Dark days 17/03/20...

State ni wahuni wale wale.

Nyerere na wenzake wanastahili lawama, walipokumbali mfumo wa vyama vingi,
Walipaswa kuweka misingi mingine ya chama kisikae madarakani muda wote kimoja,

Wangefanya japo vyama viwili vyenye sera tofauti kupishana madarakani kila baada ya muda fulani,

Hii ikitokea chama fulani kimewekwa kando kiweze kujiafakari wapi kimekosea,

Wao wakaishia tu kuwa na utaratibu wa kiti cha urais mtu akae mihula miwili,
Na eti Nchi hii bila chama cha CCM madhubuti itayumba,

Waliangalia ubinafsi si maslahi mapana ya taifa ya muda mrefu.

Mwl hayupo madarakani, katiba ameiona akitokea rais kichaa anaweza kuitumia vibaya akaonekana ni mungu mtu, wakati Mwl ushawishi kwenye chama bado anao je kitu gani kilimzuia kutengenezwa katiba mpya mwaka ule wa kukubali vyama vingi?
Akaishia kutuma mashushushu waanzishe vyama vya upinzani nchi kwa nje ionekane ina vyama vya upinzani kumbe hamna lolote,
Akina Augustine Lyatoga Mrema, Seif Sharif Hamad, Hamad Rashid, Juma Duni, Mabele Nyaucho Marandu na wengine wengi.
 

Ishu ya Muasisi sijawahi kujua kwa nini aliona hiyo hali ila hakuchukua hatua yoyote ile??

Ila kuna za chini chini sana inasemakana mwana lupaso alimtanguliza muasisi kwan alikuwa kikwazo kufanya mambo yake. Sijajua ukweli wa taarifa hii maana hata humu ilijadiliwa. Huenda kikazwo ni pamoja na uandishi wa kitabu kipya.

Hata NEW CEO alitakiwa kukubali kufanya ubariri wa kitabu lakini ameweka ngumu.

Ukweli ni kwamba mifumo yetu ni mibovu sana. Umaskini wa hali na mali ndio wenye kutudumaza. Kutegua nyaya za chama kikongwe ndio shughuli na atakayefanikiwa nchi itakuwa huru.
 
The MoNA, hata Mm namshangaa Mwl kwa nini swala la kitabu miaka ile ya kukubali vyama vya mbada kwa nini hakupigia upatu kitabu?

na nasikia aliwahi kusema kitabu kilichopo kwa muundo kilivyo kiongozi akikitumia vibaya anaweza kuwa hatari.
Issue ya Mwana lupaso ni yeye peke yake, je lordrings hakuwa miongoni?
Maana kuelekea 2005 alikuwa ni kikwazo Mwl.

Na kama alifanya naona ule msemo usemao ukiua kwa upanga nawe......... Miaka 21 baadaye naye kamfuata.
Kuhusu NEW CEO kutokushughulika na kitabu ndiyo maana nikasema hata DS nao ni wahuni wale wale, km wapo kwa maslahi ya taifa na watu wake walio wengi wanashindwaje kutumia nguvu kufanikisha hili, Je CEO ana nguvu kuwazidi wao au na wao kitabu kipya kikipatikana maslahi yataingia mashaka?
 
Tatizo chama kilichopo ni Dini kubwa ya kikristo!Sasa kuua Imani kuu lazima uanzishe Imani nyingine kwanza ndio Imani mpya ipewe Dola,Sasa hai wengine ni walutheri,wengine Anglicana Sasa hawawezi pewa hadi kuwe na makubaliano maalum ya kiimani Ili kulinda uwekezaji wa dini kubwa uliokwisha fanyika enzi na enzi Hadi leo!!!

Haha mambo Yana Imani ndani yake!
 
Aiseee hatari sana 👇👇👇
 

Attachments

  • FB_IMG_1718013121770.jpg
    98.6 KB · Views: 44
  • FB_IMG_1718013121770.jpg
    98.6 KB · Views: 40
Duuuuuuh, lkn mkuu baada ya kutangulia Mzee wa salamu ya Mambo! Na Maembe ikasikika sehemu fulani kuwa, Wagalatia wasahau kukaa kwenye U CEO je itakuwaje?
 
Si matatizo yangu mimi, ni matatizo ya nchi,
Yeye akiwa miongoni mwa waasisi na akapata hadhi ya kuitwa baba wa Taifa, baadhi ya maeneo aliyokosea yeye na wenzake tunayasema.
 

Nimemsikiliza aliyekuwa mkuu wa majeshi ya wanamaji nchi Marekani, Eric Prince anasema Afrika inabidi kutawaliwa tena kwani wanshindwa kujitawala. Viongozi wao wanatumia fedha nyingi kwenda nje kula raha miji kama Paris. Anasema viongozi kutoka Afrika wanakusanya fedha nyingi badaa ya kusaidia raia wake wanaishia kufanyia anasa, nafikiri wanastahili kutawala tena ili kupunguza wimbi la wahamiaji wengi kutoka Afrika kutokana na ugumu wa maisha.

Kauli nzito itachukuliwa tofauti ila ndani yake kuna ukweli. Afrika viongozi hawana huruma na wananchi wao hata kidogo. Uliyoyasema kuhusu nini nyuma ya kumwaga pesa nyingi simple kukalia kiti ni mwendelezo wa kuficha madudu uliyokuwa ukiyafanya. Lengo kuu ni kuendeleza pale ulipoishi katika kukusanya pesa na kuendelea kula raha. UKITAKA, UKIPATA, UNATAKA TENA.
 

Yes aliwahi kusema hayo. Kuna vile mwenyewe hakutaka kuingilia maamuzi ya waliokuwa madarakani. Alishauri akawaachia wachukue mamlaka. Labda kuna kolabo ilitokea. Ila BM alikuwa powerful sana hadi kimaamuzi sidhani kama alihitaji ushirikiano mkubwa sana labda kwa kiwango kidogo maana mambo kama haya yanahitaji watu wachache sana ili kuweka siri.
 

Sidhani kama dini ipo applicable moja kwa moja mkuu. Kama ni hivyo mibadilishano isingekuwepo mikubwa kuna nyadhifa kubwa tumeona dini ile nyingine imeshika pakubwa hasa kipi cha by gone, msaidizi wake, Mhesabu mkuu, jaji, PM n.k

Japo ukiiweka mtazamo huo unaweza kupata maana. Nafikiri ishu kubwa sio dini kwani hata ukivuka maji majority wa kule sio wa kristo na chama kimejaa wasio wa kristu kwa kule hapo uta apply vipi dini? Ishu kubwa ni kutetea maslahi ya chama kwanza kisha taifa.

Mwinyi sold mbuga
Bm sold madini
JK sold gas and other big deals kajiwekea vipasenti
By gone (may be was on process)
SSH bandari
Calculate dini hapo kisha uangalie.

Its not about dini ni kukipigania chama kwa jasho na damu, ukiwa tayari kufanya hivi umequalify.
 
Hao wasvaa kanzu walianzishiwa chama Chao Chao wavaa kanzu ambao sio halisi,yaani kampuni iliona wavaa kanzu halisi ni threat kwa kampuni ikaanzisha chama Chao Ili ku regulate imani yao!!

Ndio maana kanisa kuu halijawahi kuona wavaa kanzu waliopo kwenye chama kile ni threat Kwa maslahi Yao!

Asili ya nembo ni kanisa kuu!! Na kama wewe ni mvaa kanzu bas uwe member wa chama like Cha wavaa kanzu, protestants na wenye Imani Kali zaidi ya wavaa kanzu hawatakiwi kushika ukuu wa kampuni wanahisi wataharibu mambo!!

Hai wavaa kanzu na hao waseminari wote ni maafisa vipenyo wa kampuni !hata huyo she mkuu unakuta ni sehem ya mfumo!

Swala la wizi na ubadhirifu Kwa wakuu wanoshika ukuu inatokana na hofu ya mstakabali was maisha ya vizazi vyao coz muelekeo wa kampuni hautabiriki na haupo stable!
 

Kwa ufupi ukiwa mtu wa msimamo tofauti na wao umepigwa chini na ikibidi zaidi kuwa eliminated hawasiti kufanya hivyo.

Para ya mwisho ni ubinafsi na njaa kali ndio inatusumbua kampuni hii na viunga vyake mpaka barani kwa ujumla. Tuna hofu ya kukosa mamlaka na fedha, wasio na njaa ni wachache sana na pengine hawapati nafasi za juu kwa sababu wataharibu maslahi yao. Wanaogopa nguvu ikirudi kwa wenye nchi hawatafurahia matunda. Mwl ni mf. Tosha kiongozi wa juu ambaye hakujaa njaa, hayati Moringe ni miongoni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…