Tetesi: Darasa la saba kufutwa, somo la maadili laanzishwa shule za msingi

Tetesi: Darasa la saba kufutwa, somo la maadili laanzishwa shule za msingi

Badala ya kuongeza darasa la 8 ili yaungane na kidato cha kwanza (la 9). Ila NECTA Wanakata suruali iwe bukta!! Duuh
 
Inawezekana sana kwa sasa lakini waweke msisitizo kwenye elimu ya awali kwa watoto wote.

"Enzi" zetu tulijua kusoma, kuandika na hesabu tukiwa darasa la kwanza na la pili na kiingereza tulianza kujifunza darasa la tatu (na kwa kweli mpaka tunafika la saba baadhi yetu hatukuwa na uwezo wa kufanya meaningful conversation kwa lugha ya kiingereza).

Sasa hivi watoto wetu wadogo tu wa chekechea (miaka 4+) wanahesabu vizuri, wanajua kusoma na kuandika (haya wengine tulijifunza darasa la kwanza na la pili) na wanaongea kiingereza katika level ambayo wengine tuliifikia tukiwa kidato cha kwanza au pili. Kwa hivyo nikitizama yote haya, sioni sababu ya watoto hawa wa sasa kusoma shule ya msingi kwa miaka saba....hakuna sababu!
 
Elimu ya msingi kuishia la sita si mbaya ni hatua nzuri maana itapunguza miaka ya kuwa masomoni na sioni adhari yeyote hapo ila kuhusiana na TEHAMA kufutwa this isn't fair....tuna wanyima wadogo zetu na watoto zetu nafasi nzuri maishani ukizingatia ulimwengu wa sasa ulivyo wahusika walitizame hili kwa umakini..
 
Sio tetesi hiyo.Ni kitu kipo katika maandalizi.
Naunga mkono kufupisha elimu ya msingi.
Ila hiyo elimu ya uraia isije ikawa kufundisha watoto ukada wa CCM.
 
Hiyo ni kweli, na walimu wapo semina nchi nzima wanapata mafunzo ya huo mataala mpya utakao anza mwakani ila utawahusu drs la 1 hadi la nne wa mwakani.
Kiwango cha elimu ya msingi kitakuwa ni darasa la sita.
Kwa miaka yote sita mtoto anatakuwa akikazaniwa
ajue K.K.K.
 
Isije kuwa somo la madili ni kufundisha watoto utii wa serikali bila kuuliza chochote?
na TEHAMA ifutwe dunia hii ya sasa?
 
Nimepata taarifa zisizo rasmi,kama mdau wa elimu Tanzania,kuwa kuna mabadiliko makubwa katika elimu ya msingi yatafanyika hivi karibuni. Mabadiliko hayo yatahusu mitaala,masomo husika na muda wa elimu ya msingi. Kwanza,elimu ya msingi itaishia darasa la sita. Madarasa ya kutahini yatakuwa ni la nne na la sita. Baada ya hapo ni masomo ya sekondari.

Pili,yapo masomo yatakayofutwa na yapo yatakayoanzishwa. Mfano wa masomo yatakayofutwa ni masomo ya Teknolojia,Habari na Mawasiliano (TEHAMA). Mfano wa somo jipya ni lile la Maadili litakalofundishwa pamoja na somo la Uraia. Litaitwa Uraia na Maadili.

Kwa miaka sita ya Shule ya Msingi,ni dhahiri kuwa wanafunzi watafika vyuo vikuu wakiwa bado wadogo. Itakuwaje huko Vyuoni? Dunia inategemea mawasiliano na teknolojia,TEHAMA kwanini isiendelee kuwepo? Nini hasa lengo la mabadiliko haya kwa mustakabali wa taifa letu? Natamani zibaki kuwa tetesi tu


Leta kila kitu na siyo kuchagua unachoona kinafiti na negativity yako ndiyo unaleta hapa, kama unataka mjadala weka hapa hayo mabadiliko yote tuyasome na kutajadili!

Halafu isitoshe elimu ya msingi kuishia darasa la Sita haimaanishi kwamba miaka ya kuingia Chuo kikuuu inapungua bali wanaweza wakaonngeza huwo mmoja Sekondari, ni swala la utaratibu tu, kuna nchi nyingine Elimu ya msingi inaishia darasa la 4 lkn bado mtoto anaingia Chuo Kikuu na miaka kuanzia 19 -21!
 
Somo la maadili lina umuhimu wa pekee, we watafute wanafunzi waliosoma Sekondari ya Loyola ndiyo utajua ninacho maanisha hapa.

TEHAMA ianze kufundishwa Sekondary sio shule ya msingi.
Sijui wanafunzi wa Loyola labda unielezee mwenyewe
Tuchukue viongozi as a sample.Unazani wengi hawakufundishwa au hata kupitia course ya hiyo "maadili", lakini wangapi tunaweza tukasema wana maadili mazuri. Few if not none.
Kwanini TEHAMA isifundishwe shule ya msingi? provide reasons.
 
ama kweli kazi ipo kwann somo la TEHAMA lifutwe jamani na siku hizi teknolojia ndo kila kitu ukitaka kuapply chuo wanakwambia utumie CAS duh
 
Inawezekana sana kwa sasa lakini waweke msisitizo kwenye elimu ya awali kwa watoto wote.

"Enzi" zetu tulijua kusoma, kuandika na hesabu tukiwa darasa la kwanza na la pili na kiingereza tulianza kujifunza darasa la tatu (na kwa kweli mpaka tunafika la saba baadhi yetu hatukuwa na uwezo wa kufanya meaningful conversation kwa lugha ya kiingereza).

Sasa hivi watoto wetu wadogo tu wa chekechea (miaka 4+) wanahesabu vizuri, wanajua kusoma na kuandika (haya wengine tulijifunza darasa la kwanza na la pili) na wanaongea kiingereza katika level ambayo wengine tuliifikia tukiwa kidato cha kwanza au pili. Kwa hivyo nikitizama yote haya, sioni sababu ya watoto hawa wa sasa kusoma shule ya msingi kwa miaka saba....hakuna sababu!
Eti eeee
Haya hongera lakini kaa na ufikiri vizuri tena
 
  • Thanks
Reactions: SMU
utafiti ni muhimu kabla ya kulalamika, au kutoa tamko la kulaani.


tehama imeungwa pamoja na somo la sayansi. itajulikana kwa jina la Sayansi na Teknolojia.
 
Ndalichako ni mzuri, lakini kwa utawala huu atakuja kuwa kituko cha milenia! Atafute ushauri kwa wataalamu wasiojikomba!
suala la kuishia std six lilianzishwa last year utekelezaji wake uliamuliwa uanze kwa darasa la pili la mwaka huu kwa maana ya kua mwaka 2020 wakimaliza std six wanaletwa secondary straight yaani from std one to form four ni primary school education.

Ila mheshimiwa Ndalichako naona ameharaka sana kwa kila kitu!

Pia ilipangwa mwaka huu kuwe na mtihani wa taifa wa darasa la pili ili kuwachuja wasiojua kusoma na kuandika!Ila nimesikia haupo tena na form two necta wanasahihisha walimu wa shule husika!
 
Majungu kutoka kwa wambea wa ufipa at work.

Kila siku mnaleta tetesi kuhusu utawala Wa Magufuli na mambo yao.

Tunaomba mtuletee na tetesi kuhusu kuondolewa uenyekiti mfalme Mbowe
wala hakuna jungu wala funiko ukweli mtupu kasema labda waraka wafute Leo!
 
Nimepata taarifa zisizo rasmi,kama mdau wa elimu Tanzania,kuwa kuna mabadiliko makubwa katika elimu ya msingi yatafanyika hivi karibuni. Mabadiliko hayo yatahusu mitaala,masomo husika na muda wa elimu ya msingi. Kwanza,elimu ya msingi itaishia darasa la sita. Madarasa ya kutahini yatakuwa ni la nne na la sita. Baada ya hapo ni masomo ya sekondari.

Pili,yapo masomo yatakayofutwa na yapo yatakayoanzishwa. Mfano wa masomo yatakayofutwa ni masomo ya Teknolojia,Habari na Mawasiliano (TEHAMA). Mfano wa somo jipya ni lile la Maadili litakalofundishwa pamoja na somo la Uraia. Litaitwa Uraia na Maadili.

Kwa miaka sita ya Shule ya Msingi,ni dhahiri kuwa wanafunzi watafika vyuo vikuu wakiwa bado wadogo. Itakuwaje huko Vyuoni? Dunia inategemea mawasiliano na teknolojia,TEHAMA kwanini isiendelee kuwepo? Nini hasa lengo la mabadiliko haya kwa mustakabali wa taifa letu? Natamani zibaki kuwa tetesi tu
Sisi zamani hatukusoka hiyo TEHAMA tunawezaje kusavivu buana?
 
Najiuliza kulikua na haja gani ya kuifanya elimu iwe bure ilhali serikali sasa inakwepa mzigo wa gharama kwa kupunguza huduma? Ni kweli hiki ndicho watanzania walikihitaji?

Ni kweli watanzania walichoshwa na mzigo wa elimu bora waliyogharamia angalau na kuletewa elimu bure ya bana matumizi isiyo na tija? Mwanafunzi kufanya mitihani miwili tu yakuchapwa kwa mwaka ndicho hiki watanzania walihitaji?

YETU MACHO!!!
Binamu hakuna elimu buree!
Nenda shule ya msingi bunge pale wazazi wanatoa elf kumi za tuition na elf 2 ya mtihani kila ijumaa!

Usanii mtupu ule elimu bure huko mbwinde huko na uswahilini wasikojua maana ya elimu!
 
Hii habari ni ya kweli na inaanza kutekelezwa mwakani.tatzo kuna mwaka 2020 kutakuwa na mitihani miwili wa kuhitimu darasa la saba yaani wale wanaomalizia mtaala wa sasa na wale wanaonza kuhitimu mtaala mpya wa miaka sita mzigo kwa waalimu wa sekondari
 
Elimu ya msingi kuishia la sita si mbaya ni hatua nzuri maana itapunguza miaka ya kuwa masomoni na sioni adhari yeyote hapo ila kuhusiana na TEHAMA kufutwa this isn't fair....tuna wanyima wadogo zetu na watoto zetu nafasi nzuri maishani ukizingatia ulimwengu wa sasa ulivyo wahusika walitizame hili kwa umakini..
Tehama haifundishwi isipokuwa shule chache sana, kwa sababu nadhani zaidi ya 75% ya shule hazina mazingira na vifaa vya kufundisha somo hilo, kwa hiyo wala usicomplain kwa hilo!!
Somo likifundishwa kuanzia sec/sch.no sawa tu!
 
Back
Top Bottom