David Kafulila atolea ufafanuzi wa Adani kuwekeza katika Miundombinu ya Umeme kwa Ubia

David Kafulila atolea ufafanuzi wa Adani kuwekeza katika Miundombinu ya Umeme kwa Ubia

Napata shida kukosoa au kukubali huu mradi sababu sijui wamekuja na na hoja gani kutofautisha na walipo kwama serikali kwenye usafirishaji umeme.
Huenda wana jipya au hawana jipya ni miradi ya watu waliomo serikalini. i.e 10% au Wana hisa humo.
Kuweka wazi mapema habari hii kunasaidia watu wanao ijua hiyo kampuni kuweka matatizo yao bayana.
Hapa sio 10% Bali zaidi ya hapo na ni kwa hiyo miaka 30 na uwezekano wa kuendelea. "Wahuni" hawana nia njema na hili taifa bali wana nia njema na mafisudi.
 
Acha uongo na uzushi wako
Sasa dhumuni la kufanya hivyo ni nini ?? Ikiwa aliyewekeza atapata faida, lakini Sisi hatuitaki hiyo faida, matokeo yake ndio hayo ya kuitwa "wahuni" au hamjui mko hapo kufanya nini
 
Ridiculous.

Wanachokuja kuwekeza ni nini wakati Nchi imesha wekeza matrilioni ya fedha humo?

Ni nini haswa hawa wawekezaji wanaleta ambacho hakipo kwenye huo mfumo wa Usambazaji wa Umeme?

Itoshe, nilishasema hapa wakati tunailalamikia serikali na Uwekezaji wa DP World Bandarini.

Ukoloni mamboleo is Real.

=========
Hatahivyo. Kuna shida gani wakipewa kampuni za wazawa kufanya 'Distribution"?
Hilo ulilosema Mwisho ndio linatakiwa la kampuni ya wazawa na hisa ziwe DSE
 
Ndugu zangu Watanzania,

Kampuni mbili kubwa, Adani Group ya India na Gridworks Development Partners LLP ya Uingereza, zimeonesha nia ya kuwekeza katika mradi wa kusafirisha umeme nchini Tanzania kupitia mfumo wa ubia. Mradi huo unalenga kujenga njia za kusafirisha umeme wa juu kwa lengo la kuboresha miundombinu ya nishati nchini Tanzania.

Akizungumza kwa njia ya simu na Jambo TV, David Kafulila, Kamishna wa Ubia wa Sekta ya Umma na Binafsi (PPP), amefafanua kuwa utaratibu huo unajulikana kama "expression of interests,"ambapo wawekezaji wanaweza kueleza nia yao ya kuwekeza kwenye miradi kwa kushirikiana na serikali.

"Kampuni (Wawekezaji) mbili ambazo zimeomba kufanya mradi wa kusafirisha umeme kwa utaratibu wa ubia, inaitwa expression of interests yaani kwamba inaruhusu mwekezaji kueleza nia yake ya kuwekeza kwenye mradi fulani katika utaratibu wa ubia na serikali" ameeleza Kafulila.

Kafulila ameeleza zaidi kuwa sheria za ubia nchini Tanzania zinaruhusu kampuni kuwasilisha maombi yao kwa hatua za awali, na serikali inaweza kuamua kuitangaza miradi hiyo kwa kampuni zingine kushindana ili kuhakikisha uwazi na ufanisi. Hivi sasa, Adani na Gridworks ndio kampuni mbili zilizowasilisha maombi ya kuwekeza katika mradi huo wa kusafirisha umeme.

Ameongeza kuwa zipo njia nne zinazotumika kuingia kwenye ubia wa umma na binafsi nchini Tanzania. Njia hizo ni pamoja na serikali kutangaza mradi na kuruhusu ushindani (Solicited), mwekezaji kuomba kuandaa mradi (Unsolicited), serikali kutafuta mwekezaji wa moja kwa moja wa haraka hasa baada ya kuwa tayari imeandaa mradi (Direct Negotiation), na ya utaratibu maalum (Special Arrangement). Katika kesi ya Adani na Gridworks, wameomba kuwekeza kupitia njia ya kusudio la mwekezaji (Unsolicited).

Kafulila amesisitiza kuwa maombi yaliyotolewa na Adani na Gridworks ni hatua ya awali, na michakato ya kuchunguza kama kampuni hizo zina sifa stahiki itaendelea. Serikali kupitia TANESCO itazingatia mahitaji ya mradi huo na kuamua kama kutangaza zabuni kwa kampuni zingine au kuendelea na kati ya waombaji wa sasa.

"Adani ameleta kusudio awekeze, ni hatua ya awali ya kueleza kusudio, na siyo Adani peke yake ambayo imeomba iwekeze, sasa baadaye kwa mujibu wa sheria TANESCO sasa inaweza ikaamua kutangaza na kampuni zote ambazo zinahitaji zikashindana kutegemea mahitaji yake kwa wakati huo. Sasa hiyo iliyofanyika ya Adani na Kampuni nyingine ya Uingereza ya Gridworks Development Partners LLP, ni kampuni mbili ambazo zimeomba kuwekeza, na sheria inawaruhusu kuomba. Sasa ukiomba, ndiyo michakato inaanza ya kama una sifa au hauna sifa", ameeleza Kafulila.

Adani Group, kampuni inayoongozwa na bilionea Gautam Adani, imekuwa ikiongeza uwepo wake katika ukanda wa Afrika Mashariki, huku Tanzania ikiwa sehemu ya mikakati yao ya kuimarisha miundombinu ya nishati kupitia mradi unaotajwa kuwa na thamani ya takriban dola milioni 900. Tanzania pia iko kwenye mazungumzo na Gridworks Development Partners kuhusu mradi wa dola milioni 300.

Kwa upande wake, Tanzania imeweka kipaumbele katika kuboresha miundombinu ya nishati ili kukidhi mahitaji ya umeme yanayoendelea kuongezeka, hatua inayosaidiwa na miradi kama hii ya ubia. Ushirikiano huu pia ni muhimu kwa kuboresha mfumo wa usafirishaji wa umeme wa juu nchini.View attachment 3116153
Wizi mwingine unaenda kutengenezwa in the name of ubia. Hatuna rangi tutaacha kuona
 
Kanji akiwekq kibunda chake $900 million unadhani anategemea kupata hasara!? Hapo mnaelewa kuwa huyu faida yake ni kiasi gani na kwa muda gani!?? Gautam Adani atawanyoosha!
 
Hapa kafulila umechemka ,yaani kusafirisha tu serikali kupitia REA hawawezi? Wizzy Wiizy.

Kama DERM ameweza kutengeneza nguzo na kuna kampuni hapa hapa nchini zinatengeneza transforma na nyaya ,kwanini tusiwape hao na serikali iwe inawalipa kidogo kidogo kuliko kwenda kumpa muhindi aliyefukuzwa kenya kuja kutupiga kama HABINDA SINGI?
Nchi hii tuna wajinga wengi sana! Sasa Lucas Mwashambwa the headless chicken anashabikia nini hiki?
 
REA wameweza kusambaza Umeme nchi nzima vijijini kwa pesa za Tanzania wapewe kazi ya kujenga miundombinu kusambaza hatutaki matapeli kupitia PPP

Kazi kubwa iko kwenye kuzalisha umeme Tanesco imeweza

Sasa huku kwenye duka la rejareja la kusambaza umeme tu kama kusambaza tu gesi ya kupikia na majiko yake ndio tushindwe locally?
Mbona REA wameweza kusambaza Umeme vijijini kuliko kugumu kama nini

Haya mambo ya kuleta PPP kwenye miradi kama ya usambazaji umeme ambayo REA wameonyesha uwezo mkubwa kusambaza hadi sehemu zisizofikika kwa usafiri wowote nchi nzima tena kwa pesa za Tanzania kuanzia nguzo, nyaya transformer nk

Huyo anayetaka kuleta kampuni ya kigeni ilipwe dola ambazo kwa sasa dola hatuna ukienda benki shida nani huyo hasa ?

Kampuni nyingi mfano za China zinazojenga miradi mikubwa Tanzania ni za serikali ya China zikiwemo zinazojenga reli ya SGR zina ufanisi

Sasa REA wameonyesha uwezo mkubwa wa wazi huyo msambazaji wa kutaka PPP anataka kusambaza kupeleka wapi? Mijini Tanesco wamekumudu vizuri tu ,vijijini wasambaza umeme REA wamemudu huyo wa PPP anataka kusambaza umeme kupeleka wapi ambako Tanesco na REA hawajaweza?
 
Ndugu zangu Watanzania,

Kampuni mbili kubwa, Adani Group ya India na Gridworks Development Partners LLP ya Uingereza, zimeonesha nia ya kuwekeza katika mradi wa kusafirisha umeme nchini Tanzania kupitia mfumo wa ubia. Mradi huo unalenga kujenga njia za kusafirisha umeme wa juu kwa lengo la kuboresha miundombinu ya nishati nchini Tanzania.

Akizungumza kwa njia ya simu na Jambo TV, David Kafulila, Kamishna wa Ubia wa Sekta ya Umma na Binafsi (PPP), amefafanua kuwa utaratibu huo unajulikana kama "expression of interests,"ambapo wawekezaji wanaweza kueleza nia yao ya kuwekeza kwenye miradi kwa kushirikiana na serikali.

"Kampuni (Wawekezaji) mbili ambazo zimeomba kufanya mradi wa kusafirisha umeme kwa utaratibu wa ubia, inaitwa expression of interests yaani kwamba inaruhusu mwekezaji kueleza nia yake ya kuwekeza kwenye mradi fulani katika utaratibu wa ubia na serikali" ameeleza Kafulila.

Kafulila ameeleza zaidi kuwa sheria za ubia nchini Tanzania zinaruhusu kampuni kuwasilisha maombi yao kwa hatua za awali, na serikali inaweza kuamua kuitangaza miradi hiyo kwa kampuni zingine kushindana ili kuhakikisha uwazi na ufanisi. Hivi sasa, Adani na Gridworks ndio kampuni mbili zilizowasilisha maombi ya kuwekeza katika mradi huo wa kusafirisha umeme.

Ameongeza kuwa zipo njia nne zinazotumika kuingia kwenye ubia wa umma na binafsi nchini Tanzania. Njia hizo ni pamoja na serikali kutangaza mradi na kuruhusu ushindani (Solicited), mwekezaji kuomba kuandaa mradi (Unsolicited), serikali kutafuta mwekezaji wa moja kwa moja wa haraka hasa baada ya kuwa tayari imeandaa mradi (Direct Negotiation), na ya utaratibu maalum (Special Arrangement). Katika kesi ya Adani na Gridworks, wameomba kuwekeza kupitia njia ya kusudio la mwekezaji (Unsolicited).

Kafulila amesisitiza kuwa maombi yaliyotolewa na Adani na Gridworks ni hatua ya awali, na michakato ya kuchunguza kama kampuni hizo zina sifa stahiki itaendelea. Serikali kupitia TANESCO itazingatia mahitaji ya mradi huo na kuamua kama kutangaza zabuni kwa kampuni zingine au kuendelea na kati ya waombaji wa sasa.

"Adani ameleta kusudio awekeze, ni hatua ya awali ya kueleza kusudio, na siyo Adani peke yake ambayo imeomba iwekeze, sasa baadaye kwa mujibu wa sheria TANESCO sasa inaweza ikaamua kutangaza na kampuni zote ambazo zinahitaji zikashindana kutegemea mahitaji yake kwa wakati huo. Sasa hiyo iliyofanyika ya Adani na Kampuni nyingine ya Uingereza ya Gridworks Development Partners LLP, ni kampuni mbili ambazo zimeomba kuwekeza, na sheria inawaruhusu kuomba. Sasa ukiomba, ndiyo michakato inaanza ya kama una sifa au hauna sifa", ameeleza Kafulila.

Adani Group, kampuni inayoongozwa na bilionea Gautam Adani, imekuwa ikiongeza uwepo wake katika ukanda wa Afrika Mashariki, huku Tanzania ikiwa sehemu ya mikakati yao ya kuimarisha miundombinu ya nishati kupitia mradi unaotajwa kuwa na thamani ya takriban dola milioni 900. Tanzania pia iko kwenye mazungumzo na Gridworks Development Partners kuhusu mradi wa dola milioni 300.

Kwa upande wake, Tanzania imeweka kipaumbele katika kuboresha miundombinu ya nishati ili kukidhi mahitaji ya umeme yanayoendelea kuongezeka, hatua inayosaidiwa na miradi kama hii ya ubia. Ushirikiano huu pia ni muhimu kwa kuboresha mfumo wa usafirishaji wa umeme wa juu nchini.View attachment 3116153
Bado haya maneno yanatakiwa kutoka tanesco na bodi yao
 
Back
Top Bottom