Dar yakusanya Tsh. Trilioni 13 kati ya 16.5 zilizokusanywa na TRA. Ni aibu kwa Tanzania kutegemea 80% ya Mapato kutoka Mkoa mmoja

Dar yakusanya Tsh. Trilioni 13 kati ya 16.5 zilizokusanywa na TRA. Ni aibu kwa Tanzania kutegemea 80% ya Mapato kutoka Mkoa mmoja

With last December's release of GDP numbers by the Bureau of Economic Analysis (BEA), the top five states – which contribute 41% of the total U.S. GDP in 2022 – were California, Texas, New York, Florida, and Illinois, in that order. Figure 1 shows the real GDP for these states in trillions of dollars. Size matters

Sijui kama utaelewa ila acha uvizu soma sio kukurupuka tu, ikiwa states 5 tu zinachangia 41% hiyo 59% gawa kwa states 45 au hesabu ngumu tukusaidie.
Lakini waoa Uchumi wao sio centrally planned kama huku Bongo.

Wana formula nzuri ya mgawanyo na mchango wa Kila states kwenye federal unlike hapa Tanzania

So huo sio mfano mzuri wa kulinganisha na Tanzania.
 
Jinga kweli,kama GDP ni hela Mwanza ingekuwa namba 2 Kwa kuchangia pesa nyingi ,badala yake inazidiwa Hadi na Songwe 😁😁
Screenshot_20250212-131435_1.jpg

Labda income ni makaratasi sio pesa
 
Sasa mada ni GDP au mapato ya kodi ...maana alicholeta mtoa uzi ni mapato ya kodi sio GDP ...sio ajabu kwa nchi kuwa na GDP kubwa kwenye eneo moja kuliko mengine ila ni ajabu kwa nchi kuwa na collection ya mapato kubwa eneo moja kuliko mikoa mingine
Sasa ukitaka kulete kodi nikuulize wewe bidhaa gani inaingia Tanzania bila kupitia bandari ya Dar? kila unacho kula wewe au kujaza mafuta yote yanalipiwa Dar mpaka kampuni zote za simu zinalipa Dar. Kipimo sahihi cha uchangiaji pato kwa mkoa ni uzalishaji.
 
Lakini waoa Uchumi wao sio centrally planned kama huku Bongo.

Wana formula nzuri ya mgawanyo na mchango wa Kila states kwenye federal unlike hapa Tanzania

So huo sio mfano mzuri wa kulinganisha na Tanzania.
Ndio maana inakuwa sio sawa pia kusema Dar inachangia 80% maana bidhaa zote zinapita Dar na zinalipiwa hapo. Kama tunataka kupima basi tungefanya kama Zanzibar wao wanakusanya chao na bidhaa hiyo ikifika Dar inapigwa tena kodi kwa maana kama ushindani. Kwa hapa tungesema kama umeleta mafuta na liter Mil 2 unapeleka soko la Arusha basi yanapita kama transit ikifika Arusha yanalipiwa. USA japo nchi moja ila ni states na mifumo ta Tax tofauti ushindani. Ndio maana kusema Dar 80% ni kwa sababu ya mfumo wetu wa kukusanya kodi unaipa hiyo 80%.
 
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imesema Mkoa wa Dar es Salaam ni wa kipekee katika ukusanyaji wa mapato nchini.

Kamishna Mkuu wa TRA, Yusuph Mwenda alisema hayo Dar es Salaam juzi usiku wakati wa hafla ya kuwapa tuzo walipa kodi bora wa mikoa ya kikodi ya Dar es Salaam kwa mwaka 2023/2024.

Mwenda alisema Dar es Salaam ni mkoa wa kipekee kwa kuwa kuna mikoa mitano ya kikodi: Ilala, Temeke, Kinondoni, Tegeta na Kariakoo. “Licha ya kuwa na mikoa mitano ipo Idara ya Forodha na ina mikoa mitatu mikubwa, kuna Kituo cha Huduma Maalumu, Kituo cha Kukusanya Kodi za Mafuta na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ambako tunakusanya kodi,” alisema.

Mwenda alisema sababu hizo na nyinginezo ziliwezesha TRA ikusanye Sh trilioni 16.5 kuanzia Julai hadi Desemba mwaka 2024 na kati ya fedha hizo trilioni 13 zilikusanywa katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Habari Leo

===

MY TAKE

Kitendo cha Nchi kutegemea asilimia 80% ya Mapato Kwa Mkoa mmja wa Dar ni jambo la ajabu na la kushangaza na inaonesha jinsi Nchi Ina uneven distribution of resources. Pia soma Miaka Zaidi ya 60 Baada ya Uhuru,Tanzania Imeshindwa Kuondoa Mizizi ya Ukoloni Kwa Nchi kuwa tegemezi wa Uchumi na Mapato Kwa Jiji Moja tuu la Dar

Hatuwezi kuendelea na utaratibu huu,ni muda muafaka sasa Kwa Serikali kutawanya maendeleo na economic centres kwenye Kila Kanda.

Kwamba Mikoa 25 inakusanya Trilioni 3.5 yaani hata nusu ya Mapato ya Dar hayafiki harafu Walioko kwenye Utawala wanaona sawa Dependency ya hivi Kwa Mkoa mmja Haina Afya kiuchumi na ni hatari sana kiusalama.

Hivi tuna watu wa Mipango kweli? Hivyo Vyuo vyenu vya Planning mnafundisha nini Sasa? Mambo kama haya ndio yanafanya watu waamini mtu mweusi hajatimia kichwani.

Ngoja ije itokee Dar kuwa paralysed siku Moja Kwa tukio.loloye ndipo akili zitawajia maana Mtu mweusi Huwa hajifunzi na hana akili za kesho Hadi apigwe tukio.

Soma hapa zaidi Mikoa 13 Kinara wa Kuchangia Kodi ya TRA mwaka 2023
Wakati Dar pekee wanakusanya Trilioni 13 Kwa miezi 6 eti Hawa Kagera wamevuka malengo Kwa kukusanya Bilioni 92 😁😁👇👇

View: https://www.instagram.com/p/DF-FqdGuhMw/?igsh=MWc1NzdqazZmcnJhNA==
 
Hiyo ni calculation na estimates ,GDP sio hela na kuthaminisha vitu Kwa bei
Kwenye income approach unathaminisha vitu gani ..GDP inajumlisha mapato ya serikali pamoja na halmashauri jumlisha mishahara ya wafanyakazi jumlisha mapato ghafi ya taasisi na kampuni jumlisha makisio ya mapato ya watu binafsi waliojiajiri ndio unapata GDP
 
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imesema Mkoa wa Dar es Salaam ni wa kipekee katika ukusanyaji wa mapato nchini.

Kamishna Mkuu wa TRA, Yusuph Mwenda alisema hayo Dar es Salaam juzi usiku wakati wa hafla ya kuwapa tuzo walipa kodi bora wa mikoa ya kikodi ya Dar es Salaam kwa mwaka 2023/2024.

Mwenda alisema Dar es Salaam ni mkoa wa kipekee kwa kuwa kuna mikoa mitano ya kikodi: Ilala, Temeke, Kinondoni, Tegeta na Kariakoo. “Licha ya kuwa na mikoa mitano ipo Idara ya Forodha na ina mikoa mitatu mikubwa, kuna Kituo cha Huduma Maalumu, Kituo cha Kukusanya Kodi za Mafuta na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ambako tunakusanya kodi,” alisema.

Mwenda alisema sababu hizo na nyinginezo ziliwezesha TRA ikusanye Sh trilioni 16.5 kuanzia Julai hadi Desemba mwaka 2024 na kati ya fedha hizo trilioni 13 zilikusanywa katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Habari Leo

===

MY TAKE

Kitendo cha Nchi kutegemea asilimia 80% ya Mapato Kwa Mkoa mmja wa Dar ni jambo la ajabu na la kushangaza na inaonesha jinsi Nchi Ina uneven distribution of resources. Pia soma Miaka Zaidi ya 60 Baada ya Uhuru,Tanzania Imeshindwa Kuondoa Mizizi ya Ukoloni Kwa Nchi kuwa tegemezi wa Uchumi na Mapato Kwa Jiji Moja tuu la Dar

Hatuwezi kuendelea na utaratibu huu,ni muda muafaka sasa Kwa Serikali kutawanya maendeleo na economic centres kwenye Kila Kanda.

Kwamba Mikoa 25 inakusanya Trilioni 3.5 yaani hata nusu ya Mapato ya Dar hayafiki harafu Walioko kwenye Utawala wanaona sawa Dependency ya hivi Kwa Mkoa mmja Haina Afya kiuchumi na ni hatari sana kiusalama.

Hivi tuna watu wa Mipango kweli? Hivyo Vyuo vyenu vya Planning mnafundisha nini Sasa? Mambo kama haya ndio yanafanya watu waamini mtu mweusi hajatimia kichwani.

Ngoja ije itokee Dar kuwa paralysed siku Moja Kwa tukio.loloye ndipo akili zitawajia maana Mtu mweusi Huwa hajifunzi na hana akili za kesho Hadi apigwe tukio.

Soma hapa zaidi Mikoa 13 Kinara wa Kuchangia Kodi ya TRA mwaka 2023
Issue ya Dar kukusanya hela nyingi ni changa la macho la upuuzi wa TRA. Ukishakuwa na Biashara kubwa file lako linahamishiwa Large Taxpayers Department - ilala haijalishi uko mkoa gani. Migodi yote mikubwa nchini mafile yako ilala na kampuni zingine zote kubwa za mikoa mbali mbali hata billionea Mlokozi file lake lipo TRA - Dar ilala japo kiwanda kiko Babati - Manyara.
 
Trilioni zaidi ya 12 ni Bandari, mtu wa mkoani akitoa mzigo wake Bandari basi unahesabiwa kama ni mapato ya Dar,

Sina uhakika ila sitashangaa pia kampuni kubwa kulipa kodi zao dar hata kama mzigo umeuzwa mkoani.

GDP za mikoa ni indicator nzuri kuliko hii.
Bado ni uzembe kwanini wasiwekeze bandari ya Tanga kuioa nguvu nayo ikaribiane atleast na dar kupunguza mzigo na foleni bandari ya dar?
 
Bado ni uzembe kwanini wasiwekeze bandari ya Tanga kuioa nguvu nayo ikaribiane atleast na dar kupunguza mzigo na foleni bandari ya dar?
Bandari ya Tanga ngumu kuiendeleza, eneo lake ni strategic zaidi (Kivita), sema lipo eneo ambalo inaweza kujengwa Bandari mpya ya maana, Eneo ni natural lenye kina Kirefu. Mwambani.
 
Bado ni uzembe kwanini wasiwekeze bandari ya Tanga kuioa nguvu nayo ikaribiane atleast na dar kupunguza mzigo na foleni bandari ya dar?
Bandari ya Tanga ngumu kuiendeleza, eneo lake ni strategic zaidi (Kivita), sema lipo eneo ambalo inaweza kujengwa Bandari mpya ya maana, Eneo ni natural lenye kina Kirefu. Mwambani.
Hayo hayo maeneo strategic ya kibita ndio wenye akili wanawekeza na kuyalinda kweli kweli.

Pili sio uzembe ni uzezeta wa kushikiliwa akili au muendelezo wa fikra z kikoloni na watu kuwa na akili ndogo.
 
Issue ya Dar kukusanya hela nyingi ni changa la macho la upuuzi wa TRA. Ukishakuwa na Biashara kubwa file lako linahamishiwa Large Taxpayers Department - ilala haijalishi uko mkoa gani. Migodi yote mikubwa nchini mafile yako ilala na kampuni zingine zote kubwa za mikoa mbali mbali hata billionea Mlokozi file lake lipo TRA - Dar ilala japo kiwanda kiko Babati - Manyara.
Sasa mambo kama haya manake nini? TRA wanaweza leta sababu za msingi za kufanya huu ujinga?

By the way ni wachache sana wa hivyo,Kwa sababu hata kama faili.lako limehamishiwa huko Ilala kwani unatoka Geita kuja kufanya malipo Ilala? Si unalipa huko huko tuu ila control namba ndio inasoma ya Ilala.
 
Kwenye income approach unathaminisha vitu gani ..GDP inajumlisha mapato ya serikali pamoja na halmashauri jumlisha mishahara ya wafanyakazi jumlisha mapato ghafi ya taasisi na kampuni jumlisha makisio ya mapato ya watu binafsi waliojiajiri ndio unapata GDP
Hoja ni Mapato directly yaliyokusanywa kutoka sources mbalimbali.

Habari ya GDP ni mada nyingine has nothing to do here
 
Hakuna kitu cha kulaumu hapo , ndio maana utafutaji wa Dar ukitumia akili ni rahisi kupata pesa. Vitu vingi vya kustimulate uchumi viko Dar huu ni ukweli mchungu
Alafu pesa za dar ni za mikoa yote si dar pekee. Ile business center kama hujui. Lakini pia population ya dar ni sawa mega city hivyo factor za kukusanya mapato mengi dar zipo nyingi kuliko ulinganishe na kigoma etc
 
Sasa mambo kama haya manake nini? TRA wanaweza leta sababu za msingi za kufanya huu ujinga?

By the way ni wachache sana wa hivyo,Kwa sababu hata kama faili.lako limehamishiwa huko Ilala kwani unatoka Geita kuja kufanya malipo Ilala? Si unalipa huko huko tuu ila control namba ndio inasoma ya Ilala.
Mkuu File lako lilipo ndio ofisi yako kikodi na ndipo utakapolipia na inaporipotiwa...
 
Hayo hayo maeneo strategic ya kibita ndio wenye akili wanawekeza na kuyalinda kweli kweli.

Pili sio uzembe ni uzezeta wa kushikiliwa akili au muendelezo wa fikra z kikoloni na watu kuwa na akili ndogo.
Kwa Hapo Tanga huwezi kujenga Bandari kubwa, sababu sio Bahari kuu bali ni Ghuba, kuna wakati inabidi meli kubwa ipaki mbali halafu vile vimeli vidogo vipakue na kuleta Bandarini.

Screenshot_20250218_113756_Maps.jpg


Hio bandari ni strategy ya Vita ya wajerumani sababu hilo eneo ni rahisi kujilinda incase mnavamiwa toka Baharini, hio Ras unayoiona Raskazone ndio kuna makambi ya jeshi, Mizinga etc.

Ili upokee Meli kubwa za kisasa kuenda na wakati unahitaji sehemu kubwa kushinda hio
 
Back
Top Bottom