DART yawasimamisha kazi Maafisa wa Mwendokasi walioshindwa kudhibiti vurugu zilizotokea Kituo cha Kivukoni

DART yawasimamisha kazi Maafisa wa Mwendokasi walioshindwa kudhibiti vurugu zilizotokea Kituo cha Kivukoni

Msisahau na gerezani pale maana wanasubiria mpaka tujae ndo waje watubebe ilihali madereva wapo wanapiga stori
 
Kwani basi zisibadilishe root kulingana na mahitaji..yaani haiingii akilini basi zinasubiria abiria wa Morocco wakati abiria wa Kimara wamejazana hapo zaidi ya saa zima. Madereva pia huenda siyo kosa Lao maana wao wamepangiwa nenda huku nenda kule. Hawajiamuliii pa kwemda. Hao maofisa ndo hopeless
Sio hivyo tu, kuna wakati gari inaondoka tupu, eti analipeleka yadi shift yake imekwisha....
 
Gari za Kimara ni chache kuliko idadi ya abiria waliopo, unaweza kufika kituoni ukasimama (Maana sehemu za kukaa ni chache) hadi dk30-saa1 na Morocco zinakwenda gari nyingi kuliko idadi ya abiria.

Wakazi wa Kimara wanapitia wakati mgumu sana.
Dakika 30? unabahati wewe, watu wanakaa masaa 2.
 
Hizi Mwendokasi safari zake hazikupangwa kutokana na mahitaji. Wamenakili vituo vya daladala na wao wakapita humohumo. Ingekuwa suluhisho kama wangenakili vituo vya kuanzia au kuishia au kugeuzia vilivyotumika kabla daladala hazijapakwa mikanda ya njia.
Mfano huku kwetu Dar Barabara ya Nyerere, kuna daladala zilikuwa zinaanzia/zinaishia/zinageukia Vingunguti, Uwanja wa Ndege, Banana, Mombasa na Gongo la Mboto. Hizi terminal za kuanzia/kuishia/kugeukia ndizo zilipaswa kutambulishwa kwenye Mwendokasi. Nina maana Mwendokasi zilipaswa kuanzia/kuishia/kugeukia vituo hivyo nilivyotaja. Kusingekuwa na vurugu vituoni
 
Back
Top Bottom