Davis Mosha akusanya zaidi ya milioni 400 kanisa la KKKT-Arusha Mjini

Davis Mosha akusanya zaidi ya milioni 400 kanisa la KKKT-Arusha Mjini

babi

Member
Joined
Jul 24, 2012
Posts
79
Reaction score
109
Mfanyabiashara Davis Mosha leo ameongoza Harambee ya ujenzi wa Kanisa, Katika misa ya harambee hiyo iliyoendeshwa katika Kanisa la KKKT usharika wa Arusha Mjini, Davis Mosha aliyeongozana na Familia yake aliweza kuchangisha jumla ya kiasi cha Shilingi Milioni mia nne.

Akizungumza katika Hafla hiyo fupi kanisani hapo, Davis Mosha alisema yeye pamoja na rafiki zake aliowashirikisha kwa Muda mchache baada ya kujua hitaji la kanisa hilo waliweza kumuunga mkono na kumuomba Mchango wao utambuliwe kama sadaka katika kufanikisha lengo hilo la kanisa. Huku akiahidi kuendelea kuwa bega kwa bega na kanisa hilo mpaka kuhakikisha lengo kuu linakamilika kwa kiwango kinachohitajika.

"Leo kupitia waumini wenzangu pamoja na Rafiki zangu tumeweza kukusanya zaidi ya Shilingi Milioni Mia nne, Huu mi mwanzo mzuri katika Ujenzi wa kanisa na kukuza huduma ya kanisa, Nitoe wito kwa yeyote atakayeguswa kushiriki katika jambo hili basi ajiungane nasi katika kukamilisha kazi ya Mungu." Alisema Davis Mosha.

Ikumbukwe kuwa Mfanyabiashara Davis Mosha amekua Mstari wa mbele katika kujitoa katika ujenzi wa nyumba za ibada ikiwemo Misikiti na Makanisa katika maeneo mbalimbali

IMG-20211114-WA0000.jpg
 
Hamna lolote hapo, mahekalu ya Mungu wa kweli ni matumbo ya yatima, wajane, viwete, masikini, wagonjwa wafungwa n.k

Majengo hat kina farao waliacha pyramids na mahekalu ya mawe. Hapo ni lichaka la kujifichia maovu nyuma ya pazia na mabilionea wa Arusha wanauweza sana huu mchezo.
 
Hamna lolote hapo, mahekalu ya Mungu wa kweli ni matumbo ya yatima, wajane, viwete, masikini, wagonjwa wafungwa n.k

Majengo hat kina farao waliacha pyramids na mahekalu ya mawe. Hapo ni lichaka la kujifichia maovu yuma ya pazia.
Amejenga vituo vya watoto yatima, ana Centre zaidi ya 10 anazihudimia

Sent from my SM-G980F using JamiiForums mobile app
 
Amejenga vituo vya watoto yatima, ana Centre zaidi ya 10 anazihudimia

Sent from my SM-G980F using JamiiForums mobile app
Yatima hawaishi kama ambavyo kipato chake kinavyoongezeka, mahekalu yanayokaa wazi wiki nzima kusubiri ibada mara moja kwa juma ni upuuzi wakati kuna watoto bado wengi mitaani.

Kwanza hizo sadaka za kujitangaza wakati Biblia yao inawataka mkono wa kushoto ukitoa wakulia usijue naamini hawajaisoma vizuri! Mbele ya fedha hata askofu aweza pindisha maandishi.
 
Yatima hawaishi kama ambavyo kipato chake kinavyoongezeka, mahekalu yanayokaa wazi wiki nzima kusubiri ibada mara moja kwa juma ni upuuzi wakati kuna watoto bado wengi mitaani.

Kwanza hizo sadaka za kujitangaza wakati Biblia yao inawataka mkono wa kushoto ukitoa wakulia usijue naamini hawajaisoma vizuri! Mbele ya fedha hata askofu aweza pindisha maandishi.
Wivu tu; tumbo la kuhara litakumaliza mwanakwetu; kila mtu aishi apendavyo
 
Back
Top Bottom