Daudi Ballali's Death

Status
Not open for further replies.

toka jamaa aingie madarakani life imekuwa kama hizi soap/ michezo ya kwenye TV, sijui tumefika episode ya ngapi, naona mpaka 2010 kuna soap kama 5 hivi

wabunge wanajitayarisha kwa mkakati mzito

Je Rostam na Lowassa, watafanya nini kulipa kisasi?

Membe anatafuta nini hasa?

Je urafiki mpya wa muungwana na membe utadumu?

2010 kutakuwa na amani kweli?

Executive Producer Jakaya Kikwete

DUH!!! BONGE LA SINEMA YANI.............

Hovyo kabisa...................
 
Ikulu bado hawajasema chochote mpaka sasa?! Kigugumizi cha nini? Si ameshakufa? Au wanawasiwasi atafufuka...au nao wanataka uthibitisho usiopingika kuwa Ballali ameshafariki?
 
Jamani Balali alifariki siku ya Ijumaa tarehe 16; ibada ya mazishi ni siku ya Ijumaa saa nne hapo Washington DC.
 
Nataka niamini kuwa Balali kafariki. Lakini je, mazingira ya utawala bora wa kutujuza habari muhimu kama hii kwa taifa iko wapi? Nina wasiwasi na umakini wa serikali inayotawala sasa Tanzania na pia washauri wa Rais.
Wanadhani kwa kufanya mambo kichini chini namna hii ndo wamefaulu? Na wamekubali kimsingi kabisa kuwa damu yake na iwe juu ya vichwa vyetu?
 

Nakubaliana nawe. Jamaa na washkaji zake wote wamezidi kuchemka. Wanajifanya hawaelewi kwamba ushkaji hauwi applied kila sehemu. Madhara yake walishaanza kuyaona siku nyingi zilizopita ila kwa kiburi yao hawataki kujirekebisha. IKO SIKU!!!!!
 
Conspiracy theories zinaweza kutuambia mambo yafuatayo:

Kama ni kweli amekufa na hajabadilisha identity..basi
a) alikufa siku nyingi na kwa namna moja au nyingine Serikali itakuwa inajua na kwamba hizi sio breaking news kwao. Kwa nini hatuambiwi medical examination report ambayo huwa inatolewa kwa public..kama alikufa Ijumaa iliyopita, na leo ni Jumatano, almost siku tano zilizopita, lazima taarifa ya dakatri aliye examine body iwe imeshatoka. Je ni hospitali gani?
b) kama atazikwa Marekani na sio Tanzania (na kwa nini azikwe haraka haraka), basi huyu alishakuwa creameted (kuchomwa) ili kupoteza ushahidi ambao especially makachero wetu na DNA analysts wa Tanzania watashindwa kuupata juu ya causes za death.
 
Jamani Mwanakijiji huyu jamaa AMEJIUA au kafa kwa ugonjwa
Inaonekana ni SIRI hadi watu walio huko US hawafahamu
 
Jamani Balali alifariki siku ya Ijumaa tarehe 16; ibada ya mazishi ni siku ya Ijumaa saa nne hapo Washington DC.

Sina shaka na habari za mwanakijiji na hata Tanzania Daima. Maswali magumu ni kwa nini SIRIKALI ya Tanzania inashikwa kigugumizi kusema lolote tangu kufariki kwake ijumaa ya 16.05.08?

Well, hata wakisema amepoteza ushahidi, historia inabaki kuwaandama kuwa yeye Balali hakutumia vema nafasi yake ya dhamana, Rais Mkapa na mawaziri wake wote na sasa Rais Kikwete na washikaji zake pia hawajatumia hekima/nguvu ya sheria katika kukabiliana na hali halisi ya ufisadi. Na kwa kiasi kikubwa ni kwa sababu fedha za EPA zinawazunguka wote walioko matawi ya juu..nadhani Tanzania ya 2010 na hasa kwenye uchaguzi mkuu ina sura tofauti na miaka yote na itashuhudia mabadiliko makubwa ya chama tawala.
 

Msee FMES,
mkuu, mie naishi Boston in the state of Massachussetts.....Ballali ndio alikuwa hapa, habari zake zilikuwa limited sana na ilikuwa mpaka uende kwenye cycles flani flani ndio unasikia hili au lile!!
Kuna kitu inaitwa HIPAA, championed by Ted Kennedy...infos za mgonjwa ni siri kubwa na si kweli kwamba unaweza kuzipata kiholela ktk internet!! sheria hii ni 'biggy' hasa hapa Massachussetts( naongea hivyo nikiwa kama mfanyakazi na mwanafunzi ktk hii system)..mtu akifa hiyo ni story nyingine.

Hashimu akai Boston, jamaa anaishi on Campus kule Storrs, Connecticut na nina uhakika kwamba hana time na mambo hii!!
 
Hakuna mwanasheria mwenye huo ujasiri TZ. Kama yeye alishindwa kujitutumua tena akiwa nje ya nchi, itawezekanaje mwanasheria wake aweze? Tena mwanasheria, kuna watu waoga kuwashinda wanasheria?

Nilimsoma na kumwelewa Invisible tangu alipoleta hizi habari mapema leo..Hakuna uwezekano mwingine wa hiyo dossier kufunuliwa isipokuwa kupitia hapa ukumbini JF. Na uwezekano mkubwa ni kwamba hao makachero na watu wao hawatalala kuanzia sasa, watafuatilia kwa karibu kabisa yanayojiri hapa JF ikiwemo possibility ya kuihujumu JF
 

Mkuu ndio maana nimesema hiyo medical examination report ambayo ninaamini kama alikufa on Friday wiki iliyopita, lazima imeshatoka...na huwa inakuwa public.
 

Well said. Hakuna mwanasheria machachari yeyote wa Tanzania atakayethubutu kusema ambacho Balali alikuwa akiseme! Japo wabunge wetu wakiendeleza mshikamano, twaweza ambulia ambulia masazo ya fedha za EPA, lakini kamwe serikali ya Kikwete haitawaweka hadharani waliokwiba fedha hizo!

Tuombe kuwa CCM igawanyike 2010, upinzani upitishe mgombea urais anayekubalika kwa wananchi ili tugeuze historia ya nchii..hapo walau kuna nuru kuwa Mkapa, Mramba, Mgonja, na washikaji zao watafikishwa mbele ya haki kwa kuifilisi Tanzania.
Ningeliweza kuwa jaji wakati huo, ningemhukumu Balali hata akishakuwa marehemu miaka 10 ilopita.
 
Ikulu yathibitisha kifo cha Balali
Shadrack Sagati
Daily News; Wednesday,May 21, 2008 @17:01

Ikulu imekiri kupokea taarifa za kifo cha aliyekuwa gavana wa Benki Kuu (BoT), Daudi Ballali. "Rais amesikitishwa na taarifa hizo za kifo cha Ballali, tunaandaa rambirambi tutazituma baadaye," alisema mwandishi habari msaidizi wa Rais, Premi Kibanga.

Hata hivyo, Premi alisema Ikulu haiwezi kutoa taarifa za kifo hicho badala yake wenye jukumu la kufanya hivyo ni ndugu zake marehemu, "Ikulu haihusiki na kutoa taarifa tafuteni ndugu zake waseme habari za hicho kifo."

Habari nyingine kutoka katika ofisi za Benki Kuu ambako Ballali hadi anaondoka kwenda kutibiwa alikuwa mtumishi wa taasisi hiyo, zilithibitisha kutokea kwa kifo hicho. Ofisa Habari wa BoT, Emmanuel Mwero alisema walipokea taarifa za kifo hicho kutoka kwa mke wa Ballali, Anna Muganda.

Mwero alisema Anna ametuma ujumbe kwa wafanyakazi wa BoT usiku wa kuamkia leo akiwajulisha kuwa mume wake alifariki dunia Ijumaa iliyopita mjini Boston, Marekani. "Ni kweli tumepokea ujumbe kutoka kwa mke wake kututaarifu kifo cha mzee Ballali," alisema Mwero.

Hata hivyo, hakutaka kuzungumzia kwa undani suala hilo akisema kuwa ujumbe uliotumwa hapo ni kwa ajili ya wafanyakazi kujulishwa kwa vile waliwahi kufanya naye kazi. "Unajua Ballali siyo tena mfanyakazi wa BoT, kwa hiyo kutoa taarifa rasmi itakuwa ni vigumu," alisema ofisa huyo.

Tetesi za kifo cha Ballali zilianza kuvuma tangu Jumapili iliyopita kupitia katika mtandao wa Jamiiforums. "Ballali hatunaye tena," ulikuwa ujumbe uliotawala katika tovuti hiyo tangu Jumapili huku wasomaji wengine wa mtandao huku wakihoji ukweli juu ya taarifa hizo.

Hata hivyo ilikuwa vigumu kuthibitisha habari hizo kutokana na usiri uliogubika kifo hicho. Hata Ikulu Dar es Salaam leo haikuwa tayari kusema ni lini imepokea taarifa hizo za kifo cha Ballali. Hadi jana hakuna ndugu ambaye alitoa taarifa za kifo hicho.

Nyumbani kwa Ballali mtaa wa Mahandu kitalu namba 347 Masaki, Dar es Salaam hakukuwa na dalili zozote za msiba. Gazeti hili lilifika nyumbani hapo na kumkuta kijana aliyejitambulisha kwa jina la Hassan, akieleza kuwa hajui chochote juu ya kifo cha bosi wake.

"Mimi kwa kweli sijui lolote, ni vyema mwende kule alikokuwa anafanyia kazi wanaweza kuwa na taarifa rasmi," alisema Hassan na kuongeza kuwa yupo peke yake na mlinzi na hakukuwa na mtu mwingine ndani.

Mama yake Ballali ameelezwa kuwa anaishi Boko, lakini gazeti hili lilishindwa kufahamu nyumbani anakokaa. Lakini baadhi ya watu wanaamini kuwa yawezekana pia hakuwa na taarifa juu ya kifo cha mwanawe.

Rais Kikwete alitengua uteuzi wa Ballali Januari 9 mwaka huu baada ya kampuni ya ukaguzi wa hesabu ya Ernst & Young kugundua Sh bilioni 133 kuchotwa kutoka katika akaunti ya madeni ya nje (EPA) iliyoko BoT.

Ufisadi huo ulifanywa na watu mbalimbali kupitia kampuni 22 ambazo zilitumia nyaraka za bandia kuchota mabilioni hayo ya fedha. Baada ya kumtimua Ballali, Rais aliunda tume iliyoko chini ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kufanya uchunguzi wa tuhuma hizo na wote wanaohusika wakamatwe na wachukuliwe katika vyombo vya sheria.

Kabla ya Ballali kutimuliwa aliondoka nchini kwenda Marekani ambako ilielezwa alikwenda kwa ajili ya kuchunguzwa afya yake baada ya kudorora kwa muda mrefu. Hali hiyo ya afya iliwafanya hata ndugu zake kutoa malalamiko kuwa yawezekana alikuwa amelishwa sumu.

Akiwa huko aliwahi kuomba ajiuzulu kutokana na matatizo ya afya, lakini Ikulu ilikataa ombi hilo hadi kusubiri ripoti ya EPA ambayo ilimkasirisha Rais Kikwete hadi akaamua kumtimua kazi.

Wakati Ballali akiwa amelazwa Marekani, Gavana wa sasa wa BoT, Benno Ndulu alikiri walikuwa wanamlipia nusu ya matibabu kwa vile aliondoka nchini akiwa mtumishi wa benki hiyo. Hata hivyo Profesa Ndulu hakuwahi kutaja hospitali ambako Ballali alikuwa amelazwa na hadi kifo chake hakuna taarifa rasmi ya kulazwa kwake hospitalini.

Amekufa zikiwa zimebaki siku chache tume ya Rais ikamilishe kazi ya uchunguzi wa ufisadi uliofanywa kupitia akaunti ya EPA. Wasifu wa Ballali unaonyesha kuwa wakati wa uhai wake aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali ndani na nje ya nchi.

Mwaka 1967-1976 alikuwa mtumishi katika BoT na alishika nyadhifa mbalimbali. Mwaka 1979 -1984 alifanya kazi Ghana akiwa mtumishi wa Shirika la Fedha Duniani (IMF) kama mchumi. Mwaka 1984-1986 akiwa IMF alihamishiwa Zimbabwe katika nafasi hiyo ya mchumi.

1986-1997 aliongoza timu ya IMF kwa ajili ya majadiliano na usimamizi wa sera ya mageuzi ya uchumi. 1997-1998 aliteuliwa kuwa mshauri wa Rais wa mambo ya uchumi na mwaka 1998 aliteuliwa kuwa Gavana wa BoT, wadhifa aliodumu nao hadi Januari mwaka huu.

Lakini wakati akiwa gavana, IMF ilimteua tena mwaka 2006-2008 kuwa mjumbe wa bodi za magavana akitokea Tanzania. Pia mwaka 2006 alikuwa mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Mapato (TRA).
 

Mkuu,

Je mtu akifa inakuwaje? Hapa issue sio kuumwa na badala yake ni kifo, je sheria inasemaje?

Kama info inaweza kupatikana, basi tusaidie kututafutia hapo, tujue kama tumefungwa magoli na tujiandae kuzika gogo.
 
Nae si ajabu ni mgonjwa mahututi anavuta pumzi zake za mwisho kabla umauti haujamfika. Machale yamenicheza mkuu, Ballali kifo chake kina utata mkubwa kama walifikiri tutaamini kirahisi kwamba Ballali kafariki basi wameula wachuya.

Eee bwana ikitokea hii habari sio kweli mimi nitajifungisha kwa muda uanachama wangu hapa JF.
 
Nachosubiri kusikia kutoka kwa mtu fulani ni kuwa "alikuwa mtendaji mzuri alikumbwa na bahati mbaya tu kazini. NI lazima tumkumbuke kwa mazuri hakufanya mabaya tu alifanya mazuri pia, tunasikitika tumepoteza mtanzania mahiri" tusubiri tu.
Lakini najua kuwa kuna watu watakaofurahi sana kutokana na kifo cha huyu ndugu. Toka mwanzo mimi nimekuwa nasita kumtwisha lawama zote huyu ndugu Balali, kama angekuwa fisadi asingekuwa na haja ya kukimbia nchi, maana mapapa yenyewe bado yako nchini, vijisamaki na vidagaa ndio vimekimbia. Binafsi nasikitika huyu Mtanzania amekufa, kama ameandaa ushahidi kwenye record, ni vizuri ukawekwa wazi ili usijedakwa, i am starting to worry kuwa hao walosema wanaenda US kumsaka walienda kusaka vitu vingine, since they knew that he was dead already, so there was something else they were lookin for. I ma very much interested in knowing ni mheshimiwa gani aliempa sumu kule Dodoma, i hope we will know that sooner than later.
 
Mkuu ndio maana nimesema hiyo medical examination report ambayo ninaamini kama alikufa on Friday wiki iliyopita, lazima imeshatoka...na huwa inakuwa public.

sio lazima!? kama family ikiomba privacy inapewa unless authorities ziwe zina-suspect foul play ndio lazima infos hizi zitakwenda public!!! haipo eazy kihivyo......
 

Afariki Ijumaa, mpaka Jumanne hata nyumbani kwake hakuna hata dalili ya msiba? Mimi jamani siamini hili, hapa tunadanganywa.

Jiandaeni kutoa rambirambi kwenye gogo.

Huyu mkewe ana nguvu ya kutoa taarifa Ikulu na BOT lakini hakuna taarifa hata kwa familia yake Iringa.

Jamani nisaidieni, ni mimi tu ambaye naona kuna mambo sio sawa?

Mkuu ES, mimi nakubaliana na data zako, hapa tunadanganywa.
 
ni uwongo mtupu, hajafa...walikuja kumsaidia ahame, passport mpya, new life...mtaoenda kwenye msiba tuambie kama ni open casket (si mkristu au?)...Usanii mtupu.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…