volcano sijui japo nilikuta maneno ya watu wanasema hivyo ila swali langu linabaki vile vile inamana Volcano mtu akizama ukimtoa haungui kumbe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…