Darasa Punguza ulevi

Darasa Punguza ulevi

Darassa ni mlevi hata ile ajali walipata wakiwa wamelewa
 
Darassa ni mlevi hata ile ajali walipata wakiwa wamelewa
Sasa nimeelewa halafu kuna maneno aliongea baada ya ajali akisema hawatuwezi ...kweli ilikuwa pombe ile.
 
Kabla hamjafahamu huwa anakunywa bia na analewa sasa mnampangiaje maisha?
Sahivi akikosolewa mnaona kama anaonewa gere, siku akifulia ndio wa kwanza kuwacheka, mtaanza kusema 'alizidi ulevi', 'tulimwambia aache kutumia ngada', kama mnavyowacheka sahv wakina 20% na Mr. Nice
 
Anakunywa na kuvuta mineli hatari. Kuna show flani hapa morogoro club inaitwa downtown alifanya hovyo sana kwasababu ya hayo makitu
Hii show ya club downtown nilikuwa pale MG hotel opposite na hiyo club.. Niliwasikia watu wanasema jamaa yuko bwiiii ameharibu show.. Sikuchukulia serious sana nikajua labda Bahati mbaya tu.. Ila sasa kama kumbe ni tabia yake inabidi ajitathimini upya..

Kuna watu watasema anaonewa gere ila ni watu hao hao watakuwa wakwanza kumcheka siku akipotea..

Nakumbuka siku MDB alipokuwa anamtema kwa mara ya kwanza young dee akasema kinachomponza young dee ni kampani aliyo nayo! Na hiki pia kiko kwa darasa watu wanaomzunguka ni wa hovyo sana.. Kuwa na kipaji ni jambo moja but unahitaji uzungukwe na watu positive wenye kuona mbali..

Binafsi alinidissappoint juzi alivyopata ajali alafu anasema "hawatuwezi"!! Ni utoto wa hali ya juu..

Darasaa ni msanii mzuri but ana mambo mengi sana ya kuyarekebisha ili afike kule anakotaka..
 
Kabla sijacomment habari yoyote huwa naenda all content ya mtu aliyepost..we jamaa ni hater na habari yako imekaa kimipasho..kweli vijana wa muziki wa ujanja ujanja mnapenda fitna...Moshi nzima ubaki weye tu na hearsay zako au club nzima ndani ulikua weye?acha umbeya mtoto wa kiume kumshusha darasa sio kumpandisha diamond
Cjaona chuki yoyote ya mleta uzi. Kuwepo klabu haimaanishi kila aliyekuwepo pale ana access ya JF,au ni lazima aandike huku. Big up mleta uzi!
 
Back
Top Bottom