Dark days 17/03/20...

Dark days 17/03/20...

Yaani yanaisha muda huo huo na wanawapa moyo wale wa chini kupiga kazi haswaaa, sema siasa wanasiasa wanafanya kudivide na ku rule ,akiahidiwa cheo au zawadi anaweka weledi pembeni.

Ila kiongozi wao akiamua kuwaunganish wote wawe kitu kimoja na asiwaingilie maamuzi yao ya busara na ujuzi walio nao ni taasisi nzuri sana.
Sahihi kabisa. Hawa ndio watu tunawategemea. Kazi zao ni za kutukuka zikifanywa kwa weledi.

Na sisi hatutaki demokrasia ya vurugu. Tunataka demokrasia ya maendeleo. Kwanini iwe Ulaya na Marekani tu?
 
Nashauri serikali ifanye vetting kwenye jeshi la Polisi wanaoingia, wafuatilie historia zao,screening iwe kubwa wasio na uwezo wasipewe nafasi zenye vitengo nyeti unakuta hawa ndio wavujisha siri za raia na kuleta ugomvi mtaani.
Ushauri mzuri sana.
 
Wamo kibao humu utaona wanavyomtukuza na kumpamba utadhani malaika.Watafutwe wasukumizwe kwenye kamkoa kao watuachie kampuni yetu hatujazoea mambo ya maugomvi wala ubaguzi wa kikanda na ukabila, kokote kwenye kampuni yetu mtu unaishi raha mustarehee hakuna anayeuliza wa wapi labda kwa ajili ya utani au akutambulishe na mtu wa kwenu, ila kwenye kubaguana hakuna kitu kama hicho.
Mimi nimzalendo ila wewe jamaa naona umenizidi. Kauli na maneno yako yanathibitisha hivyo. Barikiwa sana.
 
Nadhani kitu kama hicho ila sikumbuki vizuri. Pia inawezekana ndio huyo huyo aliwahi kumpiga mkwara Paka kwamba usipoacha ujinga wako wa kupigana pigana huko ninakufuata nikiwa full.Akatulia.

Sasa huwa ninashangaa eti ana nguvu sana,mara atatupiga, ana jeshi imara sana, hizi propaganda siyo nzuri ifike mahali zife kabisa maana zimeshawaharibu baadhi ya vijana na kumuona shujaa.
Mzee yule yuko vizuri kwenye Propaganda unaona alichoenda kufanya kule Cabo De Ligado? Mtu ambaye hata kampuni yake uko hoi kwa njaa na umaskini eti ndiye anaenda kutoa msaada wa kijeshi😅😅
 
Sahihi kabisa. Hawa ndio watu tunawategemea. Kazi zao ni za kutukuka zikifanywa kwa weledi.

Na sisi hatutaki demokrasia ya vurugu. Tunataka demokrasia ya maendeleo. Kwanini iwe Ulaya na Marekani tu?
Eti bwana tunawatolea mifano mizuri tu wakati tuna mambo tunayaweza vizuri kabisa.

Kuna kipindi askari wa US walikuja kwetu kufanya mazoezi na shindano la kutembea mwendo mrefu huku wakiwa wamebeba mzigo wa kg 50 mgongoni, pia wako full combat huwezi kuamini walioshinda ni wa kampuni yetu.

Kwa utimamu wa mwili wako vizuri sana,ila hizi habari kwa waandishi wetu siyo habari au wanaogopa kuziandika.

Ingekuwa ni kampuni nyingine wangeipaisha sana hii habari. Vyombo vyetu vya ulinzi viwe vinatoa tips fulani fulani ili kuonyesha vipo active lasivyo tutalishwa habari za nje na kuziamini huku tukiona vya kwetu siyo lolote wala chochote.
 
Mimi nimzalendo ila wewe jamaa naona umenizidi. Kauli na maneno yako yanathibitisha hivyo. Barikiwa sana.
Amen sana.Yaani mimi ninavyoipenda nchi yangu siko tayari kuona mtu anataka kutuvuruga eti kwasababu ya upole wetu, utulivu wetu,amani yetu na ukimya wetu.

Somo la Uzalendo lipewe umuhimu sana kwenye mitaala ya elimu yetu. Tukiwa na kizazi chenye utu,ubinadamu na utii kitaifanya jamii yote ibadilike na kupata viongozi sahihi na wenye maono ya kulipeleka Taifa mbele.

Haya ndio yataleta haki katika jamii na kutengeneza nchi yenye maelewano mazuri pasipo misingi ya kubaguana, kuoneana, kudharauliana.Haki haiwezi kutolewa kama jamii haikujengwa katika misingi imara ya uzalendo.
 
Mzee yule yuko vizuri kwenye Propaganda unaona alichoenda kufanya kule Cabo De Ligado? Mtu ambaye hata kampuni yake uko hoi kwa njaa na umaskini eti ndiye anaenda kutoa msaada wa kijeshi[emoji28][emoji28]
Watu wake wanavyoisifu sasa,ohhh! Ni tajiri sana kuliko sisi, halafu jambo la kushangaza kuna watu wanaamini kabisa kwamba wako juu ya kampuni yetu kwa kila kitu, kilichofanyika ni propaganda tu na ikaeleweka [emoji3][emoji3][emoji3]

Na sisi kampuni yetu ianzishe kitengo cha propaganda kuelezea news za namna hii badala ya kushinda tunasoma udaku mitandaoni itasaidia sana kuwaelimisha watu..

Ila isijekuwa kama kile kitengo cha Joseph Goebbells Waziri wa Propaganda wa Hitler aliyeishia kujiua kwa aibu ya kushindwa vita si kwa propaganda aliyokuwa amewalisha Wajerumani [emoji41][emoji41][emoji41][emoji41].
 
Tukiongea hapa watu wanadhani tuna chuki binafsi na Paka how ? Mambo yake siyo, hana uchungu na nchi yetu,hatupendi watanzania, shida yake kubwa ni rasilimali za nchi yetu. Atuongoze kwani sisi hatuwezi kujiongoza, sisi siyo wajinga kiasi hicho.

Mbaya zaidi hata watu wake wana dharau sana akija kwako anataka kukutawala, anakupangia nini cha kufanya, dharau kama zote anaweza kukutemea mate usoni. Ni wachafu hawa watu,wawachunguze vizuri. Sisi tuliowahi kuishi karibu nao ndio tunawajua na hatunaga shobo nao kabisa.
Mungu ambariki sana PK , alimradi atatusaidia kwa sababu yoyote ile kulipa kisasi cha kutuulia kipenzi chetu "the gone" CEO. Kumbu adui wa adui yako ni rafiki mura!
 
Huu ni uongo kabisaa, akat PK ndo alisema shuka analolalia born town analijua, woiiiiiiiih
Ww kamama sikia,hapa nazungumzia baada ya CAT kutamka maneno hayo na vitisho vingi . Kama unavyojua mr born town kalelewa jeshini na si hivyo tu pia alikua kua ni luten kanali wajeshi na kipindi kile alikua anapendwa na bakabaka hatari mpaka sasa mana aliwaboreshia maslahi mengi sana , ndipo iliandaliwa operation maalum mmoja wa makomando kutoka 92 Kj alikwenda mpaka viungani mwa CAT tena ndani Kbsa unajua nn kiliendelea baada ya hapo [emoji23] [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Vitu vingine naogopa kuongea sana nisije nikavuka mstari mwekundu maana dah ulimi uliponza kichwa.

Kuna kamanda amestaafu anaitwa sabuni Toffy ile ya kufulia nguo ,hiyo hiyo mkuu [emoji846]

Huko bwana kuna kipindi kulikuwa na ujambazi sana magari kutekwa tekwa hovyo, askari wananyang'anywa hadi bunduki halafu zinatumika kutupiga sisi wenyewe.

Ukifuatilia unakuta ni watu wanavuka mipaka wanaingia kutoka nje na wanafanya yao,yaani hiyo njia kama mnaianza kuna kibao kinasema "sasa unaanza kuingia pori la..."Kama mlikuwa mnapiga story kila mmoja kimyaaaaa, unawaza sijui nitamaliza salama?

Roho mkononi mwenye kuomba anaanza, tasibihi mkononi, Rozary, wa njia ya msalaba ilimradi kila mmoja anamlilia muumba wake.

Walivyozidi ikabidi wampeleke huyo Kamanda kufanya utalii kwenye mapori yote, yeye mwanzo hakuwa anaenda front anawatuma tu vijana wake.Wakienda na kurudi hawaji na majibu ya uhakika sana maana baada ya muda unasikia tena wapuuzi wameanza tena.(wameteka) na kuua.

Akaona huu ujinga, akaita vijana wake kadhaa akasema kuanzia sasa mimi sikai ofsini tunaenda wote, vijana wanashangaa boss uko serious? Akawaambia twendeni na msiseme tunaenda wapi.

Kabla hawajafika zikaanza kulia,nao wakajibu ila upande wa maharamia ukaonekan una nguvu zaidi. Akaita Landrover kwa simu ya upepo kutoka makao makuu ya mkoa, ikaja iko loaded.

Mkuu tumefika, akawaambia nipishe niwaonyeshe, yeye mwenyewe akapanda juu weeeh, unaambiwa hadi kuku walikuta ni manyoya tu. Salamu zikapelekwa kwa wengine kwamba tulichofanyiwa si kwa akili hizi za hawa jirani zetu tulivyodhani wako, sivyo kumbe, adabu.

Akaendelea kuwajengea uwezo hadi sasa ukisikia ni kwamba aidha wamekufa wakijaribu au walikimbia kuko shwari. Kumbuka huyu alipelekwa huko na born town. Sasa hapa mtu atasemaje jeshi la Polisi ni dhaifu, hatuyajui mengi wanayoyafanya.

Jamani makamanda nimeamua kuongelea mazuri yenu ambayo wananchi hawayajui ndio maana wakati mwingine wanaleta dharau, ila kama mtaona naenda kinyume tafadhali niambieni nifunge kinywa changu.

Nimeongea kwa kifupi sana hilo tukio maana nilisimuliwa ila ni la kweli siku hizi kuko shwari, so Mr born town hawaachi kumlaum na kumlaani kule aliweka intelijensia kali ambayo ilitibua mambo yao mengi.

Utasikia Chi...mbaya sana,hovyo sana, wengi hawawezi kutamka herufi ya jina lake la kwanza.
Dah.. Mkuu hiyo sabuni V.. Ilikuwa ni kiboko ya uchafu na madoa haswaaa..

Alikuwa na kikosi chake cha vishandu ni hatari sana. Watu wana achia usukani wa bike wanapiga njugu na zinaingia halafu mwendo sanaaa.. Kiddon wakasome yani..
 
Kuna kitu kwenye Kampuni nyingi Duniani kinaitwa... To Maintain Public Investment Security...
CEO wa Kampuni Mbalimbali huko mjuu hulinda hii kitu ili UKUSANYE KODI na KUMAINTAIN JOB SECURITY..
Born Town alijitahidi ndio maana angalau Govt na Private Institution ziliajiri...

Alipoingia The so called Late... Alijua Private Institution hazilipi kodi... Akazinyonya balaa... Nguvu ya kuajiri ikaisha....

Yeye alijua tuu... Kamua tuu.... Na baadhi ya watu.. Nenda Benki angalia ana salio lipi.... Kamuaaaa...

Mwisho wa siku... Kila Big Companies zikapunguza wafanyakazi... Pia Jobs zikawa shida.. Sanaaa...

Washikadau flani flani wakaondoka wakaenda njeeee kabisa... Maana wangefilisika....

Kuwa na M 500 Benki sio kosa kama unaweza kuonyesha umepataje.. Kwa kazi zipi kihalali...

...kuna watu wanaingiza 20 M kwa mwezi na kodi analipa.... Je hawezi kuwa na 500 M benki...? Basi hawa wengi waliumizwa... Huku mzilankende akijua anajenga kampuni.... Kumbe ndio anaua employment industry..

Anyway tumetoka mbali...
Sure kabisa mzilanKENDE alikuwa mshamba tu
 
Mungu ambariki sana PK , alimradi atatusaidia kwa sababu yoyote ile kulipa kisasi cha kutuulia kipenzi chetu "the gone" CEO. Kumbu adui wa adui yako ni rafiki mura!
Duh! Mzee we noma,ni mawazo yako lakini, kama ambavyo na mimi nilikuwa ninatoa ya kwangu.Fita ni fita mura. Siipendi fita mie we acha tu.
 
Ww kamama sikia,hapa nazungumzia baada ya CAT kutamka maneno hayo na vitisho vingi . Kama unavyojua mr born town kalelewa jeshini na si hivyo tu pia alikua kua ni luten kanali wajeshi na kipindi kile alikua anapendwa na bakabaka hatari mpaka sasa mana aliwaboreshia maslahi mengi sana , ndipo iliandaliwa operation maalum mmoja wa makomando kutoka 92 Kj alikwenda mpaka viungani mwa CAT tena ndani Kbsa unajua nn kiliendelea baada ya hapo [emoji23] [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Shida ilijitokeza hapa kwenye kampuni yetu nikuacha kuongelea mambo yetu mazuri na kuongelea siasa tu. Sasa yeye alijua ya upande mmoja baada ya kumsikia akiongea au jinsi yalivyosambazwa hayo maneno na hao hao, ndio maana hataki kuamini.

Nilivyoongelea mboga na ugali nilikuwa ninamaanisha hiki ulichokisema japo wewe unaonekana unakijua zaidi kuliko mimi ungeelezea kwa undani kidogo.

Kuna baadhi ya taarifa hazitakiwi kufichwa sana maana watu wataona hizi taasisi hazipo na kuanza kushabikia za jirani. Kumbe wapo wanakufikia popote ulipo.
 
Mungu ambariki sana PK , alimradi atatusaidia kwa sababu yoyote ile kulipa kisasi cha kutuulia kipenzi chetu "the gone" CEO. Kumbu adui wa adui yako ni rafiki mura!
Pk huyu huyu anayenuka damu ama? Rutamzalisha vifaranga vya kuku... tumlee wenyewe halafu atushindwe?

Sent from my SM-G960U using JamiiForums mobile app
 
Dah.. Mkuu hiyo sabuni V.. Ilikuwa ni kiboko ya uchafu na madoa haswaaa..

Alikuwa na kikosi chake cha vishandu ni hatari sana. Watu wana achia usukani wa bike wanapiga njugu na zinaingia halafu mwendo sanaaa.. Kiddon wakasome yani..
Ahsante sana mkuu. Hapo kwenye uskani wa bike sasa,zinaachiwa halafu baada ya muda unasikia kimya hata ndege na wadudu wapiga miluzi porini kimyaaaaa!

Unaambiwa wakifika kwenye tukio utadhani Bucha. Huyu alikuwa noma mzee, alifanya kazi ya kutukuka huko.
 
Ahsante sana mkuu. Hapo kwenye uskani wa bike sasa,zinaachiwa halafu baada ya muda unasikia kimya hata ndege na wadudu wapiga miluzi porini kimyaaaaa!

Unaambiwa wakifika kwenye tukio utadhani Bucha. Huyu alikuwa noma mzee, alifanya kazi ya kutukuka huko.
Nyakanazi - Lusahunga - Biharamulo - Bukoba hadi Mutukula

Unapita muda wowote sasa hivi

V T alipaweka shwari kabisa
 
Back
Top Bottom