Dar yakumbwa na Mgao wa Maji. Ratiba ipo hivi;

Dar yakumbwa na Mgao wa Maji. Ratiba ipo hivi;

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Ikiwa ni Wiki ya Pili sasa mgao ukiendelea kimya kimya, hatimaye DAWASA yatoa ratiba ya Mgawo wa Maji.

Nanukuu kiongozi wa Mkoa: "Naomba niwaambie wananchi kuwa mgawo haupekuki kutokana na ukame ambao tayari TMA ilishatangaza kuwepo kwa hali hii muda mrefu kulikosababishwa na kunyesha kwa mvua chache msimu wa mvua uliopita na kuchelewa kunyesha kwa mvua katika msimu huu wa vuli.

"Pia watu waelewe hali hii haisababishwi na Serikali wala sera za CCM bali ni mipango ya Mungu, hivyo asitokee mtu huko akaanza kupotosha huko, kikubwa tuendelee kumuomba Mungu atuletee mvua za vuli na vyanzo vyetu vya maji viweze kujaa,” alisema Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makalla siku ya Jumanne 25 Oktoba 2022 baada ya kutembelea vyanzo vya vya kuzalisha maji vya Ruvu Chini na Ruvu Juu.

IMG_20221026_234104_009.jpg

Screenshot_20221027-030745.jpg
 
Hiyo ratiba haitakuwa hivyo.

Baadhi itapitiliza zaidi hata siku tano au hakuna kabisa na baadhi watapata maeneo fulani.

Kilichobaki tuombe Mungu tu, ajaalie uadilifu, neema na kutuepusha na shida za maisha.

Na umeme nao utaanza kwa nguvu zaidi na joto lina kuja na mwisho wa mwaka karibu.

Na shule zimeongeza ada na ulipe mapema kuanzia November.

Bado mwezi ujao bei ya mafuta huenda ikapanda.
 
Mbezi ya kimara na maeneo hayo mpaka ubungo hakuna mgao? Kinyerezi na gmboto je? Naona hakujatajwa.
 
Kama yuko aliyeona Ilala itanufaika siku gani naomba anijulishe. Nataka kuandaa vyombo vya kuwekea maji
 
Sala sala Mbezi beach hakuna maji kama ratiba inavyoonyesha..
 
Sijaona Kiluvya ikitajwa hapo.

Hivi Kiluvya ipo Pwani au Dar?
 
"Pia watu waelewe hali hii haisababishwi na Serikali wala sera za CCM bali ni mipango ya Mungu, hivyo asitokee mtu huko akaanza kupotosha huko, kikubwa tuendelee kumuomba Mungu atuletee mvua za vuli na vyanzo vyetu vya maji viweze kujaa,” alisema Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makalla siku ya Jumanne 25 Oktoba 2022 baada ya kutembelea vyanzo vya vya kuzalisha maji vya Ruvu Chini na Ruvu
Amos ni wa dar?
 
Back
Top Bottom