Davido kaikataa Afrika na nchi yake Nigeria

Davido kaikataa Afrika na nchi yake Nigeria

CARIFONIA

JF-Expert Member
Joined
Aug 17, 2013
Posts
616
Reaction score
1,453
Msanii maarufu wa Afrobeats, Davido, ameibua gumzo baada ya kutoa tahadhari kali kwa Waafrika walioko ughaibuni na Wamarekani Weusi wanaopanga kuhamia Afrika. Katika mahojiano ya hivi karibuni kwenye podcast ya Big Homies House, Davido alisema wazi kwamba hali si shwari barani Afrika, hasa nchini mwake Nigeria.

Akitolea mfano wa Nigeria, alifafanua kuwa licha ya kuwa mzalishaji mkubwa wa mafuta, wananchi wanalipa bei ya juu kuliko nchi zinazolazimika kuagiza mafuta hayo kutoka nje. "Uchumi uko kwenye mtikisiko mkubwa, na kiwango cha kubadilisha fedha kimevurugika vibaya," alisema msanii huyo.

Davido pia aliongeza kuwa tasnia ya burudani kama muziki wa Afrobeats inafanya Afrika ionekane nzuri machoni pa ulimwengu, lakini hali halisi ni tofauti kabisa. "Hatuwezi kufurahia rasilimali zetu wenyewe. Ninapokuwa nyumbani, huwa sionyeshi sehemu mbaya za maisha, lakini ukweli ni kwamba uongozi wetu haujafikia kiwango kinachohitajika," aliongeza.

Huku akiweka wazi kuwa hataki kuharibu sura ya Afrika, Davido aliwataka wale wanaofikiria kuhamia bara hilo kufikiria tena mpaka hali itakapokuwa bora.

1000034620.jpg
 
Davido ni mmarekani na nyumbani kwao Atlanta. Kuhusu hali mbaya ya uchumi Afrika, sijui nani amfunge paka kengele? Watu wote tunajua kwamba bado tunatawaliwa lakini tunajifanya vipofu na kukalia politic tu.
Hatutawaliwi mkuu ila viongozi wazembe na wasiowajibika kama wa CCM wanataka kuwaaminisha watu kuwa tunatawaliwa ili kukwepa lawama mbona wale wa north Africa kama Morocco, Algeria na Libya hawana maisha kama yetu?
 
Hajaikataa afrika Bali kasema ukweli wenyewe.Mfano tu hapa Tanzania tunanunua mafuta(petroli,diseli n.k)Kwa bei kubwa kuliko Zambia ,Uganda na Rwanda ambao hupitisha mafuta Yao hapa hapa Tanzania.Afrika ina viongozi wengi vichaa.
 
Hatutawaliwi mkuu ila viongozi wazembe na wasiowajibika kama wa CCM wanataka kuwaaminisha watu kuwa tunatawaliwa ili kukwepa lawama mbona wale wa north Africa kama Morocco, Algeria na Libya hawana maisha kama yetu?

Kama unabisha Africa haijapata uhuru basi hujui siasa na mfumo mzima wa kiuchumi wa bara letu. Kwanza lini viongozi wa CCM wametuaminisha kama tunatawaliwa?

Tusipokubaliana kwa hili tutabaki kuwa kama tulivyo milele. Viongozi wa kiafrika si wazembe, ni wawajibikaji lakini wanawajibika kwa ajili ya bwana zao mabepari si waafrika. Wanaongoza mataifa huku wakiwa na hofu ya kuondolewa madarakani wasipotii matakwa ya wazungu.

Tunaongozwa na mfumo tuliopangiwa na walewale waliotutawala. Wametutawala miaka na miaka mpaka leo hawajatulipa fidia na bado wanatudai lakini hata Mbowe sijawahi kumsikia ameongelea hili swala.
Mavuno na malighafi zetu zinawafaidisha wazungu sisi tunabaki bila kitu nani hajui?

Ibrahim Traore kachukua Bukina Faso kutoka kwenye mikono ya Ufaransa na wote tunajua udhalimu wa wafaransa kwa waafrika, ni kiongozi gani Samia, Ruto au Kagame aliyemuunga mkono? Wanaogopa kufukuzwa kazi. Na ndio ujue sisi bado tunatawaliwa, sio CCM tu yoyote atakayechukua nchi hawezi kwenda kinyume na mfumo huu. Hata akija Mbowe lazima atapanda ndege aende Washington DC akapige picha na Trump
 
Kama unabisha Africa haijapata uhuru basi hujui siasa na mfumo mzima wa kiuchumi wa bara letu. Kwanza lini viongozi wa CCM wametuaminisha kama tunatawaliwa?

Tusipokubaliana kwa hili tutabaki kuwa kama tulivyo milele. Viongozi wa kiafrika si wazembe, ni wawajibikaji lakini wanawajibika kwa ajili ya bwana zao mabepari si waafrika. Wanaongoza mataifa huku wakiwa na hofu ya kuondolewa madarakani wasipotii matakwa ya wazungu.

Tunaongozwa na mfumo tuliopangiwa na walewale waliotutawala. Wametutawala miaka na miaka mpaka leo hawajatulipa fidia na bado wanatudai lakini hata Mbowe sijawahi kumsikia ameongelea hili swala.
Mavuno na malighafi zetu zinawafaidisha wazungu sisi tunabaki bila kitu nani hajui?

Ibrahim Traore kachukua Bukina Faso kutoka kwenye mikono ya Ufaransa na wote tunajua udhalimu wa wafaransa kwa waafrika, ni kiongozi gani Samia, Ruto au Kagame aliyemuunga mkono? Wanaogopa kufukuzwa kazi. Na ndio ujue sisi bado tunatawaliwa, sio CCM tu yoyote atakayechukua nchi hawezi kwenda kinyume na mfumo huu. Hata akija Mbowe lazima atapanda ndege aende Washington DC akapige picha na Trump
Huo ni uongo hao wafaransa walikuepo hapo Kwa matakwa ya watawala waliopita kabla ya huyo traore hayo ya kupiga picha na hiyo mifumo ni nadharia tu hakuna ushahidi wowote
 
Huo ni uongo hao wafaransa walikuepo hapo Kwa matakwa ya watawala waliopita kabla ya huyo traore hayo ya kupiga picha na hiyo mifumo ni nadharia tu hakuna ushahidi wowote

Kama hujui kitu achana na hizi mada nyingine zilizokuzidi.
 
Msanii maarufu wa Afrobeats, Davido, ameibua gumzo baada ya kutoa tahadhari kali kwa Waafrika walioko ughaibuni na Wamarekani Weusi wanaopanga kuhamia Afrika. Katika mahojiano ya hivi karibuni kwenye podcast ya Big Homies House, Davido alisema wazi kwamba hali si shwari barani Afrika, hasa nchini mwake Nigeria.

Akitolea mfano wa Nigeria, alifafanua kuwa licha ya kuwa mzalishaji mkubwa wa mafuta, wananchi wanalipa bei ya juu kuliko nchi zinazolazimika kuagiza mafuta hayo kutoka nje. "Uchumi uko kwenye mtikisiko mkubwa, na kiwango cha kubadilisha fedha kimevurugika vibaya," alisema msanii huyo.

Davido pia aliongeza kuwa tasnia ya burudani kama muziki wa Afrobeats inafanya Afrika ionekane nzuri machoni pa ulimwengu, lakini hali halisi ni tofauti kabisa. "Hatuwezi kufurahia rasilimali zetu wenyewe. Ninapokuwa nyumbani, huwa sionyeshi sehemu mbaya za maisha, lakini ukweli ni kwamba uongozi wetu haujafikia kiwango kinachohitajika," aliongeza.

Huku akiweka wazi kuwa hataki kuharibu sura ya Afrika, Davido aliwataka wale wanaofikiria kuhamia bara hilo kufikiria tena mpaka hali itakapokuwa bora.

View attachment 3169181
Ameongea ukweli
 
Kama hujui kitu achana na hizi mada nyingine zilizokuzidi.
Wewe ndo hajui kitu unasikiliza propaganda umasikini wetu unasabishwa na uzembe na ufisadi wa viongozi au unataka kusema wakoloni ndo wanakwambia watawala wa Africa wawe mafisadi?
 
Back
Top Bottom