David Kafulila anakumbukwa na wakulima wa Simiyu kwa kupaisha bei ya Pamba kufikia Tsh. 2200 kwa kilo katika historia ya Taifa letu alipokuwa RC

David Kafulila anakumbukwa na wakulima wa Simiyu kwa kupaisha bei ya Pamba kufikia Tsh. 2200 kwa kilo katika historia ya Taifa letu alipokuwa RC

Kafulila ni mwizi tu.
Kafulila angeacha kuendekeza tumbo huenda angefika mbali na kuheshimiwa, lakini pale ni tumbo tu linamtesa. Kajamaa ni kajinga halafu kana tamaa balaa.
Ni lazima UFE na wivu wako pamoja na chuki yako binafsi kwa Mhessimiwa David Kafulila. Ungekuwa na akili ungeweka huo ushahidi wako wa maneno yako ya kijinga ambayo hakuna mtanzania mwenye akili Timamu anayeweza kukusikiliza na kubali. Kwa kuwa kila mtu anafahamu uzalendo na usafi wa Mhessimiwa Kafulila.
 
Kafulila ni mwizi tu.
Kafulila angeacha kuendekeza tumbo huenda angefika mbali na kuheshimiwa, lakini pale ni tumbo tu linamtesa. Kajamaa ni kajinga halafu kana tamaa balaa.
Sijui kama ni kweli,
Nimesoma Kafulila alikataaga 2.8bl
Sasa yaani mtu akatae 2.8bl za bila ushahidi aje aibe zenye ushahidi nahisi mkuu akili yako inashida kidogo
 
Sijui kama ni kweli,
Nimesoma Kafulila alikataaga 2.8bl
Sasa yaani mtu akatae 2.8bl za bila ushahidi aje aibe zenye ushahidi nahisi mkuu akili yako inashida kidogo
Umeongea ukweli kabisa na huo ndio ukweli wenyewe.Mheshimiwa Kafulila alikataa kupokea na kuchukua pesa za mafisadi ili aachane na sakata la Escrow.lakini kwa uzalendo na msimamo mkali alikataa kabisa pesa hizo chafu na akaamua kuendelea na msimamo wake uliokuwa unaungwa mkono na mamilioni ya watanzania waliokuwa nyuma yake.
 
Mimi ni mtetezi wa wazalendo.sisiti wala sioni haya wala aibu kuwaunga mkono WAZALENDO aina ya Mheshimiwa CHUMA Mwenyewe David Kafulila. Naomba tuendelee kuwaunga mkono na kuwatia moyo watu kama MheshimiwaKafulila
hujaweka mawasiliano tatizo
 
Ilitakiwa uonyeshe kwa hoja nzito na zenye ushahidi kiwa ni wapi nimepotosha.Unabisha kuwa pamba haikuuzwa 2200 kwa kilo wakati Mheshimiwa Kafulila akiwa mkuu wa mkoa? Je wakulima wamewahi kuuza kwa bei hiyo kabla ya Mh Kafulila kufika?
Mwashambwa ni nani alikuaminisha kwamba Mkuu wa mkoa anaweza pandisha bei ya mazao hasa mazao ya biashara (CASH CROPS)? Ulisha wahi sikia kuna Mkuu wa mkoa alipandisha bei ya tumbaku, korosho, katani, kahawa n.k? Kabla hamjasifia muwe mnauliza kwanza mnatia aibu! Kama una ubavu elezea Kafulila alipandishaje bei ya pamba nikufumue humuhumu ndani.
 
Mwashambwa ni nani alikuaminisha kwamba Mkuu wa mkoa anaweza pandisha bei ya mazao hasa mazao ya biashara (CASH CROPS)? Ulisha wahi sikia kuna Mkuu wa mkoa alipandisha bei ya tumbaku, korosho, katani, kahawa n.k? Kabla hamjasifia muwe mnauliza kwanza mnatia aibu! Kama una ubavu elezea Kafulila alipandishaje bei ya pamba nikufumue humuhumu ndani.
Ngoja kwanza arudi Kwa mtu aliyemtuma Ili ampe ufafanuzi. Kimsingi huyu chawa Hana uwezo wa kujibu Hilo swali.

Nimemuuliza swali kama Hilo akakimbilia kusema eti 70% ya Pamba inatoka Simiyu!!

Chawa wa siku hizi unamuandikia tu maneno kisha yeye ndo anapost!! Ndo kazi ya huyu mtumwa
 
Ndugu zangu Watanzania,

Uongozi ni kuacha alama zinazoishi katika Maisha na mioyo ya watu, ni kuacha kitu kitakacho simuliwa vizazi kwa vizazi,ni kuacha rekodi ambayo itaimbwa na kuzungumzwa na watu kwa miaka mingi hata kama wewe utakuwa haupo uongozini au Duniani lakini utaendelea kuishi na watu japo hupo Duniani au madarakani.

Uongozi siyo habari ya umeongoza miaka mingapi au umekaa miaka mingapi. kinachomfanya mtu akakumbukwa na watu ni kazi alizozifanya kwa muda alipokuwa na madaraka au hai na faida ya uhai wake kwa watu na uongozi wake ulivyogusa maisha ya watu.

Ndio maana leo hii viongozi na watu kama John F Kennedy, Dr Martin Luther King Junior, BoB Marely, Abraham Lincolin wanaendelea kukumbukwa na watu wengi sana Duniani kwote licha ya kwamba walikufa miaka mingi na waliishi miaka michache Duniani kabla ya kufikia uzee wao. Ndio maana pia viongozi kama Edward Moringe Sokoine wanakumbukwa na Taifa letu japo walikaa madarakani kwa Muda mfupi lakini historia zao na majina yao yameganda na kunasa katika mioyo ya watanzania kutokana na mikono yao na kazi zao kugusa maisha ya watu na kuleta matokeo Chanya.

Hii maana yake nini? Unaweza kuongoza kwa miaka mingi, kukaa madarakani au kwenye cheo fulani kwa miaka mingi na bado usikumbukwe na yeyote yule pale ambapo utaondoka leo. Unaweza kuondoka leo kwenye ukuu wa mkoa au uwaziri au uwaziri mkuu au uspika au ukurugenzi wa taasisi fulani halafu kesho watu wakasahau kabisa kama ulikuwepo kwenye nafasi fulani. Kwanini? Kwa sababu uongozi wako na uwepo wako kwenye kiti haukugusa wala kubadilisha maisha ya watu au mtu yeyote yule, kwa hiyo ulikuwa kama mvuke au moshi tu ambao umekuja na kupita.

Mheshimiwa David Kafulila licha ya kukaa katika nafasi ya Ukuu wa mkoa Wa Simiyu kwa muda mfupi lakini bado anaendelea kukumbukwa na wana Simiyu kama mkuu wa mkoa aliyeleta tabasamu, furaha, matumaini na kuwainua kiuchumi kwa kupaisha Bei ya pamba yao ambayo kwa karibu 70% ya pamba yote Tanzania inatokea Simiyu kufikia bei ya 2200 kwa kilo, bei ambayo haikuwa kutokea tangia Nchi yetu ipate uhuru. Leo anakumbukwa na kusemwa kuwa hapa Simiyu kilipita na kulipita CHUMA David Kafulila aliyeleta Nuru kwa wakulima na maendeleo kwa kaya za wanasimiyu.

Jiulize wewe kiongozi uliyepo kwenye cheo fulani au wadhifa fulani ukiondoka leo kwenye nafasi uliyopo watu watakukumbuka kwa lipi? Umegusa maisha ya watu wangapi? Umeleta tabasamu kwa kaya ngapi? Wangapi wamepata nuru kutoka gizani? Wangapi wamepata matumaini kupitia mikono yako? Wangapi wanatamani urejee au urudishwe au uongezewe muda au kukuombea dua na maombi mema ya kurejea au kupata cheo kikubwa au nafasi fulani? Utakumbukwa kwa lipi ndugu yangu? Au unaisha na kufanya kazi ilimradi tu watoto wako wapate ugali mezani? Umebadilisha maisha ya wangapi?

Wangapi wanaona uwepo wako hapo ulipo ni baraka na mlango wa wao kutokea kimaisha na kuinuka kiuchumi? Wangapi wanakukumbuka kwa mema?

Gusa maisha ya watu, Leta tabasamu kwa watu,washa taa kwenye mioyo ya watu,inua watu,shika mikono ya watu uwainue juu,wape matumaini watu ili siku moja Ukumbukwe kama ilivyo kwa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere,Nelson Mandela,kwame Nkrumah, Keneth Kaunda, Winnie Mandela na wengine wengi sana. Lakini pia ukifanya vyema utaungwa mkono ukiwa bado hai kama ilivyo kwa Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Mwamshamba & Kafulila
 
Mwashambwa ni nani alikuaminisha kwamba Mkuu wa mkoa anaweza pandisha bei ya mazao hasa mazao ya biashara (CASH CROPS)? Ulisha wahi sikia kuna Mkuu wa mkoa alipandisha bei ya tumbaku, korosho, katani, kahawa n.k? Kabla hamjasifia muwe mnauliza kwanza mnatia aibu! Kama una ubavu elezea Kafulila alipandishaje bei ya pamba nikufumue humuhumu ndani.
Tumia akili,

RC amethibiti Ulanguzi aki-create scarcity kwa wanunuzi wakaanza kupambana kupata mzigo ndio wao wenyewe wakaongeza bei.

Scarce and availability
 
Mnabubujikwa na machozi,

Huku Pamba mnauza 800,

Mnabubujikwa na machozi huku watu wanawalangua wakulima Pamba zao.

Mnabubujikwa na machozi huku CHICCO wanatengeneza barabara ya udongo badala lami,

Nyie mnabubujikwa na machozi tu duuuh.

Simiyu mmetisha.

Endeleeni kububujikwa na machozi mama atamrudisha naamini.
Tumbili hatakiwi huku sisi mtu mpenda sifa na maneno kibao kujifanya msomi hatumtaki
 
Mwashambwa ni nani alikuaminisha kwamba Mkuu wa mkoa anaweza pandisha bei ya mazao hasa mazao ya biashara (CASH CROPS)? Ulisha wahi sikia kuna Mkuu wa mkoa alipandisha bei ya tumbaku, korosho, katani, kahawa n.k? Kabla hamjasifia muwe mnauliza kwanza mnatia aibu! Kama una ubavu elezea Kafulila alipandishaje bei ya pamba nikufumue humuhumu ndani.
Swali lako lilitakiwa uulize ni vipi alipandisha bei akiwa mkuu wa mkoa.lakini umetanguliza jibu lako kuwa hawezi.basi baki gizani .lakini wana Simiyu wanafahamu vyema ni vipi chuma David Kafulila alipandisha beo ya Pamba mkoani Simiyu
 
Tumbili hatakiwi huku sisi mtu mpenda sifa na maneno kibao kujifanya msomi hatumtaki
Mheshimiwa Kafulila ni mtu mnyenyekevu,mpole,mkarimu, mzalendo na mwenye usikivu wa hali ya juu sana kwa kila mtu pasipo kujali hali ya mtu au cheo cha mtu.
 
Back
Top Bottom