Ametaja kuanzia 1 Aprili, 2024 wakati tarehe hiyo ni siku ya waongo duniani.
Huyo nabii wa kwenye channel ya Unyakuo TV amewahi kutoa unabii upi kwa taifa na ukatimia?
Ntapandisha Uzi nijaribu kuelezea kuhusu Nyikani Kwa kirefu, labda utaelewa,
Kwa kifupi, Israeli halisi Si Ile ya Mashariki ya kati. Nyikani ndiyo Israel halisi ya Rohoni.
Waisraeli halisi Wana wa Ibrahimu Kwa Imani ni walokole, waliookoka, WATAKATIFU walioko duniani.
Ukristo ulioenzwa Kwa mfumo wa Dini kupitia waroma ni WA mchongo.
Waisraeli halisi walitawanyika Dunia nzima baada ya mateso Yale Kwa Kanisa la kwanza,
2023 na kuendelea, mateso hayo hayo, yakichagizwa na majanga yatalikusanya tena Kanisa.
Mahali salama Dunia nzima patakuwa hapa Nyikani,
Ndipo sasa ujue, Mungu anaandaa Nchi hii Kwa ajili ya kupokea watakatifu wake.
Atainuka Mtawala atakayeandaa jambo Hilo kubwa na atakuwa Mlawi. Hayo yatatukia wakati DHIKI Ile ya Mathayo 24 ikiendelea.
Nia Hasa ya mapigo hayo ya may 2024, ni wote wastuke na kusikia maelekezo juu ya nini Cha kufanyika.
Kukusanywa Kwa Kanisa halisi ni kuwatoa wote Kutoka katika dini zao na warudi kuabudu Kwa UMOJA, na kusanyiko kuu litakuwa siku ya sabato,kama ilivyo Kwa Wayahudi hata sasa.
IBADA itakuwa moja. Na wengi watakuja hapa, Mahali salama.
Wakati huo Wayahudi, Russia,waarabu na mataifa mengine yatakuwa yakipigana vita kugombea hekalu ya Suleiman,
Mpinga kristo ndo atawajengea na wataungana kuabudu siku moja ya jumapili.
Ndipo wote wataompinga Dunia nzima watakimbilia hapa Nyikani.
Ndipo tunapoelekea.
Ull surely see!!!