David Kafulila anakumbukwa na wakulima wa Simiyu kwa kupaisha bei ya Pamba kufikia Tsh. 2200 kwa kilo katika historia ya Taifa letu alipokuwa RC

Sasa Kafulila huyu alieachwa na Mbunge kisa kufulia anahela gani ya kulipa mtu
🀣🀣🀣
 
Mama ametufikia Kafulila ametufikia,
 
Uzalendo unalipa sana hawa vijana akina Makonda, Kafulila, Mwigulu, Bashe, January wanabebwa kwa Uzalendo wao.
Kwa hakika Uzalendo ndio silaha yao kikuu ya kuendelea kuwepo katika vinywa na midomo ya watanzania.
 
Huyu mshenzi atakuwa anawalipa sana hawa wapuuzi waje wamsifie sifie humu.
Acha wivu wako hapa wewe. Mchapa kazi na mzalendo ni lazima apate wa kumuunga mkono kama ilivyokuwa kwa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kuungwa mkono na watanzania mpaka leo hii. Mheshimiwa Kafulila ni mzalendo anayestahili kabisa kuendelea kuungwa mkono na mamilioni ya watanzania.
 
Hata mimi naliona hilo. Kuna kampeni za kuwasifia watu katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi Mkuu mwakani. Hili jambo si sawa. Subirini wakati ukifika anzeni masifu.
 
Ngoja Nikufumbue tu akili yako hiyo . Ni kuwa ningependa kukwambia ya kuwa 70% ya pamba yote unayoiona hapa Tanzania inatokea Mkoani Simiyu.
Kwahiyo Kafulila ndo kakulisha maneno hayo? Hiyo ni takwimu kabla Mkoa wa Shinyanga haujagawanywa na kuzaliwa Mkoa wa Simiyu.

Ningekuelewa kama ungezungumzia Uzalishaji Mkubwa wa Pamba unatoka Simiyu, lakini eti Bei ya pamba anahusika Kafulila hapana hapana!! Tunalo Soko la Dunia na kama nchi tunayo Bodi ya Pamba. Pitia Sheria ya Bodi ya Pamba ujielimishe na kumuelimisha huyo Muha
 
Unajua mamlaka aliyonayo Mkuu wa Mkoa?
Mkuu wa Mkoa ni Rais wa Mkoa,
Sasa kama Pamba ilitoka kuuzwa TZS 800 hadi 2,200 na Leo hayupo bei ni 1,000 why tusiamini Kuna uhuni kule wakulima wanafanyiwa?
Hilo neno Rais wa Mkoa ndo linakufanya uamini huo uongo!??

Ulivyotaja tu eti Mkuu wa Mkoa ni Rais wa Mkoa naladhamika kusitisha kukuelimisha. Utakuwa na upeo mdogo mno
 
Hilo neno Rais wa Mkoa ndo linakufanya uamini huo uongo!??

Ulivyotaja tu eti Mkuu wa Mkoa ni Rais wa Mkoa naladhamika kusitisha kukuelimisha. Utakuwa na upeo mdogo mno
Kwani kwa akili yako unafikiri ni nani aliye muwakishi wa Rais katika mkoa? Mkuu wa mkoa ndiye Rais wa Mkoa.
 
Wananchi wabubujikwa na machozi!
 
mkuu umehamia kwa kafulila...naona makonda hajapokea simu wala kukupigia.... πŸ˜€ πŸ˜€ πŸ˜€ πŸ˜€ πŸ˜€
 
mkuu umehamia kwa kafulila...naona makonda hajapokea simu wala kukupigia.... πŸ˜€ πŸ˜€ πŸ˜€ πŸ˜€ πŸ˜€
Mimi ni mtetezi wa wazalendo.sisiti wala sioni haya wala aibu kuwaunga mkono WAZALENDO aina ya Mheshimiwa CHUMA Mwenyewe David Kafulila. Naomba tuendelee kuwaunga mkono na kuwatia moyo watu kama MheshimiwaKafulila
 

Duuuh kumbe hata anavyoandikaga kumuhusu Rais Samia ni Rais Samia anamlisha hayo maneno?

Kwa taarifa tu hiyo ni kazi ya Kila mwanachama wa CCM tena hupewi hata mia.

Lucas Mwashambwa yeye ametoa sababu kwanini anavutiwa na Kafulila,

Wewe kama unasababu ambazo unaamini sifa anazopewa Kafulila ni za uongo pia zilete hapa,

Ila Mimi kwa kuwa niko field acha nikusaidie kidogo.

πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

Kafulila alianzisha kitu kinaitwa "Simiyu model" .

Nia ya hii Model ni kutaka Ushirika kushindana na watu binafsi katika ununuzi wa Pamba.

Lakini pia Kafulila alianzisha kamati za pamba kudhibiti Kila hujuma ya walanguzi wa Pamba.

Matokeo ndio hayo bei ikafika mpaka 2200 wakati miaka yote bei ya pamba haijawahi kuzidi 1,200 kwa mkulima.

Ndio Wapo watu kama wewe mnaoweza kusema sababu ni kupanda kwa bei ya pamba katika soko la dunia dine,

Ukweli ni kwamba haukuwa mwaka wa kwanza bei kupanda katika soko la dunia na bado bei haikuzidi 1200/.

Mfano wa miaka ambayo Pamba ilipanda sana katika Soko la dunia ni Mwaka 2011, 2012, 2018 katika miaka hii bei ya pamba katika soko la dunia ilipanda na bado mkulima hakupata zaidi ya 1200/=.

Sasa huyu Kafulila alidhibiti chain ya wapigaji eneo la pamba ndani ya Mkoa mpaka kwenye mfumo wa wanunuzi.

Mimi naombeni watu wakafanye utafiti alichofanya Kafulila na kilichotokea kwenye bei ya pamba ili kitumike kama mwongozo wa Serikali Kwa manufaa ya Sasa na kizazi kijacho.

Ukiongea na wazee wa pamba hapa Simiyu au mchambuzi wa miaka kama Mzee Joseph Mihangwa watakwambia yule kijana alikata mtandao wote wanaokula jasho la mkulima wa pamba.

Tunaweza kuzungumza mengi lakini Kafulila bado ni mtu mwenye uthubutu na ujasiri mkubwa wa kiuongozi.

Soma hii pia itakusaidia,
πŸ‘‡πŸ‘‡

 
Hata mimi naliona hilo. Kuna kampeni za kuwasifia watu katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi Mkuu mwakani. Hili jambo si sawa. Subirini wakati ukifika anzeni masifu.
Hata wewe kama ni mzalendo na mchapakazi utasifiwa na kupongezwa bure kabisa na watanzania. Lakini kama wewe ni fisadi ,mla rushwa basi usitegemee kuungwa mkono na mtu yeyote humu jukwaani. Na hata ukija mwenyewe kujipa promo utaona watu watakavyo kushambuliwa kwa nguvu.maana watanzania wanataka mtu safi , mzalendo na makini aina ya Mheshimiwa David Kafulila.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…